Kwanini mnyika?

Mara kwa mara tumeona na kusikia John Mnyika akikaimu nafasi ya Katibu Mkuu wa CHadema.
Protokali ziko wazi kuwa Naibu Katibu MKuu hupaswa kukaimu nafasi ya Katibu Mkuu pindi katibu Mkuu anapokuwa hayupo.
Hili halifanyiki Chadema. Je Zitto haaminiki? Hana uwezo wa kushika nafasi hiyo nyeti?
Na kwanini yeye mwenyewe yupo kimya halalamiki mtu wa chini yake kuwa bosi wake kwa muda chamani?
Slaa(PhD) na Zitto ni member humu, nawaomba watatue huu utata


Mkuu mie nayaita haya majungu kwa kweli .Maan wewe ulitakiwa uende Chadema ukasemee kule hapa ni JF si Chadema.Pili wewe ni nanio hadi uhoji utaratibu wa Chadema na nambo yao ?Wao wana utaratibu wao kama ule wa CCM na mafisadi na kusema leo kujibua gamba kesho wanasema hatukuwa na mana hiyo mkuu lete hoja acha vioja hii ni JF .
 
Hayo Maswali yanaweza kujibiwa na Viongozi tu wa Chadema, Unless wengine mnaojibu ni Viongozi pia! - William

Haswaaaa! jibu lako ni sahihi,
Naona watu wanajisahau wanayatolea majibu mambo ambayo hayawahusu, chama kina viongozi, kuna msemaji wa chama yawezekana wote ni member jf. Watakuja kujibu hoja sisi tusiwaingilie.
 
Wakuu mimi sio gamba na sitakuwa gamba. Swali hili ni muhimu kujibiwa kwa umakini. Zitto mwenyewe alishawahi kunukuliwa akilalamika udini unamtengenezea maadui ndani ya chama. Na hili la Mnyika kukaimu sio mara ya kwanza. Hii sababu ya ugonjwa sioni kama ina mantiki kwa sababu kwenye ukatibu hakuna kazi ya kubeba zege, ni busara na maamuzi tu. Kama Zitto aliweza kuongea na media alipotoka India na bado akaenda kufungua kongamano la vijana wa kiafrika lililoandaliwa kwa ushirikiano na Bavicha sioni kama ana ugonjwa unaomfanya asiweze kukaimu ukatibu mkuu. Hata kama Dokta Slaa alienda kuuguza familia kipindi ambacho Zitto alikuwa India bado Zitto baada ya kurudi alipaswa kukaimu hiyo nafasi.
Kuna jambo cdm hawataki kuliweka wazi kuhusu Zitto. Ni kama vile haaminiki!
"Common Sense is not common to Common People Like You"

Unalazimisha vitu visivyokuwapo.Delegation huwa inapangwa kwa kipindi fulani kwa yule aliyekabidhiwa.Umetumwa na una lako jambo.I hate watu wanafiki kama wewe.
 
Mkuu mie nayaita haya majungu kwa kweli .Maan wewe ulitakiwa uende Chadema ukasemee kule hapa ni JF si Chadema.Pili wewe ni nanio hadi uhoji utaratibu wa Chadema na nambo yao ?Wao wana utaratibu wao kama ule wa CCM na mafisadi na kusema leo kujibua gamba kesho wanasema hatukuwa na mana hiyo mkuu lete hoja acha vioja hii ni JF .
Kilichobaki ni kuhoji kwa nini Mnyika alivaa sare na rais wakati wengine wamepiga magwanda.................Hapo hata wangetumwa mapadri au mashekhe hayo ni ya chadema na wanayajua wenyewe.............Udini huu hautatupeleka kokokte zaidi ya kujenga chuki miongoni mwetu
 
hoja haina mpango zaidi ya umbea haya angesema zito yangekuwa muhimu kujadili lakini wewe huna tofauti na wale wakujivua gamba mara nec mara kamati mara tume wakati walisema 90 days umbea hauna kwao..........
 
zitto ni mgonjwa,otherwise angekaimu
Hili jibu lina mashaka sana. Wapo watu wanaosema tuache kujadili mambo ya cdm. Hao watu wana ubongo wa jongoo. Tumejadili hapa dhana ya kujivua gamba mara kadhaa, tumejadili hapa issue ya Mabatia na mgogoro ndani ya NCCR Manunuzi, tumejadili GOGORO la Hamad Rashid na Maalim Seif ndan ya CCM-B. Leo ni dhambi kujadili mwenendo wa mambo ndan ya cdm?
Viongozi wa cdm lazima wajue watu tunaki-monitor hicho chama kila siku na tunaokitakia mema hatutanyamaza kama kuna matatizo tunayaona.
Kuna mtu mmoja wa cdm hq aliwah kuniambia hata kwenye vikao vizito vya siri Zitto huwa haitwi.
Na mwenendo wa chama katika safu ya uongozi wa juu ndani ya chadema hakuna mwenye akili timamu atakayesema uko sawa sawa.
Haya mambo lazima yawe questioned
 
kwa kumbukumbu zangu nakubaliana sana nawe kuwa Mnyika ndio hukaimu nafasi ya Ukatibu mkuu ila mara zote anazo kaimu hata Zitto huwa hayupo

1. Sasa hivi Zitto ni mgonjwa na yuko mapumzikoni unataka aache kujenga afya yake akaimu kitu ambacho automatically ni hadhi yake?

2. Mnyika amekaimu sana nafasi hiyo kipindi cha Uchaguzi ambao Dr. Slaa akiwa mgombea Uraisi wa chama na hivyo kushindwa kufanya kazi za ukatibu mkuu ki uwajibikaji Lazima akasimu madaraka, Zitto by then ane alikuwa mgombea wa Ubunge na alipewa kazi maalumu ya kuwanadi wagombea ubunge Vijana na kuimarisha kazi mara nyingi hakuweza kuwepo Dar Es Salaam ambako kazi za kila siku zinaongozwa tokea hapo , Myika ailkuwa mgombea wa Ubungo jimbo lilopo DSM na rahisi ku deal with agent issue

Kama kuna menginme sijui ila hayo ndio niyajuayo mkuu,

Am Signing Out,

Cheeeeeeeeeeeeeeeeerrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Back
Top Bottom