jiwe angavu
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 22,199
- 42,926
Wakuu habari.
Kama wewe ni mkazi ama umewahi ishi miji ya mwambao mwa ziwa Tanganyika utajionea anina nyingi sana ya samaki wakiwamo Migebuka,kuhe,dagaa kigoma n.k.
Ukiachilia mbali dagaa wa kigoma kupendwa na kuwa ni dagaa wanaongoza kuwa na bei kubwa nchini.
Migebuka ni moja ya samaki watamu na wenye virutubisho vingi na wakubwa ila wana soko dogo na bei ya chini na wanaliwa sana na wakazi wa pembezoni mwa ziwa Tanganyika.
Pamoja na yote hayo migebuka ama samaki wanaopatikana katika ziwa Tanganyika wamekua hawana soko ama umaarufu hapa nchini ukilinganisha na samaki wanao patikana ziwa Nyanza(Victoria).
Wafugaji wengi wa samaki wamejikita katika ufugaji wa samaki wanao patikana ziwa Nyanza hususani Sato na sangara..na ndio samaki wenye soko kubwa sana ndani na nje ya nchi.
Swali langu kwenu wa dau.
Je kipi kinafanya samaki hawa kutoka ziwa Tanganyika kuwa na soko hafifu ndani na nje ya nchi?
Je hawa samaki wanaweza kufungwa nje ya mazingira yao kama ilivyo sato ama kambare?
Nini kifanyike kuongeza ulaji na soko la hawa samaki kutoka ziwa Tanganyika?
#MaendeleoHayanaChama
Kama wewe ni mkazi ama umewahi ishi miji ya mwambao mwa ziwa Tanganyika utajionea anina nyingi sana ya samaki wakiwamo Migebuka,kuhe,dagaa kigoma n.k.
Ukiachilia mbali dagaa wa kigoma kupendwa na kuwa ni dagaa wanaongoza kuwa na bei kubwa nchini.
Migebuka ni moja ya samaki watamu na wenye virutubisho vingi na wakubwa ila wana soko dogo na bei ya chini na wanaliwa sana na wakazi wa pembezoni mwa ziwa Tanganyika.
Pamoja na yote hayo migebuka ama samaki wanaopatikana katika ziwa Tanganyika wamekua hawana soko ama umaarufu hapa nchini ukilinganisha na samaki wanao patikana ziwa Nyanza(Victoria).
Wafugaji wengi wa samaki wamejikita katika ufugaji wa samaki wanao patikana ziwa Nyanza hususani Sato na sangara..na ndio samaki wenye soko kubwa sana ndani na nje ya nchi.
Swali langu kwenu wa dau.
Je kipi kinafanya samaki hawa kutoka ziwa Tanganyika kuwa na soko hafifu ndani na nje ya nchi?
Je hawa samaki wanaweza kufungwa nje ya mazingira yao kama ilivyo sato ama kambare?
Nini kifanyike kuongeza ulaji na soko la hawa samaki kutoka ziwa Tanganyika?
#MaendeleoHayanaChama