Hivi Zitto alishamaliza shule huko Ujerumani? Inawezekana ikawa ni kwa sababu Zitto yuko busy na shule kwahiyo wangependa kumpa muda zaidi wa kusoma na kufanya shughuli za shule badala ya kuwa busy na shughuli za Chama. Mtoa mada nona unaanza kupandikiza udini hapo na hili ni tatizo kubwa sana kwa ndugu zetu waislamu maana hata kwenye sababu za msingi na zisizo na udini mnaanza kuhisi hivyo. Tujenge nchi yetu kwa pamoja tuache udini.
Tatizo la watu wanakwepa kujibu hoja badala yake wanatoa majibu ya mkato. Suala la udini katika hile kamati kwa mtazamo wangu halikuwepo kwani wajumbe waisilamu walikuwa 3 na wasiokuwa waisilam 3. Tukija suala la Kukaimu linaweza kusababishwa na wakati. (1)Mfano wakati wa uchaguzi mkuu zito yeye alikuwa kwenye mambo ya kampeni na jimbo lake lipo Kigoma wakati Mnyika yupo Dar kwa hiyo ni rahisi kwa Mnyika kukaimu. 2. Kwa sasa Zitto ametoka hospitali kwa hiyo ni wakati wa kupata mapumziko. Naomba mashabiki wa CDM muwe mnajibu hoja badala ya kumkashifu mtoa mada kwani mkiwa mtafanya hivyo mtaongeza wafuasi katika chama vinginevyo mtazidi kutengeneza maadui kwani watu watawaona watu msiopenda kukosolewa.
acha kuingilia majukumu na mipangilio ya watu.mara kwa mara tumeona na kusikia john mnyika akikaimu nafasi ya katibu mkuu wa chadema.
Protokali ziko wazi kuwa naibu katibu mkuu hupaswa kukaimu nafasi ya katibu mkuu pindi katibu mkuu anapokuwa hayupo.
Hili halifanyiki chadema. Je zitto haaminiki? Hana uwezo wa kushika nafasi hiyo nyeti?
Na kwanini yeye mwenyewe yupo kimya halalamiki mtu wa chini yake kuwa bosi wake kwa muda chamani?
Slaa(phd) na zitto ni member humu, nawaomba watatue huu utata
zitto alikuwa mgonjwa so nafasi yake ilipata kaimu - akirudi rasmi ataendelea na cheo chake. mbona nyie wachokonozi sana? badala ya kujadili mambo ya msingi nyie mkiamka tu mnafikiri CDM wamefanya nini, namna hii hatuwezi kusonga mbele milele!!Mara kwa mara tumeona na kusikia John Mnyika akikaimu nafasi ya Katibu Mkuu wa CHadema.
Protokali ziko wazi kuwa Naibu Katibu MKuu hupaswa kukaimu nafasi ya Katibu Mkuu pindi katibu Mkuu anapokuwa hayupo.
Hili halifanyiki Chadema. Je Zitto haaminiki? Hana uwezo wa kushika nafasi hiyo nyeti?
Na kwanini yeye mwenyewe yupo kimya halalamiki mtu wa chini yake kuwa bosi wake kwa muda chamani?
Slaa(PhD) na Zitto ni member humu, nawaomba watatue huu utata