Kwanini Mungu alituumba sisi wanadamu, iwapo alijua kuwa tutamuasi na atatupeleka motoni?

Balqior

JF-Expert Member
Jun 8, 2021
1,709
5,697
Habarini wadau,

Binafsi naamini Mungu yupo, ni mwema, ndo aliumba vyote, anajua vyote past present and future, na ni muweza wa vyote, hakuna alie zaidi yake.

Uislamu na ukristo unafundisha kuwa mwisho wa sisi wenye dhambi ni kwenye moto wa milele, sasa mimi najiuliza.

1)Mungu akituchoma sisi kwenye moto wa milele, ataongezeka nini, na kufaidiwa nini? Asipotuchoma atapungukiwa nini?

2)Mungu atavumiliaje kuona sisi binadamu tukiwa kwenye maumivu ya kuchomeka milele na milele? ikiwa mimi mwenye dhambi siwezi vumilia kuona adui yangu akiteseka kwa mda mrefu sana?

3)Asingetuumba kuna mtu angemuuliza kwanini hajatuumba wakati yeye ni muweza wa yote?

4)Mahubiri, na vitabu vya Mungu, na shuhuda za mbinguni walipo watenda mema, na kuzimu wanakoteseka waliokufa kwenye dhambi, vikituambia sisi tulio hai kuhusu moto wa milele, ili tuache dhambi tuokolewe, je tukiwa wacha Mungu, uhusiano wetu sisi binadamu na Mungu utakuwa ni wa kweli unaotoka moyoni? au ni uhusiano utakaozaliwa kutokana na hofu, yani unamtumikia Mungu ili usiende motoni, ingawa kiuhalisia adhabu ya moto isingekuepo, ungeendelea kufurahia dhambi na kuacha kusali.

Sina nia ya kukufuru ila nimejaribu kuwaza tu, nipate ufahamu kwenye mambo haya , fundisho kuhusu adhabu ya kuchomeka kwenye moto wa milele, wakati umefanya dhambi ndani ya miaka 75, linanipa wasiwasi kuhusu asili na tabia ya huyu Muumba wetu kwakweli. Nahisi hio adhabu ni too much kuliko makosa yaliyofanyika. Kwenye vitabu vya dini Quran na biblia, malaika wa mbinguni wanakiri hukumu za Mungu ni za haki na kweli, labda kuna vitu ambavyo sivijui.
 
Hizo ni Nadharia tu za kututawala na kututia hofu.

Mimi ni mzazi pamoja na mapungufu yangu yote, siwezi kumchoma mwanangu moyo.

Mungu amejaa Upendo hawezi kuwachoma watu wake kwa moto wa milele.
 
Hizo ni Nadharia tu za kututawala na kututia hofu.

Mimi ni mzazi pamoja na mapungufu yangu yote, siwezi kumchoma mwanangu moyo.

Mungu amejaa Upendo hawezi kuwachoma watu wake kwa moto wa milele.
Ni kweli Mungu ana huruma ndio maana alimtoa mwanaye wa pekee Yesu kristo ili watu watakao mwamini na kumfuata waepuke kwenda Motoni.tofauti na hapo moto uko palepale.
 
Kama una amini Mungu yupo,

Halafu hapohapo unajiuliza swali kwanini Mungu huyo alikuumba,

Ni dhahiri kwamba Mungu huyo Hayupo. Una mashaka mashaka ya uwepo wake.

Kama umeweza kujua Mungu yupo, Unashindwaje kujua kwanini Mungu huyo alikuumba?

Mungu hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Human beings created God through assumptions, Based on things beyond their imaginations.

God doesn't EXIST.
 
Kwahiyo WAKATOLIKI wote wataenda peponi?

Unataka kuniambia Azarel mla nguruwe anaenda peponi!

Maghayo mbeba mabox anaenda!

Tate Mkuu mfilaji anaenda!

FRESHMAN muabudu sanamu ataenda?
Kama unatenda tofauti na maagizo ya Yesu hapo unakuwa humwamini na moto utakuhusu,ndio sehemu ya wale wanaomtaja Yesu kwa vinywa vyao,na kumwabudu lakini mioyo yao na matendo yao yako mbali naye.
 
Mungu akituchoma sisi kwenye moto wa milele, ataongezeka nini, na kufaidiwa nini? Asipotuchoma atapungukiwa nini?
1. Moto ni mara moja tu zaaap sio milele ni jambo lisilokuwepo

Sina nia ya kukufuru ila nimejaribu kuwaza tu, nipate ufahamu kwenye mambo haya , fundisho kuhusu adhabu ya kuchomeka kwenye moto wa milele, wakati umefanya dhambi ndani ya miaka 75, linanipa wasiwasi kuhusu asili na tabia ya huyu Muumba wetu kwakweli. Nahisi hio adhabu ni too much kuliko makosa yaliyofanyika. Kwenye vitabu vya dini Quran na biblia, malaika wa mbinguni wanakiri hukumu za Mungu ni za haki na kweli, labda kuna vitu ambavyo sivijui.
Kuna mambo mawili tu mwisho wa siku baada ya huu UHAI kaka yaani baada ya hiki KIFO: ni UZIMA na MAUTI

UZIMA ni hao watakaokuwa uweponi mwa Bwana walioifuata njia ya KWELI

MAUTI ni kwa waliopotea, huu ni u kutokuwepo yaani watafutika milele. Lakini kwao wenyewe itakuwa ni kama usingizi ni hawapo.

Fikiria moto huwa unafanya kazi gani? Moto unatawanyisha vitu virudi kwenye asili yake ya kutokuwepo. Unaondoa order inakuwa chaos. Unaunguza protini inakuwa elements na atoms. Kitu kikisharudi chaos kinakuwa ni hakipo tena ndio maana

Utaunguza kiti kitabakia majivu, ukiamua kuyachoma majivu utakuwa haukiathiri kiti kinamna yoyote ile zaidi bali wewe unacheza na majivu tu yasiyo na maana. Hivyo unaweza kuchoma majivu milele ukadanganya watu kuwa nimekichoma kile kiti milele? Ni jambo lisilo na maana hivyo ni HALIPO.

Mauti ni milele kiotomati

Ila ili uhai uweze kuwa milele ndio unahitaji nguvu ya Mungu, UZIMA WA MILELE. Naishia hapa utafune kwanza. Tumia akili. Udadisi ndo akili.
 
Asingetuumba kuna mtu angemuuliza kwanini hajatuumba wakati yeye ni muweza wa yote?
Kuumbwa ni kama zawadi ya Uhai. Ni zawadi fulani nzuri tu kuendelea kuwepo.

Basi kuna watakaoikubali. Hawa wataipenda njia ya kweli ambayo kwa duniani inaboresha uhai wa wote. Halafu inatafsirika kuwa kwa mbinguni utaufurahia uzima uweponi mwa Mungu. Basi hawa wataishi milele. In him we live, move and have our being.

Lakini pia kuna watakaoikataa, watamkataa Mungu na zawadi yake ya uhai wa njia inayoelekeza kwenye uzima. Hawa mwisho wa siku Mungu atawapatia haja ya moyo wao kwa kuwaruhusu wapotee katika Mauti. Yote haya ni katika upendo mkuu kuwapa haswa walichochagua na wanachokitaka hata kama Mungu 'hangependa' iwe hivyo

Hawataendelea kuteseka milele maana mauti ni kutokuwepo. Hivyo hautajiskia vibaya milele kumtesa adui. La. Ni simply adui atacease tobe. Zaap. Dubwi. Hayupo!! Wameikataa zawadi ya UZIMA WA MILELE.

Mungu atavumiliaje kuona sisi binadamu tukiwa kwenye maumivu ya kuchomeka milele na milele? ikiwa mimi mwenye dhambi siwezi vumilia kuona adui yangu akiteseka kwa mda mrefu sana
 
Achana na hadithi zisizo na kichwa wala miguu. Mungu wa kwenye Biblia ama Quran hayupo.

Kwa ujumla Mungu hayupo. Mungu ni fiction figure tu hakuna kitu kama hicho.

Habari kuhusu Mungu ni za kutunga na zisizo za muunganiko ulionyooka.
 
Embu waza beer, nyagii, whiskey, .... nyonyoo jinsi vilivyo vitamuu why aliviumbaaa?
 
Alijua tuta muasi ndo maana akaweka moto mwishoni.
So hio ni win win situation kwake mkuu.
 
Habarini wadau,

Binafsi naamini Mungu yupo, ni mwema, ndo aliumba vyote, anajua vyote past present and future, na ni muweza wa vyote, hakuna alie zaidi yake.

