Kwanini "maridhiano" yanaitaja sana CHADEMA?

Kwanini "maridhiano" yanaitaja sana CHADEMA?

Analogia Malenga

Platinum Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,292
Reaction score
10,842
Neno maridhiano limeshika kasi kwa siku za hivi karibuni. Lakini mjadala upo zaidi kwa CHADEMA. Maswali niliyonayo ni nini kilitokea?

Chadema hawakushiriki uchaguzi, je watafanya maridhiano gani kama sio kuyafuata waliyohahitaji kabla ya uchaguzi?

Lakini kama maridhiano ni matokeo ya kilichotokea Octoba 2025, ni nani aliathirika? CHADEMA au wananchi? Je wananchi ni CHADEMA?

Moja ya point yangu ni kuwa kama tunaenda kwenye Maridhiano kwa kichotokea Oktoba kuna haja ya kuchukua watu ambao wana influence kwa wananchi lakini hawana ukaribu na chama cha siasa.

Lakini kama maridhiano ni ya kuingia kwenye uchaguzi bila CHADEMA basi ni kweli chadema ni wa kuangaliwa kwa uzuri. Hata hivyo kuona CHADEMA kama key katika hili ni kunasibisha na kilichotokea kuwa kilikuwa cha Chadema.

Naishia hapo.
 
Hayo makundi mengine ukiacha cdm hawako tayari kulipa gharama ya kupata mabadiliko. Cdm ndio wamesimama kidete kwa zaidi ya miaka 15 wakitaka mabadiliko, kwa jasho na damu. Nyie makundi mengine jitajeni tuone msukumo wenye kwenye kupata mabadiliko.
 
Chadema ndio mwakilishi sahihi wa Watanzania. Heche na Lissu ndio watu wanaoaminika
Je haoini ni kuingia mtego kwamba watu walioathirika moja kwa moja wataonekana kuwa ni CHADEMA, which means inaweza kutumika against them baadae?
 
Hayo makundi mengine ukiacha cdm hawako tayari kulipa gharama ya kupata mabadiliko. Cdm ndio wamesimama kidete kwa zaidi ya miaka 15 wakitaka mabadiliko, kwa jasho na damu. Nyie makundi mengine jitajeni tuone msukumo wenye kwenye kupata mabadiliko.
Sijataja makundi, nimesema kama maridhiano ni matokeo ya Oktoba, je aliyeathirika oktoba ni nani? Chadema au wananchi? Je wananchi wale walikuwa CHADEMA? Au wananchi kwa ujumla regardless ya itikadi ya vyama?
 
Je haoini ni kuingia mtego kwamba watu walioathirika moja kwa moja wataonekana kuwa ni CHADEMA, which means inaweza kutumika against them baadae?
Haitabadilisha ukweli kwa kukaribisha hisia tu zitawale mahitaji halisi.Walikataa kukubali matakwa ya CHADEMA kuelekea uchaguzi wa Oktoba 29,2025,wananchi wakaamua.
 
Chadema ya Simba ni kama maji yani, usipoyanywa, utapikia, usipopikia utayaoga, usipooga ukurutu wako mkeo atasafishia mambo yake yani ndo maana haiishi midomoni kwa mama, mwegulu na kuendelea chini hadi kwa chawa wote mitandaoni na mitaani.

Lakini ujue nini? Chadema is here to stay, sio mama yao wala baba kakwete kanaweza kuiua! Watakufa wamfuate jiwe aliyejaribu kuiua, wasira alisema chadema itakufa angali kijana wakati nusu ya chawa hawajazaliwa hadi sasa keshafikia kupoteza kumbukumbu anakaribia kutangulia mbele ya haki pia.

Wataiacha... kiufupi ipo mioyoni mwa watanzania.

Chadema is not their league vijana chawa wala masisiemu mengine yote


Na wanajua, hivyooo yani!



 
Sijakuelewa, tumia maneno mengine
Kwamba, CHADEMA ikiwa ni key discussant maana yake walioathirika na Oktoba ni CHADEMA. Maana yake baada ya maridhiano watasema walioandamana Oktoba ni CHADEMA. Na hiyo ikatumika against them.
 
Sijataja makundi, nimesema kama maridhiano ni matokeo ya Oktoba, je aliyeathirika oktoba ni nani? Chadema au wananchi? Je wananchi wale walikuwa CHADEMA? Au wananchi kwa ujumla regardless ya itikadi ya vyama?
Kwa taarifa yako kilichotokea hiyo October kama cdm wangekubali kushiriki uchaguzi ingekuwa ni business as usual. Hakuna wananchi bila muongozo toka sehemu fulani. Vinginevyo utaje hao wananchi walikuwa wapi hadi kusubiri siku ya uchaguzi tu ambao cdm walisema hautafanyika. Kama ni wananchi waambie hata sasa Wadai hayo mabadiliko kama kuna yoyote atajitokeza kuongoza hayo mapambano.
 
Mnajidanganya tuu mbona Jana Rais wa JMT hajasema hayo? Na Maridhiano yanaanza mara moja.
 
Kwa taarifa yako kilichotokea hiyo October kama cdm wangekubali kushiriki uchaguzi ingekuwa ni business as usual. Hakuna wananchi bila muongozo toka sehemu fulani. Vinginevyo utaje hao wananchi walikuwa wapi hadi kusubiri siku ya uchaguzi tu ambao cdm walisema hautafanyika. Kama ni wananchi waambie hata sasa Wadai hayo mabadiliko kama kuna yoyote atajitokeza kuongoza hayo mapambano.
Mtego upo wapo, CHADEMA walisema hawashiriki au walisema wataenda barabarani?
 
Kwamba, CHADEMA ikiwa ni key discussant maana yake walioathirika na Oktoba ni CHADEMA. Maana yake baada ya maridhiano watasema walioandamana Oktoba ni CHADEMA. Na hiyo ikatumika against them.
Walioathirika ni wananchi, na walioudhika na ule unyama ni wananchi. Hao wananchi wanaona watu pekee wanaoguswa na shida zao na wanaowaamini ni Chadema.

Hata baada ya hicho kikao cha jana maoni mengi ilikuwa kama Chadema haipo ni kama wanapoteza muda tu.

Kuhusu Chadema waliandamana au lah kwa propaganda unaweza kusema hivyo, ila kisheria na facts itakuwa hoja ya kijinga kwa sababu haithibitishi kama Chadema waliandamana
 
Neno maridhiano limeshika kasi kwa siku za hivi karibuni. Lakini mjadala upo zaidi kwa CHADEMA. Maswali niliyonayo ni nini kilitokea?

Chadema hawakushiriki uchaguzi, je watafanya maridhiano gani kama sio kuyafuata waliyohahitaji kabla ya uchaguzi?

Lakini kama maridhiano ni matokeo ya kilichotokea Octoba 2025, ni nani aliathirika? CHADEMA au wananchi? Je wananchi ni CHADEMA?

Moja ya point yangu ni kuwa kama tunaenda kwenye Maridhiano kwa kichotokea Oktoba kuna haja ya kuchukua watu ambao wana influence kwa wananchi lakini hawana ukaribu na chama cha siasa.

Lakini kama maridhiano ni ya kuingia kwenye uchaguzi bila CHADEMA basi ni kweli chadema ni wa kuangaliwa kwa uzuri. Hata hivyo kuona CHADEMA kama key katika hili ni kunasibisha na kilichotokea kuwa kilikuwa cha Chadema.

Naishia hapo.
Ndio chama kikuu cha siasa Tanganyika
 
Walioathirika ni wananchi, na walioudhika na ule unyama ni wananchi. Hao wananchi wanaona watu pekee wanaoguswa na shida zao na wanaowaamini ni Chadema.

Hata baada ya hicho kikao cha jana maoni mengi ilikuwa kama Chadema haipo ni kama wanapoteza muda tu.

Kuhusu Chadema waliandamana au lah kwa propaganda unaweza kusema hivyo, ila kisheria na facts itakuwa hoja ya kijinga kwa sababu haithibitishi kama Chadema waliandamana
Now you get my point, kwamba ni mtego
 
Neno maridhiano limeshika kasi kwa siku za hivi karibuni. Lakini mjadala upo zaidi kwa CHADEMA. Maswali niliyonayo ni nini kilitokea?

Chadema hawakushiriki uchaguzi, je watafanya maridhiano gani kama sio kuyafuata waliyohahitaji kabla ya uchaguzi?

Lakini kama maridhiano ni matokeo ya kilichotokea Octoba 2025, ni nani aliathirika? CHADEMA au wananchi? Je wananchi ni CHADEMA?

Moja ya point yangu ni kuwa kama tunaenda kwenye Maridhiano kwa kichotokea Oktoba kuna haja ya kuchukua watu ambao wana influence kwa wananchi lakini hawana ukaribu na chama cha siasa.

Lakini kama maridhiano ni ya kuingia kwenye uchaguzi bila CHADEMA basi ni kweli chadema ni wa kuangaliwa kwa uzuri. Hata hivyo kuona CHADEMA kama key katika hili ni kunasibisha na kilichotokea kuwa kilikuwa cha Chadema.

Naishia hapo.
CDM ina ufuasi mkubwa sana alafu haina habari ya kupakwa mafuta kwa mgongo wa chipa.
 
Hayo makundi mengine ukiacha cdm hawako tayari kulipa gharama ya kupata mabadiliko. Cdm ndio wamesimama kidete kwa zaidi ya miaka 15 wakitaka mabadiliko, kwa jasho na damu. Nyie makundi mengine jitajeni tuone msukumo wenye kwenye kupata mabadiliko.
Wewe mwenyewe unataka maridhiano ?
 
Mtego upo wapo, CHADEMA walisema hawashiriki au walisema wataenda barabarani?
Sio kwamba tu walisema hawatashiriki, bali hata uchaguzi hautafanyika. Nitajie wananchi/kundi waliojitokeza hadharani kusema kuwa watazuia uchaguzi. Mnakaa kwa kujificha, wakijitoa muhanga wengine, na nyie mnajifanya mlikuwepo. Ndio maana nataka unitajie kundi lolote lililokuwa wazi kugomea uhuni zaidi ya cdm na kanisa Katoliki.
 
Back
Top Bottom