Kwanini Nyati ana nguvu za kuua Simba?

Kwanini Nyati ana nguvu za kuua Simba?

Anammeza mkuu, ingia youtube uone hizo video. Chatu anammeza hata simba
Ninakoishi mimi ambako ndiko nimekulia tangu utoto kuna maeneo yenye mito mikubwa hiyvo chatu ni wengi sana. Siku zote tangu utoto wangu nimekuwa nikisikia hata kushuhudia chatu amemeza mbwa, mbuzi, banadamu wachoma mkaa na wawindaji hasa wamasai lkn sijabahatika kusikia chatu kameza ng'ombe! Tena chatu wana akili sana utakua umeongozana na kundi kubwa la mifugo ukichunga wala hafanyi kitu watapita wote hata kumkanyaga lkn hatajigusa anakusubiria wewe wa mwisho ambaye ni mchungaji!!!
 
Mimi nafikir mfalme wa mwitu ni chui au tiger au cheeter japo wanamuogopa simba lakini huwa hawasumbuliwi na wanyama wengine na wakinda na kukamata msosi wao hupeleka juu ya mti na kujilia vizur tofauti na simba akipata msosi wale fisi na mbwa mwitu huja kwa makundi na kumtishia simba na hatimae simba hukimbia
Kwanini mfalme asiwe tembo ambaye wanyama wote humgwaya hata kumsogelea???
 
Sawa simba,mara huwa anatumia nguvu katika kupata chakula chake,lazima akimbize ndiyo apate lindo chakula chake,na miguu ndiyo nyenzo yake kubwa,hana wakumletea chakula,
Sasa hiyo si ina apply kwa wanyama wote wa porini, mbona umemtaja simba tu au kuna wanyama wengine wanaoleteana msosi pindi wanapoumia? Hasa wale wanaokula nyama
 
Wanyama wengine huwa wanatabia ya kula vilivyobakishwa na wengine ila simba utaribu huo hana huwa anapenda nyama iliyofresh,sijajua kwa nini ila ndiyo alivyo
 
Wanyama wengine huwa wanatabia ya kula vilivyobakishwa na wengine ila simba utaribu huo hana huwa anapenda nyama iliyofresh,sijajua kwa nini ila ndiyo alivyo
Huo ndo utegemezi wa kiasili, kwa wanyama wengine kama fisi hawawezi kuwinda hivyo wanasubiria simba au chui akamate ale na kubakisha na wao wapate riziki yao
 
Kasigazi kweli huyo ni ngurue pori ila ni mnyama anaeinjoi sana maisha ya porini,ni mnyama ambae yuko very shap,na anafurahisha hasa wakati anakula ,huwaga anakula haraka haraka hana mda wa kupoteza
 
wakuu tujuzane hapa kwa nini nyati ana ubavu wa kupambana na simba na kumuua? inafahamika kuwa simba ni mfalme wa nyika na ana uwezo kufanya atakalo ndani ya mbuga, lakini nyati nae ni mbishi sana akikutana na simba lazima pachimbike? sasa kwa nini nyati ana uwezo wa kupambana na simba?

Kwa sababu Simba Ni sisiem na Nyati ni Kafu
 
Kasigazi kweli huyo ni ngurue pori ila ni mnyama anaeinjoi sana maisha ya porini,ni mnyama ambae yuko very shap,na anafurahisha hasa wakati anakula ,huwaga anakula haraka haraka hana mda wa kupoteza
Huyo ni msosi mzuri wa chatu mkuu ingia youtube uone chatu anavyomkamua damu na kummeza
 
Karibuni mbugani
 

Attachments

  • 1455444317520.jpg
    1455444317520.jpg
    49.3 KB · Views: 39
Ninakoishi mimi ambako ndiko nimekulia tangu utoto kuna maeneo yenye mito mikubwa hiyvo chatu ni wengi sana. Siku zote tangu utoto wangu nimekuwa nikisikia hata kushuhudia chatu amemeza mbwa, mbuzi, banadamu wachoma mkaa na wawindaji hasa wamasai lkn sijabahatika kusikia chatu kameza ng'ombe! Tena chatu wana akili sana utakua umeongozana na kundi kubwa la mifugo ukichunga wala hafanyi kitu watapita wote hata kumkanyaga lkn hatajigusa anakusubiria wewe wa mwisho ambaye ni mchungaji!!!
Duuh! Mi nafikiri labda chatu anamuogopa binadamu kumbe na yy anamezwa
 
Duuh! Mi nafikiri labda chatu anamuogopa binadamu kumbe na yy anamezwa
Ah! Chatu amuogope binadamu???!!! Thubutu usije ukachezea shilingi jirani na tundu la toilet, faster tutasimama kuomboleza. Katika nyoka chatu anaaminika kuwa na uwezo mkubwa sana kiakili & kuhisi hivyo kuwa na uwezo mkubwa sana kuwinda. Kaa mbali na lile lidubwana.
 
Back
Top Bottom