Uislamu na ukristo unafundisha kuwa mwisho wa sisi wenye dhambi ni kwenye moto wa milele, sasa mimi najiuliza.

1)Mungu akituchoma sisi kwenye moto wa milele, ataongezeka nini, na kufaidiwa nini? Asipotuchoma atapungukiwa nini?

2)Mungu atavumiliaje kuona sisi binadamu tukiwa kwenye maumivu ya kuchomeka milele na milele? ikiwa mimi mwenye dhambi siwezi vumilia kuona adui yangu akiteseka kwa mda mrefu sana?

3)Asingetuumba kuna mtu angemuuliza kwanini hajatuumba wakati yeye ni muweza wa yote?

4)Mahubiri, na vitabu vya Mungu, na shuhuda za mbinguni walipo watenda mema, na kuzimu wanakoteseka waliokufa kwenye dhambi, vikituambia sisi tulio hai kuhusu moto wa milele, ili tuache dhambi tuokolewe, je tukiwa wacha Mungu, uhusiano wetu sisi binadamu na Mungu utakuwa ni wa kweli unaotoka moyoni? au ni uhusiano utakaozaliwa kutokana na hofu, yani unamtumikia Mungu ili usiende motoni, ingawa kiuhalisia adhabu ya moto isingekuepo, ungeendelea kufurahia dhambi na kuacha kusali.

Sina nia ya kukufuru ila nimejaribu kuwaza tu, nipate ufahamu kwenye mambo haya , fundisho kuhusu adhabu ya kuchomeka kwenye moto wa milele, wakati umefanya dhambi ndani ya miaka 75, linanipa wasiwasi kuhusu asili na tabia ya huyu Muumba wetu kwakweli. Nahisi hio adhabu ni too much kuliko makosa yaliyofanyika. Kwenye vitabu vya dini Quran na biblia, malaika wa mbinguni wanakiri hukumu za Mungu ni za haki na kweli, labda kuna vitu ambavyo sivijui.
Niliposoma hiko kitabu cha uongo kwa kina nimebaini ni stori za uongo Mtupu
1. Mungu gani huyo anayebebwa na shetani mpaka kilimani?
2.Ni nani aliyekuwa anarekodi wakati huyo Mungu anaumba Dunia?
3.Hivi jua liliumbwa siku ya ngapi na kabla ya kuubwa Jua mwanga gani uliokuwepo?
4.Yesu alivyokwenda Mlimani kusali peke yake muandishi wake alikuwa nani mpaka mazungumzo yake na Mungu yawe kitabuni?
5..Eti ukiwa na Imani unaweza ukaamuru mti ng'oka na utang'oka lakini Yesu huyo huyo akasaidiwa kubeba msalaba tu maana aliushindwa ili akatundikwe.
6.Hivi inakuaje mnatembea kwa mguu km1400 kwa usiku mmoja lakini km 700 tu miaka 40 Hao wanaIsrael na Mussa wao
7.Imani yako inasema Umerithi zambi za Adam na Eva lakini kituko kwani Hamjarithi Utajiri wa Suleiman
8. Eti Nuhu alijenga Safina sababu ya Gharika kuu na akapakiza viumbe jike na dume swali linakuja (i)Taarifa ilifikishwa vipi Afrika,Ulaya,Amerika kusini? na Australia ?(ii)Simba alikula nini kipindi chote cha gharika ndani ya Safina(iii) Watu walikula nini baada ya mafuriko hayo makali maana ardhi ilikuwa tupu mazao yamekaisha na mafuriko? (i)Kangaroo alisafiri vipi mpaka Australia
7.Baada ya kula Tunda huko bustani ya Eden Mwanamke Eva akasema Atazaa kwa Uchungu Swali hawa ng'ombe wetu hapa Tarime mbona wanazaa kwa Uchungu wametenda kosa gani?
8.Kwenye Sodoma na Gomola tunaambiwa Mke wa Ruthu aligeuka Mwamba wa Chumvi swali ni hili nani aliyemuona kwamba amegeuka Mwamba wa Chumvi wakati walipewa taarifa kuwa ni marufuku kugeuka?
9.Hivi ni Mungu gani huyo aliyevumilia miaka 400 ya utumwa tuliofanyiwa na kuuzwa mnadani kama maembe halafu ataniadhibu kwa kutokumuamini?
10.Eti msamehe Mtu 7x70 kwa makosa aliyotenda Lakini huyo Mungu kashindwa Kumsamehe Adam na Eva kwa kula Apple moja?
11.Samson alimuua Simba kwenye jangwa la Palestina aaahaaaa Toka lini simba anaishi kwenye jangwa?.

