Kwanini Makamu wa Rais hasemi "Bwana Asifiwe"?

Kwanini Makamu wa Rais hasemi "Bwana Asifiwe"?

Analeta udini kwenye nchi secular kama hii sio,anataka kusema viongozi wetu wakristo na baadhi ya waislamu hawazipendi dini zao,ajiangalie kodi za watu wa dini zote zinamweka hapo wala yeye sio kiongozi wa dini.
 
Wakuu, heshima kwenu!

Ukifuatilia hafla nyingi za awamu hii ya 5, viongozi wamejijengea tabia ya kuanza hotuba zao kwa kutoa salamu kuu za kidini kama "Asalaam Aleiykum", " Tumsifu Yesu Kristo", "Bwana Yesu Asifiwe" nk

Imekuwa hivi sana kwa Mh. Rais Magufuli, Waziri Mkuu na pia kwa mawaziri na viongozi wengi wa juu.

Lakini hali ni tofauti kwa Makamu wa Rais, mama Samia. Ukifuatilia ufunguzi wa hotuba zake, huishia tu kusema "Asalaam Aleykum". Hasemi zile salamu nyingine za Wakristo.

Hii inajenga picha gani, wakuu?
Sasa mtu haziamini unatakaje? Unaelewa maana ya assalaam aleykum?
 
Kwani "Asalaam Aleykum" ni salamu ya kiislamu?
 
Wakuu, heshima kwenu!

Ukifuatilia hafla nyingi za awamu hii ya 5, viongozi wamejijengea tabia ya kuanza hotuba zao kwa kutoa salamu kuu za kidini kama "Asalaam Aleiykum", " Tumsifu Yesu Kristo", "Bwana Yesu Asifiwe" nk

Imekuwa hivi sana kwa Mh. Rais Magufuli, Waziri Mkuu na pia kwa mawaziri na viongozi wengi wa juu.

Lakini hali ni tofauti kwa Makamu wa Rais, mama Samia. Ukifuatilia ufunguzi wa hotuba zake, huishia tu kusema "Asalaam Aleykum". Hasemi zile salamu nyingine za Wakristo.

Hii inajenga picha gani, wakuu?
Huu Upupu Mtupu hakuna la maana apo
 
Muislamu hajawahi kuwa mnafiki kuhusu imani yake, atatenda dhambi yoyote lakini lakini atapigania la Mungu wake, nà muislamu akiamini ameamini kweli kweli. Ndio maana waislamu hupigania kuwa na maeneo ya kufanyia ibada kila mahali, vyuoni, viwanja vya ndege, na hospitali na ibada zao zinafanana.
Wakristo kwa asiri ni wanafiki, baada ya mitume kufa wamejiundia makampuni ya kidini(madhehebu), wanawaza kupiga ela, hawana ibada moja hawaelewani. Wachungaji wenyewe wanahuburi wasichokiamini. Kwa ufupi mkristo hayuko tayari kupigania jina la Mungu wake, ndiyo maana yuko tayari kutaja jina Mungu yeyote bila kujali.
In short ili uwe mkristo mzuri lazima uwe mnafiki kwa jina la Mungu wako na kwa Mungu wako mwenyewe.
 
Sasa kama hataki kusema salamu za wengine hata ya dini yake akaushie tu Serikali haina dini
 
Wakristo hawana mtume anayeitwa Yesu. Acha kulazimisha vitu
Nadhani kila mwenye akili anaamini kuwa binadamu anayetumwa na Mwenyezi Mungu kuleta ujumbe kwa wanadamu anaitwa Mtume, kwa mujibu wa biblia Yesu anasema alitumwa na Mungu, sasa wewe unapinga umekuwa nani? Tulizana.
 
Hata kikabila unaweza kusalimia ,alimuradi umetoa salamu na imefahamika kuwa ni salamu.
Ila kutoa salamu kwa kitu ambacho sio chako ni kujitoa fahamu na wengi wanaofanya hivyo hawaeleweki hata kwenye hotuba zao,peleleza.
 
Wakuu, heshima kwenu!

Ukifuatilia hafla nyingi za awamu hii ya 5, viongozi wamejijengea tabia ya kuanza hotuba zao kwa kutoa salamu kuu za kidini kama "Asalaam Aleiykum", " Tumsifu Yesu Kristo", "Bwana Yesu Asifiwe" nk

Imekuwa hivi sana kwa Mh. Rais Magufuli, Waziri Mkuu na pia kwa mawaziri na viongozi wengi wa juu.

Lakini hali ni tofauti kwa Makamu wa Rais, mama Samia. Ukifuatilia ufunguzi wa hotuba zake, huishia tu kusema "Asalaam Aleykum". Hasemi zile salamu nyingine za Wakristo.

Hii inajenga picha gani, wakuu?
Unataka aseme hizo salamu kwa faida gani?
Huu udini tunaoletewa na hii awamu ya tan tutakuja kuulipia na itatugharimu sana. Kiongozi anakuwa mdini wa waziwazi halafu anafunika kwa kuwachanganyia salamu! Kama kweli angekuwa na nia ya kuonesha maelewano na mashirikiano baina na watu wa dini mbalimbali tuongeona hivyo hata katika muundo wa serikali yake. Hizi hotuba za kanisani anapokwenda kusali jumapili, ingekuwa ni rais muislam amefanya hivyo msikitini tungesikia malalamiko ya wakristo kuhusu udini. Lakini waislamu wamenyamaza. Ni funzo kubwa, litusaidie mbele ya safari.

Kwenye salamu. Maneno "Assalaam alaykum" yanamaanisha amani iwe nanyi. Kila mtu anapenda amani, bila kujali ni dini gani.
Lakini salamu ya "Tumsifu Yesu Kristo" au "Bwana Asifiwe" inajulikana ni ya wakristo tu wanasisitiza kumsifu Yesu, lakini sio jambo universal linalokubalika kwa wote. Ukimlazimisha asiyekuwa mkristo kusalimia kikristo au kujibu imani ya kikristo unamuonea na kumdhalilisha kiimani. Kila mwenye imani yake aifuate, tusilazimishane.
Kwahiyo nasema salamu ya kutakiana amani inafaa kwa watu wote, na hivyo makamu wa rais yuko sahihi 100% kutumia salamu hiyo kwa umma wote. Na pia yuko sahihi kuziacha hizo salamu nyingine zinazogawa watu.
Kama kuna mtu ambaye hata hiyo assalaam alaykum inamkera, basi asalimie tu kiserikali kwakuwa kwanza kabisa serikali haina dini.
 
Suluhisho ni kusalimiana kiserikali tu. Salamu za kidini pelekeni huko mnakoabudu, zitaitikiwa kwa imani, heshima na uchaji.
Salamu za kidini nje ya imani ni kukejeliana tu. Mtu anawaambia watu "asaramareko", unatarajia wanaichukulia serious hiyo salaam?
 
Waseme tu tanzania oyeeeeh basi inatosha, wanaposalimia kuwakilisha dini zao inaleta ukakasi kwa ambao si wa imani yao, Maana watajiona kumbe hawatambuliki na kiongozi wao.
 
Nadhani kila mwenye akili anaamini kuwa binadamu anayetumwa na Mwenyezi Mungu kuleta ujumbe kwa wanadamu anaitwa Mtume, kwa mujibu wa biblia Yesu anasema alitumwa na Mungu, sasa wewe unapinga umekuwa nani? Tulizana.
Hiyo Biblia unayoinukuu kwa kusema "kwa mujibu wa biblia" inasema Yesu nani?

Hiyo Biblia unayoirefer hapo ina mahali popote inaposema Yesu ni mtume?

Hiyo Biblia unayoisema hapo (ambayo wewe binafsi huiamini) imezungumza sana na imesema sana kuwa Yesu ni nani, Tena imesema kwa uwazi kabisa.

Sasa tulizana mzee, huyo Yesu wa kwenye Biblia achana naye wala asikupe tabu, wewe komaa na mtume Issa wa kwenye Quran, huyo ndio mtume wenu kwa mujibu wa kitabu chenu... Usilazimishe mambo.
 
Hiyo Biblia unayoinukuu kwa kusema "kwa mujibu wa biblia" inasema Yesu nani?

Hiyo Biblia unayoirefer hapo ina mahali popote inaposema Yesu ni mtume?

Hiyo Biblia unayoisema hapo (ambayo wewe binafsi huiamini) imezungumza sana na imesema sana kuwa Yesu ni nani, Tena imesema kwa uwazi kabisa.

Sasa tulizana mzee, huyo Yesu wa kwenye Biblia achana naye wala asikupe tabu, wewe komaa na mtume Issa wa kwenye Quran, huyo ndio mtume wenu kwa mujibu wa kitabu chenu... Usilazimishe mambo.
Tatizo umebebewa dini....

YOHANA MT. 7
16 Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma. 17 Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe. 18 Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
 
Nadhani kila mwenye akili anaamini kuwa binadamu anayetumwa na Mwenyezi Mungu kuleta ujumbe kwa wanadamu anaitwa Mtume, kwa mujibu wa biblia Yesu anasema alitumwa na Mungu, sasa wewe unapinga umekuwa nani? Tulizana.
Na nikusaidie kitu kingine... unasema "kila anayetumwa na Mwenyezi Mungu kuleta ujumbe anaitwa Mtume"... hiyo ni kwa mujibu wa kitabu gani?

Kama ni kwa mujibu wa Quran uko sahihi, na hayo ni mambo yenu...sisi wengine hatuyaingilii.

Ila Kwa mujibu wa Biblia, kila anayeleta ujumbe kutoka kwa Mungu HAITWI mtume.. ndio maana kuna Manabii kama Isaya, Hosea, Nahum, etc.. walileta ujumbe lakini HAWAKUWA MITUME, waliitwa Manabii.

Na kuna mitume kama Paulo, Yohana etc walileta ujumbe, lakini hawaitwi Manabii, wanaitwa Mitume.

Sio lazima dini yako ifanane na ya mwingine na wala usifosi hilo. Wewe kaa na mtume Issa na tosheka hivyo.
 
Tatizo umebebewa dini....

YOHANA MT. 7
16 Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma. 17 Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe. 18 Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
USILAZIMISHE MAMBO AISEE
Hahaha, naomba nirudie comment yangu hapa.

Wewe unasema "kila anayetumwa na Mwenyezi Mungu kuleta ujumbe anaitwa Mtume"... hiyo ni kwa mujibu wa kitabu gani?

Kama ni kwa mujibu wa Quran uko sahihi, na hayo ni mambo yenu...sisi wengine hatuyaingilii.

Ila Kwa mujibu wa Biblia, kila anayeleta ujumbe kutoka kwa Mungu HAITWI mtume.. ndio maana kuna Manabii kama Isaya, Hosea, Nahum, etc.. walileta ujumbe lakini HAWAKUWA MITUME na Biblia haijawaita Mitume, imewaita Manabii.

Na kuna mitume kama Paulo, Yohana etc walileta ujumbe, lakini hawaitwi Manabii, wanaitwa Mitume.

Sio lazima dini yako ifanane na ya mwingine na wala usifosi hilo. Wewe kaa na mtume Issa na tosheka hivyo.
 
Back
Top Bottom