Kwanini Rais analazimisha kuungwa mkono?

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,243
103,945
Katika maisha ya kawaida mtu unaweza kumlisha,kumpeleka chooni,kumuogesha,kumvisha nk lakini bado akakununia na kukusema vibaya kwa watu. Ndani ya familia mke anaweza kumpa mumewe kila kitu,lakini bado akadundwa na familia ikaendelea. Hizi ni principles za kawaida kabisa.

Sasa iweje katika nchi ya kidemokrasia rais alazimishe watu kumuunga mkono.

Je, rais hatambui mawazo kinzani na mbadala.Hivi kweli hakuna jema ambalo linaweza kupatikana katika kupigwa huko?Mbona Tundu Lissu akimpinga Rais lakini leo hii tunaona mnapita mlemle?

Kinachonishangaza zaidi ni rais kuhusisha "Mashehe wa Lowasa" na matukio ya Kibiti!

Ndugu yangu tema chini.
Siasa na madaraka sio jambo la kujidai nalo leo ni hisia na miongozo ya kibinadamu.

Miaka 20 iliyopita mtu angemuuliza Lowasa kuwa kuna siku chama cha CCM kitageuka kuwa ni mtesaji wake mkuu na watawala aliofanya nao kazi kwa umoja na kutembea kifua mbele kama marafiki na mara nyingine kuwasaidia kwenye majimbo yao mpaka wakashinda ubunge angepinga vijali na mara nyingine ungeitwa mchochezi na mfitinishi tena unataka kuwagambanisha viongozi na chama chao.
Tafakari!!!
Leo hii Lowasa na wengineo wamekua ni wahanga juu ya matamshi yao amaboyo mara nyingine wanayatoa kwa nia njema wakiamini kuwa wanawaambia watu miaka mitano iliyopita walikuwa marafiki na watawala pamoja.
Tafakari!!!!!!!!!
Usijivunie kile unachokishabikia leo hata kama kina kiuka haki za wengine. Ni bora ukae kimya mana ni wazi kuwa wanayoyasema wale usiowakubali yapo mengine yana ukweli na hekima na yanazungumzwa na jamii pana.

Suala la mtu kukaa gerezani tu bila kuhukumiwa kwa miaka nenda rudi wen lisikie tu kwa watu wengine lakini omba Mungu sana ili akuepushe na balaa hilo na pia onyesha huruma kwa hao wanaofanyiwa hivyo mana nao mara nyingine hawakupenda ila tu yamewakuta kutokana na tofauti za kiimitizamo tu.
Tofauti hizo hizo kama zitaendelea ipo siku utajikuta uko upande wa pili wa kupingana na wale usio wataka leo huku wao wakiwa na mamlaka ya kukufanyia hayo unayoona ni haki wao kufanyiwa leo.
Ndio maana watu wengi wasioamini sana katika vyama na itikadi za vyama vya kisiasa wanapigania suala la Haki za Binadamu na utawala bora wa kusimamia katiba na sheria zilizopo. Wanajua kuwa Mahakama ndicho chombo pekee cha kutoa haki na sio vinginevyo. Wanajua kuwa watu wanaweza kwa makusudi kuchochea na kuharibu tamko lenye nia njema ya mtu yeyote na hata kumuangamiza kwa makusudi kwa sababu tu ya chuki. Lakini endapo mtu atafikishwa mahakamani basi mahakama inatoa nafasi ya kusikiliaza na kuchambua ili kujua nia ovu ya mtu ya kauli au kitendo kuliko kuwaacha tu watawala wakaamua na kuhukumu juu ya wale wasio wapenda. Sio jambo zuri sana kisiasa na kijamii.

Ni vizuri kila mtu akafuata sheria na kuheshimu vyombo vya dola. Lakini pia vyombo vya dola viheshimu haki za mtu mstarabu ambaye hajafanya ukaidi. Mtu aliwa matarabu asifanyiwe ukatili kwa sababu tu ya kuwafurahisha watawala
Hayo yalifanywa wakati wa Yesu alikuwa mtu mstarabu lakini alitendewe unyama na kuuawa kwa ajili ya watawala wa enzi hizo kutaka kulinda madaraka na himaya zao.
 
mmelazimusha maandamano sasa iko wapi habari ya mikataba si tuliwaambia hamuwezi kugusa mkigusa mnashtakiwa leo prof. kabudi kamakiza mna lingine la kuongeza kiki zingine za jitoto sana mmeumbuka sana
 
Kuna msemo unaosema kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza.......

Hivi kama kweli serikali ya CCM ya awamu ya 5 wanaamini kuwa wanaungwa mkono na Umma wa watanzania, mbona wamekuwa waoga mno kwa kuamua kuufanya uwanja wa siasa kutokuwa sawa, kama vile wao CCM kupitia kwa Mwenyekiti wao wa Taifa kutumia media za Umma kukinadi chama chake cha CCM, wakati amezuia vyama vya upinzani visifanye shughuli zozote za siasa hadi mwaka 2020?

Ni dhahiri vitendo vya vyombo vya dola kuendelea kukipendelea chama cha CCM na kuvikandamiza vyama vya upinzani, kunafanya uwezekano wa vyama vya upinzani kuzoa kura nyingi sana za huruma kwa mwaka 2020.

Ni vyema serikali ya CCM ikaruhusu uwanja sawa wa ushindani wa kisiasa, ambapo wananchi ndiyo watakuwa waamuzi wa kujua upi mchele na ipi pumba.......
 
Ujui chochote na ningumu kumuelewa rais kwasababu wewe mwenyewe unaishi kama bendera na ujamuelew chochote ivi ufikili tanzania ina mashekhe wangapi kwa nini wawe wao.kwaupande walowasa bado ni mnafki na unafki wake utamuweka pabaya uzur rais anatoa onyo kabla sasa aendele na ujinga wake
 
Nguvu anayoitumia kutaka kuungwa mkono ndio itakayolibomoa taifa
 
Back
Top Bottom