Hakika ninakuambia kama kungekuwa na Nguvu kwenye jina la Yesu hao Wazungu wangeficha kama inavyofichwa Teknolojia ya Nyuklia.

Heshimu sana Babu wa Mababu zako maana wao ndiyo wenye DNA zako wewe umetoka kwao Dini ni tamaduni ndani ya tamaduni kuna mila ndani ya Mila kuna Imani na Imani ndiyo Wageni wakaita Dini hakika nakuambia Imani ya Kiafrika wala haina Masharti magumu na Inafanya kazi kwa Ubora wa juu sana na Ibada zake ni kwa Mwaka mara moja au mbili lakini Imani zingine lazima ufanye kila muda kila wakati lakini Matokeo 0.

Heshimu Afrika heshima maadili na mila ulizoachiwa..

Unaweza sema Uongo Kanisani Unaweza sema Uongo Msikitini na hakuna kinachoweza tokea usije sema Uongo kwenye Mizumu au kwenye Kilinge cha Mganga utakwenda na Maji .Toa ahaadi ya Pesa ya sadaka kanisani na Msikitini usipotoa hakuna kitakachotokea Usije thubutu Kwa Mganga au kwenye Mizimu hutoamini macho yako. KILINGE HAKITANIWI WALA HATUSEMI UONGO .
 
Habarini wadau,

Binafsi naamini Mungu yupo, ni mwema, ndo aliumba vyote, anajua vyote past present and future, na ni muweza wa vyote, hakuna alie zaidi yake.

Uislamu na ukristo unafundisha kuwa mwisho wa sisi wenye dhambi ni kwenye moto wa milele, sasa mimi najiuliza.

1)Mungu akituchoma sisi kwenye moto wa milele, ataongezeka nini, na kufaidiwa nini? Asipotuchoma atapungukiwa nini?

2)Mungu atavumiliaje kuona sisi binadamu tukiwa kwenye maumivu ya kuchomeka milele na milele? ikiwa mimi mwenye dhambi siwezi vumilia kuona adui yangu akiteseka kwa mda mrefu sana?

3)Asingetuumba kuna mtu angemuuliza kwanini hajatuumba wakati yeye ni muweza wa yote?

4)Mahubiri, na vitabu vya Mungu, na shuhuda za mbinguni walipo watenda mema, na kuzimu wanakoteseka waliokufa kwenye dhambi, vikituambia sisi tulio hai kuhusu moto wa milele, ili tuache dhambi tuokolewe, je tukiwa wacha Mungu, uhusiano wetu sisi binadamu na Mungu utakuwa ni wa kweli unaotoka moyoni? au ni uhusiano utakaozaliwa kutokana na hofu, yani unamtumikia Mungu ili usiende motoni, ingawa kiuhalisia adhabu ya moto isingekuepo, ungeendelea kufurahia dhambi na kuacha kusali.

Sina nia ya kukufuru ila nimejaribu kuwaza tu, nipate ufahamu kwenye mambo haya , fundisho kuhusu adhabu ya kuchomeka kwenye moto wa milele, wakati umefanya dhambi ndani ya miaka 75, linanipa wasiwasi kuhusu asili na tabia ya huyu Muumba wetu kwakweli. Nahisi hio adhabu ni too much kuliko makosa yaliyofanyika. Kwenye vitabu vya dini Quran na biblia, malaika wa mbinguni wanakiri hukumu za Mungu ni za haki na kweli, labda kuna vitu ambavyo sivijui.
Mwenyezi Mungu kaumba vilevile viumbe visivyomuasi, vinaitwa malaika.

Wewe usingeijuwa raha kama hakuna tabu.

Usingelijuwa jema kama hakuna ovu.

Usongeijuwa kheri kama hakuna shari.

Usingemjuwa mwanamke kama hakuna mwanamme.

Yote yameumbwa na Muumba wetu kwa faida yetu. Siyo yake.

Wewe unachotakiwa ji kuabudu.

Unafahamu maana ya juabudu?
 
Back
Top Bottom