Kwanini Mwl. Nyerere alishindwa kuhamia Dodoma?

Kwanini Mwl. Nyerere alishindwa kuhamia Dodoma?

Walipa kodi tungekuwa tunashirikishwa kwenye mipango ya maendeleo ya nchi yetu tungeokoa Pesa nyingi Sana kuwekezwa pasipo tija Leo Kilimo kwanza imetupwa,uchumi wa gas imetupwa hapa ni kodi zetu tu ndio zinateketezwa lait kila ajae angekuwa anatekeleza vipaumbele vya wananchi Na sio vyake tungekuwa mbali sana.Check jengo LA machinga complex limedoda sababu hawakushirikisha machinga
Yaani vipaumbele vyao sio vipaumbele vya wananchi wanaangalia viwapavyo sifa awajali kuhusu riba
.Wananchi ushirikishwa kwenye kulipa madeni tu.

Aisee Machinga Complex inaumiza mno.....
 
tatizo huwa mnaendekeza mihemko bila sababu ya msingi, kuhamia dodoma kuna manufaa yapi?, tunaangalia negative na positive, hamna kisicho na changamoto ila pale faida zinapokuwa ni nyingi kuliko hasara kwanini tusihamie dodoma?, lengo ni serikali dodoma sasa nyie mlivyo wakurupukaji mnataka 100% ghafla bin vuu kila mtu awe dodoma , hii inahitaji process na tulipofika ni pazuri...wamefanikiwa Nigeria abuja sembuse sisi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bado haijakaa sawa kumbuka kila mkoa unavitu sawa Madaraka mikoani ndio solution yaani ukitakacho unakipata wilayani
You mean sasa mfumo ugeuzwe na kuwa wa majimbo kuwa na nguvu. Yes! It can work also, hivyo hivyo majimbo yawe na nguvu ya kuamua matumizi ya fedha zake pasi ya kuchngwa na kuwekwa central then central ikafanya mgawanyo.
 
Rais wa nchi lazima awe mji mmoja na Balozi za mataifa makubwa ya dunia.

Pia as part of agreement na hizi Balozi lazima mji Mkuu wa Kiserikali uwe na Hospital kubwa ya Rufaa iliyopitishwa na UN, kwa sasa ni Aghakghan Dar na ile ya Nairobi tu ndipo hawa ma Diplomat wanatibiwa.

Sasa haya mengine ya Shule, Hotels, Viwanja vya ndege nk pia ni lazima yatakuwa condidered kabla ya kahamia katika mji husika.

Kwa hiyo mliofikiri Rais anahamia tu kama atakavyo si kweli...

Ndiyo maana ma Rais wengi walisita akiwemo Mwalimu mwenyewe.
 
Thubutu akae miezi 6 bila kwenda magogoni wakati ameshakua NUHU
Mkuu Dodoma kama capital ni gharama,ilishindikana enzi za Raisi Mwl.Nyerere tena baada ya yeye aliekuwa driving machine kuhamia Dodoma kuacha ghafla,sababu hazikuwekwa wazi mara tu baada ya kujengewa Ikulu hapo Chamwino na kukabidhiwa funguo!!!.

Japo tulikuwa na mfumo wa chama kimmoja, baraza la mawazi na bunge lilipinga kwa nguvu mmoja kuhamisha makao makuu,lakini Mwl.Nyerere alitishia kulivunja bunge ndipo walisalimu amri kuhamia Dodoma.
Utaratibu wake ulikuwa hivi
1.Iliundwa wizara ya ustawishaji wa makao makuu likiongozwa na Chief Adam Sapi Mkwawa.
2.Likaundwa Capital Development Authority CDA ikiongozwa na Sir George Kahama kama CEO
3.Wakahamisha ofisi ya makamu wa pili wa Raisi na waziri mkuu Mzee Rashidi Mfaume Kawawa akahamia Dodoma rasmi Jan 1975
4.Ikajengwa Ikulu Dodoma Chamwino ili Raisi akishahamia hapo ndipo wizara nyingine nazo zianze kuhamishiwa Dodoma.

Lakini cha ajabu mwaka 1975 Mwl.Nyerere alikaa siku kidogo pale hakuhamisha ofisi yake,nakumbuka picha ya gazeti la Daily News front page alionekana Mwl.Nyerere hakuwa na furaha,alikuwa na mawazo mengi.

Kilichofuata sote tunakijua alirudi Magogoni na Msasani akipunga upepo wa bahari ya Indi hadi pale alipostaafu 1985.
Mimi niliwahi kusema humu kama Magu yupo committed kuhamia Dodoma basi achukue miezi 6 bila kugusa Dar-es-salaam lakini hakustahimili so sad.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata aliyeamrisha kashindwa kuondoka Dar.

Kuagiza wengine ni rahisi sana,
 
Unaweza ukawa unadhibiti makusanyo,umefuta safari za nje,umefuta posho,umedhibiti ufisad Na upigaji,Lkn ukawa unaweka kwenye mifuko iliyotoboka yaani kuwekeza pasiporudisha Leo wala kesho pesa mfano Dodoma, ndege,Chato airport, msalato airport, nk inakuwa ni sawa Na aliyeachilia ufisad Na upigaji ukatamalaki maana kote kuna upotevu
 
Mwl. JK Nyerere alikuwa na akili nyingi sana.. Alibaini kuwa kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia hakukuwepo na haja tena ya kuhamia Dodoma bali kuwajengea uwezo wananchi ili waweze kupambana na umaskini, maradhi na ujinga!

Kwa akili ya kawaida tu... Ukihamia Dodoma ni lazima uendelee kuilinda zaidi Dar (gharama maradufu).

Jiulize, unahamia Dodoma ghafla ghafla bila kuwekeza kuboresha miundombinu yake ya barabara, maji safi, maji taka, n.k.... Je, umefanya tafiti ukajua itachukua muda gani kufikia mkwamo kama ule uliopo Dar??

Unaweka nguvu nyingi kuhamia Dodoma unaokoa nini? Au unaleta utofauti gani? Au bado unatafuta katikati ya nchi ndo uweke makao makuu??

Hiki ni kipindi ambacho badala ya kuzilundika idara, taasisi na wizara za serikali sehemu moja (centralization) ilitakiwa zitawanywe kwenye kila jiji hapa nchini kwa uwezo, nguvu na juhudi zile zile... Mfano Wizara ya Ardhi ijengwe Dodoma, Madini Mwanza, Utalii Arusha, Usafirishaji, Bandari Dar, Gesi Mtwara, n.k... Yaani kila jiji na kila Kanda ipate uwekezaji wa maana wa makao makuu ya ofisi, idara na taasisi za serikali...
Hatua hii ingechochea maendeleo ya miundombinu na mzunguko wa fedha kwenye shughuli mbalimbali za uchumi mikoani...!! Ikumbukwe kuwa kwenye nchi kama hii serikali ndo mwajiri kiongozi na mwenye job security nzuri... Badala ya kusambaza rasilimali watu na rasilimali fedha mikoani... Tunazitoa Dar na kwenda kuzilundika tena Dodoma...

Huu utawala wa sasa umeshindwa kabisa hayo mapambano. Badala yake wamekuja na vita wanavyoviweza vya maendeleo ya vitu... Yes, mtajenga sana vitu lakini ni vyema mkafahamu kuwa grafu ya ujinga, umaskini na maradhi inazidi kupanda juu!!
[emoji123][emoji106]
 
Wazo la kuhamisha makao makuu lilianza wakati wa ukoloni wa Wajerumani hasa wakati wa vita ya kwanza ya dunia walipohamishia makao Tabora kwa muda mnamo mwaka 1916. Mwaka 1959 Kupitia LEGCO Waingereza walipendekeza makao yahamie Dodoma lakini hatua hazikuchukuliwa tokana na gharama kuwa kubwa. Mwaka 1966 Joseph Nyerere mdogo wake Mwalimu alipeleka muswada bungeni kuhusu serikali kuhamia Dodoma kwa awamu, lakini pia haikufanikiwa kupitishwa. Mwaka 1972 kamati kuu ya TANU ilifikia maamuzi ya kuhamishia makao makuu ya TANU Dodoma kwa sababu kuu tatu.

Mosi, Kwa kuwa Dodoma ni katikati na inaweza kufikiwa kirahisi tokea pande zote za Tanzania.

Pili, kutokana na kuwa nyuma kimaendeleo na kuwa kwa kuhamishia makao ya chama kungechangamsha uchumi, na

Tatu. Ni kwa ajili ya Usalama kwa kuwa bara kulionekana kuwa salama kuliko ukanda wa pwani.

Mwaka huohuo serikali pia ilichagua kampuni tatu za kimataifa ili kupendekeza sehemu na master plan ya mji mkuu wa nchi. Uamuzi wa kuhamisha mji mkuu ulifikiwa katika mkutano mkuu maalum wa TANU Oktoba 1973. Na baadae Mwalimu alitangaza kupitia redio kuwa serikali na chama vitahamia Dodoma katika kipindi cha miaka 10.

Serikali ilichukua hatua kadhaa. Kwanza ni kwa kuunda Wizara ya Maendeleo ya mji mkuu Chini ya Ofisi ya Rais na pia kuunda Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) .Waziri wa kwanza akiwa Chifu Adam Sapi Mkwawa na Mkurugenzi mkuu wa CDA wa kwanza akiwa Sir George.

Majukumu ya kwanza ya Mamlaka ilikuwa ni:
Mosi, Kutafuta wana Mipango miji (Master planners) ambapo waliitisha tenda ma kampuni toka Canada Project Planning Associates ilichaguliwa

Pili, Ku recruit wafanyakazi wa mamlaka ampapo Sir George alianzisha kurugenzi tisa na kila kurugenzi ikiwa na Mkurugenzi na timu yake.

Kazi nyingine ilikuwa ni kuainisha eneo ambapo mji mkuu utajengwa na waliainisha maeneo sita tofauti na hatimaye wakachagua eneo moja karibu na mji wa zamani.

Kazi ya kutengeneza Master plan ilichukua miaka miwili na jopo la majaji likiongozwa na mtaalam Sir John Overal aliyekuwa Mkurugenzi wa Australian National Capital Development Commission walipitisha master plan mnamo Februali 1975. Master plan ilikuwa imegawanywa katika maeneo 4 yakiwemo Eneo la mjini (Downtown) ambapo pangekuwa na ofisi za serikali, bunge, mahakama na maeneo ya biashara,

Eneo la makazi ambapo makazi yalipangwa kwa mujibu wa mtindo wa TANU wa nyumba kumi. Eneo la tatu ilikiwa Maeneo ya wazi na bustani za kupumzikia na Eneo jingine ilikuwa miundombinu ya usafirishaji.

Mwalimu alipendezwa sana na mpango huo uliokuwa ukiakisi siasa ya ujamaa.
Ilikuwa imekadiriwa kuwa ujenzi utachukua miaka 10 kuanzia mwaka 1976 hadi 1986 na ungegharimu shilingi bilioni 3.6 au dola za Marekani milioni 53.
CDA Pia ilikuwa na jukumu la kuweka miundombinu kama maji, barabara,

Pamoja na malengo mazuri hali ya uchumi baada ya hapo haikuwa nzuri kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta, Vita vya Kagera nk. CDA ikaambulia kupata 10% tu ya makadirio ya gharama hata hivyo walifanikiwa kujenga baadhi ya maiundombinu ikiweko barabara; mfumo wa maji machafu na salama. Pia walijenga ikulu ya Chamwino na baadhi ya ofisi za serikali.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata aliyeamrisha kashindwa kuondoka Dar.

Kuagiza wengine ni rahisi sana,
Kaogopa labda ni rahisi mwingine kujitangazia ikulu ya dar ushind.
Mipango yake ni migumu sana kutimia
Jappo ni rahisi kutamkwa.Mwaka wa Tano sgr hata Moro haijafika
 
Kakopi mipango yote ya mwalimu aifanikishe ili apate sifa kuhamia dodoma bwawa la stigler nk
Priorities alitaka mikakati ifanyike kwa step bila kukurupuka maana kunamambo mengi ya muhimu kuliko kuhamia dodoma.
mfano mpaka enzi ya Mkapa Rais alikuwa akienda nje kuomba chakula kisingizio ukame sasa unaanzaje kuhamia Dom.
Sasahivi hata chanjo za watoto ni zashida,ajira hamna,elimu/shule siobora,kilimo hasa cha biashara kimefail lkn mtu mmoja ana force ili aweke historia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom