Kwanini Makamu wa Rais hasemi "Bwana Asifiwe"?

Kwanini Makamu wa Rais hasemi "Bwana Asifiwe"?

Tatizo umebebewa dini....

YOHANA MT. 7
16 Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma. 17 Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe. 18 Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
Kwa hiyo hiyo Yohana Mt 7 uliyoiweka hapo ndio inasema kuwa Yesu ni mtume?

Kwa staili hii Mtapata tabu sana.
 
Wakuu, heshima kwenu!

Ukifuatilia hafla nyingi za awamu hii ya 5, viongozi wamejijengea tabia ya kuanza hotuba zao kwa kutoa salamu kuu za kidini kama "Asalaam Aleiykum", " Tumsifu Yesu Kristo", "Bwana Yesu Asifiwe" nk

Imekuwa hivi sana kwa Mh. Rais Magufuli, Waziri Mkuu na pia kwa mawaziri na viongozi wengi wa juu.

Lakini hali ni tofauti kwa Makamu wa Rais, mama Samia. Ukifuatilia ufunguzi wa hotuba zake, huishia tu kusema "Asalaam Aleykum". Hasemi zile salamu nyingine za Wakristo.

Hii inajenga picha gani, wakuu?
Muslims don't believe in the Lordship of Jesus Christ. They go far claiming that he even didn't die on the cross.
 
Tuna dini za imani nyingi sana ikiwepo wapagani, ukiamua kutoa salam kwa kuzingatia dini au imani flani, fanya hivyo kwa imani zote kitu ambacho hakiwezekani.

Ingekua amri yangu salam za dini au zenye kuashiria imani flani zisingekuwepo kabisa kwenye hafla za kiserikali, hasa kama tukio halina maudhui ya kiimani.

Hata hivyo hakuapa kulinda salam za kiimani.
Wapagani salaam yao ni ipi?
 
Kwa hiyo hiyo Yohana Mt 7 uliyoiweka hapo ndio inasema kuwa Yesu ni mtume?

Kwa staili hii Mtapata tabu sana.
Mtapata tabu wangapi? Hapa ni mimi na wewe, tayari nimekupa mstari wa kitabu chako yesu akisema wazi kuwa alitumwa na Mungu, kwa maneno hayo tu yesu ni mtume full stop.

Turudi kwenye hoja, "Bwana asifiwe" ni salamu??
 
Your reply has just summed up all my assumptions of you. You might be 'holding' a master's degree but be entirely shallow minded, as you are.
If at all the gauge of your qualifications is projected by what you write here always, then clearly you are of no difference with a Standard 7 drop out.
You've nailed it.
 
Asalamu alaykum ni salamu na maamkizi kwa maana ni amani iwe juu yenu, haijalishi anayesalimiwa ni muislamu au siyo, lakini tumsifu Yesu Kristo au Bwana Yesu asifiwe siyo maamkizi kwani hata Yesu mwenyewe aliwafundisha wanafunzi wake waseme amani iwe kwenu Mat. 10:12 na Yesu mwenyewe alisema amani iwe kwenu John 20:19-21. Hivyo kuombeana amani kwa anayetaka amani ndiyo salamu na maamkizi bora hususan kwenye jamii ya watu wa imani tofauti.
Ingeekuwa vizuri kama angekuwa analitamka hivyo hivyo kwa kiswahili.
"Amani iwe juu yenu" ingeleta salamu za jumla kwa wanaomsikiliza, lakini akiingiza maneno ya kiarabu tayari inakuwa imegeuka salamu ya watu wenye imani fulani.
 
USILAZIMISHE MAMBO AISEE
Hahaha, naomba nirudie comment yangu hapa.

Wewe unasema "kila anayetumwa na Mwenyezi Mungu kuleta ujumbe anaitwa Mtume"... hiyo ni kwa mujibu wa kitabu gani?

Kama ni kwa mujibu wa Quran uko sahihi, na hayo ni mambo yenu...sisi wengine hatuyaingilii.

Ila Kwa mujibu wa Biblia, kila anayeleta ujumbe kutoka kwa Mungu HAITWI mtume.. ndio maana kuna Manabii kama Isaya, Hosea, Nahum, etc.. walileta ujumbe lakini HAWAKUWA MITUME na Biblia haijawaita Mitume, imewaita Manabii.

Na kuna mitume kama Paulo, Yohana etc walileta ujumbe, lakini hawaitwi Manabii, wanaitwa Mitume.

Sio lazima dini yako ifanane na ya mwingine na wala usifosi hilo. Wewe kaa na mtume Issa na tosheka hivyo.
Kumbe ishu ni lugha? Pole. Basi muhimu hapo ni kwamba yesu alitumwa kuja kuleta ujumbe wa Mungu kama aliyosema mwenyewe. Tumia lugha utakayo. Asante.
 
Tafuta hotuba za hayati Mzee Mkapa, utagundua na yeye akishasema Assalam aleykum alikuwa hasema Bwana Yesu asifiwe wala tumsifu Yesu Kristo
 
Ingeekuwa vizuri kama angekuwa analitamka hivyo hivyo kwa kiswahili.
"Amani iwe juu yenu" ingeleta salamu za jumla kwa wanaomsikiliza, lakini akiingiza maneno ya kiharabu tayari inakuwa imegeuka salamu ya watu wenye imani fulani.
Uko sahihi kabisa.
 
Yuko sahihi kwa imani yake
Wakuu, heshima kwenu!

Ukifuatilia hafla nyingi za awamu hii ya 5, viongozi wamejijengea tabia ya kuanza hotuba zao kwa kutoa salamu kuu za kidini kama "Asalaam Aleiykum", " Tumsifu Yesu Kristo", "Bwana Yesu Asifiwe" nk

Imekuwa hivi sana kwa Mh. Rais Magufuli, Waziri Mkuu na pia kwa mawaziri na viongozi wengi wa juu.

Lakini hali ni tofauti kwa Makamu wa Rais, mama Samia. Ukifuatilia ufunguzi wa hotuba zake, huishia tu kusema "Asalaam Aleykum". Hasemi zile salamu nyingine za Wakristo.

Hii inajenga picha gani, wakuu?
 
Tafuta hotuba za hayati Mzee Mkapa, utagundua na yeye akishasema Assalam aleykum alikuwa hasema Bwana Yesu asifiwe wala tumsifu Yesu Kristo
Mkapa kaingiaje hapa? We shule umeenda kweli? Au ndiyo walewale.
 
Kwanza huwa ni Makosa kwa Taifa ambalo sio la dini kuanza na salamu za kidni-hii ni unprofessional kabisa
 
Kumbe ishu ni lugha? Pole. Basi muhimu hapo ni kwamba yesu alitumwa kuja kuleta ujumbe wa Mungu kama aliyosema mwenyewe. Tumia lugha utakayo. Asante.
LUGHA?
Kwamba Nabii na Mtume ni sawa?
A prophet and an Apostle ni sawa?

Kwa reasoning hii unaweza hata kusema kuwa Rais na Mfalme ni sawa.

Mimi Najua umeshanielewa na umejifunza kitu. Ni vile tu huwezi kuadmit hapa.
 
Mtapata tabu wangapi? Hapa ni mimi na wewe, tayari nimekupa mstari wa kitabu chako yesu akisema wazi kuwa alitumwa na Mungu, kwa maneno hayo tu yesu ni mtume full stop.

Turudi kwenye hoja, "Bwana asifiwe" ni salamu??
Hahahaha... Ndio maana nikakuuliza hiyo verse Yesu anasema yeye ni MTUME?
Mwandishi wa hiyo verse (ambayo wewe binafsi huiamini) amesema Yesu ni MTUME?

Hilo hujalijibu mpaka sasa.

Nb:
Huwa sielewagi kwa nini Yesu wa kwenye Biblia (ambayo ninyi hamuiamini) huwa anawahangaisha sana.

Mbona wakristo hawanaga time kabisa na Issa wa Quran? Christian's don't give a damn
about the so called Issa!

Mbona huwa mnatumia nguvu nyingi sana kumuongelea huyo Yesu wa Biblia (ambayo hata hamuiamimi) na kujaribu kumlinganisha-linganisha?

Hivi Issa huwa hatoshi?
 
Nakuona mbal sanaa unafaa kua mchungaji kaka upige pesa uache kubishanaa unapoteza mda tu ni bora uanze kutangaza neno la mungu.
 
Back
Top Bottom