Kwanini Nyerere hakumkubali Lowassa?


mbona wengi wanalinda? sio tamaa ya fedha hiyo?
 


Wengi hawana akili hizi mkuu!!! wakiamua kumtusi Nyerere watamtusi weeeeee, mpaka kesho

wako ambao wakiamua kumsifu...watamsifia weeee, mpaka uone mbingu inashuka, kwano Nyerere ni mtume zaidi ya tuwajuao!

kwangu mimi namsifia Nyerere panopibidi....tatizo mambo mengi naona aliharibu sisiti kusema....
 

Hapo sijakusoma vyema, ukimwambia mtu ana chuki binafsi na mtu mwingine umemsema vibaya? Kwa mfano nikisema alikuwa na chuki na Idd Amin ntakuwa nimemsema vibaya. Nikimwambia mtu fulani amekufanyia zengwe nitakuwa nimesema vibaya. Uelewa wako hauna macho mkuu, hujui maana ya maneno mabaya. Nadhani tunazingatia na kufuata sheria na kanuni za JF. Kama kuna maneno mabaya hapo bila shaka wangeifunga thread hii. Nimeandika ninachoamini kuwa kilitokea na huo ndiyo ukweli.
 
Mtalia na kusaga meno! ukweli ni kwamba Lowassa ndiye rais ajaye
Ninyi ndio mnaojidanganya. Watanzania wa leo sio mazuzu tena kama ilivyokuwa 2005, eti chaguo la Mungu. Tutawachambua na kuwajua kwa undani wenu kabla ya kupata tena kura zetu. Lowassa ni zero.
 

Huu ndiyo ubaya wa kukaririshwa mambo. Nakumbuka enzi zile Mwalimu alikuwa akifanya ziara mahali ni lazima kila kitu kifungwe, biashara zisimame, maduka yafungwe, wanafunzi lazima wasitishe masomo wakaimbe kwaya kwa nguvu. Mtu ambaye hataonekana mkutanoni ilikuwa ni lazima akanyee debe. Hayo ni baadhi ya mapungufu katika utawala. Wengi wamebaki na kumbukumbu za ukaririfu. Sasa wakiambiwa ukweli wanakuja juu mithiri ya nyati kichaa aliyejeruhiwa.
 
Lowassa ata umsafishe vipi atabaki kuwa mwizi,acha kupoteza nguvu zako bure..
Kama unabisha tafuta mtoto wa darasa la kwanza njiani kisha muulize "ivi fisadi namba moja nchi hii ni nani?"..alafu utashangaa jinsi atakavokujibu vizuri.

mkuu hii ni kweli. mwanangu wa class two kila akiona mtu mwenye nywele nyeupe anasema ni fisadi el. yaani ni balaa.
 
Lawassa afanye siasa zake bila kumshilikisha Nyerere.
Kama Nyerere alikuwa wrong mbona, el alilazimisha uwaziri mkuu then within just 2 yrz nchi ikawa na marichmond ya ajabu

NYERERE was a VISIONARY leader sidhani kama alimsema vibaya Kikwete ila alisema Kikwete is still young for presidence on 1995 na kama basi alisema Kikwete hafai then Nyerere was Intelligent person kulingana na uongozi mbovu wa Kikwete sasa.

Ila Nyerere alimsema EL kuwa inakuwaje kijana mdogo kama el unapewa uwaziri na muda mfupi tu umekuwa tajiri kiasi hicho? sasa ilikuwa kazi ya el kuprove kwamba utajiri wake ni wa halali, inakuwaje anakuja leo kutuambia Nyerere alikuwa na chuki?
hata leo kwa nn Lowassa asituambie waTz kuwa yeye si fisadi ili tumchague kama anavyotaka?

Lakini Nyerere alimsema pia Malecela kuwa ni mtu alieweza kubadili hata dini yake na kuitwa Abdallah, akasema mtu kama huyu hawezi akapewa Urais anaweza akauza hata nchi.
 
Hapa Tanzania, inahitaji ujasiri wa mwendawazimu, kupambana na Nyerere! Kuwashawishi Watanzania kuyaamini maneno yako, kuliko maneno ya Nyerere, ni sawa na kufanya kazi ya kujaza maji kwenye gunia! Wapiga debe wa EL, ninawashauri mtafute strategy nyingine ya kumsafisha huyo mtu wenu. Mwenye masikio, asikie!
 
lowasa ama watu wooote walio nyuma yake wana usafi gani....?uhalali gani...?umahili gani...? na umakini gani...?wa kulugusa jina la gwiji la siasa za karne yake, mwana halisi wa afrika,mwanafalsafa,mwana jamii na mzalendo halisi wa utu wa mtu, baba wa taifa mwalimu julius kambarage nyerere.....!!!!! wamefanya nini kuthibitiha aliwaandama na alikuwa na chuki...??. kosa mnalo fanya ni kulitumia jina la mwalimu vibaya kutafuta uharali wa kupanda kisiasa, jina hili katu halifungamani na wachafu,halicompromise na wachafu,mafisadi wazandiki,majizi,mafisani,wauwaji,makuhadi,matapeli,wahujumu uchumi,walevi wa madaraka,wenye uchu wa madaraka,wakandamizaji,wahuni,wazurumaji,wabinafsi...........
 
Kwa ninavyo fahamu mimi, chaguo la Nyerere kwenye urais 1995 lilikuwa ni Salim Ahmed.
Bahati mbaya, au nzuri Lyatonga fyatu akajitoa CCM na kurubuni umati lukuki.
Nyerere kuhofia mgawanyiko wa kidini, hasa ukichukulia kuwa rais aliyekuwa anamaliza kipindi, Mwinyi, ni Islam na huko nyuma aliwahi kulumbana na makanisa, Kifimbo akamlazimisha Ben kuchukua form.
 
Hapa Tanzania, inahitaji ujasiri wa mwendawazimu, kupambana na Nyerere! Kuwashawishi Watanzania kuyaamini maneno yako, badala ya maneno ya Nyerere, ni sawa na kufanya kazi ya kujaza maji kwenye gunia!

Kiongozi yeyote lazima atizamwe kwa pande zote mbili katika yale aliyoyafanya. Si kila kitu alichofanya kilikuwa sawa. Lazima uwe na hoja za msingi. Naomba uniambie, kulikuwa na hatia kubwa zaidi ya kuthubutu kusema unataka kuvunja azimio la Arusha mbele ya Nyerere? Lakini lilivunjwa naye akishuhudia. Kulikuwa na hatia kubwa kama kuthubutu kusema unataka muungano ufe? Mbona watu wanapiga kelele muungano ufe? Je kudai serikali ya Tanganyika siyo kupinga msimamo wa Nyerere? Mbona mnapiga kelele kila siku mkidai Tanganyika? Nilichokiandika hapo si ugomvi wala mapambano na Nyerere. Ni mwendelezo wa yale ambayo watanzania wanadai ikiwa ni pamoja na kuua azimio la Arusha, kudai muungano ufe na kutaka iwepo serikali ya Tanganyika. Yote hayo mnayotaka kuyapindua leo si yameasisiwa na Nyerere? Je mimi niliyesema Nyerere alikuwa na chuki binafsi dhidi ya Lowassa. Nina hatia gani kuzidi yule aliyevunja azimio la Arusha, nina hatia gani kuzidi yule anayedai serikali ya Tanganyika ndani ya muungano, nina hatia gani kuzidi yule aliyeizika siasa ya ujamaa na kujitegemea. Fikiri kwa undani zaidi bila kukurupuka.
 

Unadhani kwa nini alimlazimisha badala ya kuacha demokrasia ifuate mkondo wake?
 

Kwa sifa ulizompa mwalimu hapo juu. Watanzania wengi watakuwa wanafiki. Kwa nini leo hamyaenzi mambo yaliyoasisiwa na gwiji leo mnataka kuyabomoa. Azimio la Arusha si limevunjwa mbele yake. Kazi ya watu kutembea kwa miguu kutoka Mbambabay mpaka Butiama ikawa haina thamani tena. Mndai serikali ya Tanganyika leo, je huo si unafiki na dharau kwa mwalimu? Mnahoji faida za muungano leo, huo siyo unafiki?
 
Wewe unastahili kunyongwa na wala siyo kubishana.Msalimie Ngoyai.
 

It sounds like "Tribalism!"
 
Kumbe tatizo la umasikini wa watanzania linatokana na uoga uliopitiliza katika kujaribu na kuthubutu kusema ukweli. Nafunga mjadala hapa kwa kusema maneno haya kwa kuwajibu wale wanaopotosha ukweli wa maneno yangu na kujaribu kuyafungia katika parandesi ya hatia. Nawapa ujumbe huu; Kama kweli mnayaenzi yale yote yaliyofanywa na Nyerere, anzeni sasa kudai azimio la Arusha lirudi, rudisheni mfumo wa siasa ya ujamaa na kujitegemea, komeni kudai uwepo wa serikali ya Tanganyika na wale wanaosema muungano ufe waache mara moja...Pamoja na hayo, sinta salimu amri kuamini kuwa Mwalimu alitumia sehemu ya ushawishi wake na kukubalika kwake kwa ajili ya kuwabomoa kisiasa baadhi ya wanasiasa aliokuwa na chuki nao. Huo ndiyo ulikuwa upande wake wa pili kisiasa.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…