Kwanini Mwl. Nyerere alishindwa kuhamia Dodoma?

Hata aliyeamrisha kashindwa kuondoka Dar.

Kuagiza wengine ni rahisi sana,
Kaogopa labda ni rahisi mwingine kujitangazia ikulu ya dar ushind.
Mipango yake ni migumu sana kutimia
Jappo ni rahisi kutamkwa.Mwaka wa Tano sgr hata Moro haijafika
 
Wazo la kuhamahamishia serikali Dodoma lilikuwa la Mwl. Nyerere wakati ya awamu ya kwanza. Lakini hata baada ya kuliongoza taifa kwa muda mrefu alishindwa kuitekeleza mdoto yake ya kuhamia Dodoma.

Ndoto ya kuhamia Dodoma pia haikutimia kwenye awamu zingine 3 (miaka 30) zilizofuata na ikatekelezwa awamu hii ya tano?

Swali ni ni nini kilisababisha mwalimu asiweze kuitekeleza Ndoto yake mwenyewe ya kuhamia Dodoma?

Hebu tukumbushane hapo.
Unadhani yeye hakupenda kukaa pembezoni mwa bahari huku akipogwa na upepo mwanana kabisa ?
 
kwanini-mwl-nyerere-alishindwa-kuhamia-dodoma === kwa nini Mwl nyerere hakupenda mchagga ama mdau wa kaskazini awe raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania

Mwl. Nyere alikuwa na akili mingi sanaa == Mwl Nyerere ni sawa na Vichwa 100 vya mawaziri wa leo hahaaaa
 
Wazo la kuhamahamishia serikali Dodoma lilikuwa la Mwl. Nyerere wakati ya awamu ya kwanza. Lakini hata baada ya kuliongoza taifa kwa muda mrefu alishindwa kuitekeleza mdoto yake ya kuhamia Dodoma.

Ndoto ya kuhamia Dodoma pia haikutimia kwenye awamu zingine 3 (miaka 30) zilizofuata na ikatekelezwa awamu hii ya tano?

Swali ni ni nini kilisababisha mwalimu asiweze kuitekeleza Ndoto yake mwenyewe ya kuhamia Dodoma?

Hebu tukumbushane hapo.
Ni kweli Mwalimu Nyerere alikuwa wa kwanza kuhamasisha Makao Makuu ya nchi kuhamia Dodoma.
Nilikuwa mtu mzima wakati ule na nilikuwa Chuo na nilikuwa kada mtiifu wa TANU.
Sababu alizozitoa zilikuwa nzito ambazo kwa kweli hakuna mwenye akili timamu kwa wakati ule angezipinga.
Baadhi ya sababu zilikuwa
1. Dodoma ni katikati ya nchi yetu. Kuhamia kule kungerahisisha utawala kwani wote wangeweza kufika kwa kutumia muda mfupi.
2. Usalama. Alisema Jiji la Dar Es Salaam lililoko pembezoni mwa bahari ya Hindi liko sehemu ngumu ki ulinzi kwa hiyo ingekuwa salama zaidi kama Makao yangehamishiwa katikati ya nchi.
Izingatiwe nchi yetu ilikuwa ikitishiwa na mashambulio toka kwa Wakoloni na Walowezi wa Msumbiji, Rhodesia na Afrika ya Kusini ya kibaguzi.
Mwisho alisisitiza kuhamia Dodoma si kuhamisha majumba. Na alisisitiza zoezi lile kufanywa kwa awamu, taratibu bila kuujeruhi uchumi.
Kweli mchakato ulianza na kuendelea vema hadi ilipozuka vita dhidi ya Nduli Iddi Amin ambapo fedha, mali na amali zote zilielekezwa huko.
Uchumi ulivurugwa kwelikweli baada ya vita, mdororo wa uchumi ulitatiza zoezi zima na ajenda ya kuhamia Dodoma ni kama ilisahaulika.
Kuisha kwa tawala za kilowezi na kikoloni Kusini kwetu kulipunguza zaidi uzito wa sababu ya pili. Na kwa kweli mabadiliko makubwa katika tekinohama sasa yamepunguza au kuondoa kabisa sababu ya kwanza!
Kwa maoni yangu kuhamisha Makao sasa ni kujibebesha zigo lisilo na faida kubwa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Thubutuu.

Alikurupuka sema ndo hivyoo kajikausha yeye alivyoingia madarakani aliona watungulizi wake ni maboya. Kakurupuka weeee saivi akiangalia alicho fanya miaka 4+ haoni zaidi ya kununua wabunge na madiwani.

Nimecheka kama mazuri. Dunia ya leo you can’t silence wise people wanamcheka tu yaani. Wanaojifanya wapo karibu kumbe wanamsaliti. Tz kubwa sana yaani atashangaa anguko analoanguka nalo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom