Kwanini mabibi harusi wengi wanapenda kulia siku ya ndoa?

Kwanini mabibi harusi wengi wanapenda kulia siku ya ndoa?

Bwana Harusi, kwanza hongera kwa kutekeleza wajibu wako kwa jamii, wazazi na kwa Mungu kwa kufunga Ndoa!

Ni mara chache sana siku hizi kuona Bibi Harusi akitoa machozi siku ya Harusi. Wengi wao macho makavu kuangalia zawadi gani imetoka na nani ametoa - kibiashara zaidi!

Kwa maoni yangu hakuna atakayekuja na jibu moja kuhusu kwa nini Bibi Harusi atoe machozi siku ya Harusi.

Vilevile kwa maoni yangu usimuulize Mkeo sababu ya kutoa machozi. Tunza hiyo kumbukumbu ikufariji katika kila utakapopitia katika vipindi vigumu huko mbele. Just treasure the memory - it is unique!

Mpende na kumuheshimu Mkeo. Fanya kazi halali kwa bidii ili utunze familia yako. Siku za Ibada (bila kujali imani yenu) nendeni kusali - pamoja! Mtangulizeni MUNGU katika maisha yenu - A Family Which Prays Together, Stays Together!

Mungu abariki kazi za mikono na akili zenu na awajalie kila lililo la heri katika maisha yenu. Awajalie maisha marefu ya furaha na ya mafanikio - muishi kuona na kufurahia mafanikio ya wajukuu ma vitukuu wenu! Amina.

Wataalamu watakuja na majibu zaidi!

nimejifunza ktu kutoka kwako asante xana mkuu
 
Kuna sababu nyingi:-

1) Anamkumbuka ex au ma-ex waliomtenda na kumwacha bila kumwoa lakini wewe umekamilisha ahadi.

2)Anajaribu ku imagine maisha mapya na mtu mpya ambayo hana uhakika yatakavyoenda/hatma yake.

3) Kuiacha familia yake ya tangu anazaliwa, atawa miss wapendwa wazazi na ndugu zake.

4) Machozi ya furaha, kwamba hatimaye analiosha gundu kwa kuolewa 😉 tena pengine na her dream husband(dream come true). Akitafakari jinsi unavyompenda na kuona kama anaota vile,,mbona wale wa nyuma walimtenda hivyo huyu malaika sijui ametoka wapi, " he must be sent from heaven" 🙂

5) Mwingine anawaza madeni aliyoingia kwasababu ya harusi, namna atakavyo yalipa, shida alizozipitia kipindi cha maandalizi ya harusi ambayo hatimaye imekua. Mwingine anagharamika kusudi ajionyeshe vilivyo siku ya harusi yake hahah.

Wengine watamalizia.
 
Wengi nlowashuhudia wakilia sana kwenye harusi zao unakuta mtu anakua anafuraha na alitamani mtu fulani angekuepo ashare nae furaha hiyo mfano wazazi wake, Na kwa bahati mbaya hawapo.
 
Labda huwa wanawaza namna walivyo "tendwa" mara kadhaa siku za nyuma . Na ile hofu kwamba itakuwaje na huku nikitendwa? Kiujumla ni kukosa kujiamini labda.
 
kwenda kuanza maisha mapya na yeye kuwa ndiye mwanzilishi wa familia kwake ni jambo gumu, je litawezekanaje
 
Pitia mkanda wa harusi utaona jamaa aliyemkumbatia kwa sekunde nyingi na kumnong'oneza neno....labda alimwambia "nashukuru Suzy" au " Ndio umeamua kuolewa na huyu sio" au "naomba usinisahau" au "kwa nini umenifanyia hivi Suzi"....any way, yeye ndiye anajua vizuri.

Mpige kabali mpaka aseme jamaa alitamka nini mpaka akaanza kulia.
 
Bwana Harusi, kwanza hongera kwa kutekeleza wajibu wako kwa jamii, wazazi na kwa Mungu kwa kufunga Ndoa!

Ni mara chache sana siku hizi kuona Bibi Harusi akitoa machozi siku ya Harusi. Wengi wao macho makavu kuangalia zawadi gani imetoka na nani ametoa - kibiashara zaidi!

Kwa maoni yangu hakuna atakayekuja na jibu moja kuhusu kwa nini Bibi Harusi atoe machozi siku ya Harusi.

Vilevile kwa maoni yangu usimuulize Mkeo sababu ya kutoa machozi. Tunza hiyo kumbukumbu ikufariji katika kila utakapopitia katika vipindi vigumu huko mbele. Just treasure the memory - it is unique!

Mpende na kumuheshimu Mkeo. Fanya kazi halali kwa bidii ili utunze familia yako. Siku za Ibada (bila kujali imani yenu) nendeni kusali - pamoja! Mtangulizeni MUNGU katika maisha yenu - A Family Which Prays Together, Stays Together!

Mungu abariki kazi za mikono na akili zenu na awajalie kila lililo la heri katika maisha yenu. Awajalie maisha marefu ya furaha na ya mafanikio - muishi kuona na kufurahia mafanikio ya wajukuu ma vitukuu wenu! Amina.

Wataalamu watakuja na majibu zaidi!
Aisee uko vizuri.Natamani na mimi unisemee haya maneno yawe yangu.Barikiwa sana mkuu
 
Anasikitikia atakavyo gegedwa bure..... just kidding bana. Huwa ni machozi ya furaha maana hayawi hayawi sasa yamekuwa anakumbukia na waliotoka nduki bila kuaga.
 
Bwana Harusi, kwanza hongera kwa kutekeleza wajibu wako kwa jamii, wazazi na kwa Mungu kwa kufunga Ndoa!

Ni mara chache sana siku hizi kuona Bibi Harusi akitoa machozi siku ya Harusi. Wengi wao macho makavu kuangalia zawadi gani imetoka na nani ametoa - kibiashara zaidi!

Kwa maoni yangu hakuna atakayekuja na jibu moja kuhusu kwa nini Bibi Harusi atoe machozi siku ya Harusi.

Vilevile kwa maoni yangu usimuulize Mkeo sababu ya kutoa machozi. Tunza hiyo kumbukumbu ikufariji katika kila utakapopitia katika vipindi vigumu huko mbele. Just treasure the memory - it is unique!

Mpende na kumuheshimu Mkeo. Fanya kazi halali kwa bidii ili utunze familia yako. Siku za Ibada (bila kujali imani yenu) nendeni kusali - pamoja! Mtangulizeni MUNGU katika maisha yenu - A Family Which Prays Together, Stays Together!

Mungu abariki kazi za mikono na akili zenu na awajalie kila lililo la heri katika maisha yenu. Awajalie maisha marefu ya furaha na ya mafanikio - muishi kuona na kufurahia mafanikio ya wajukuu ma vitukuu wenu! Amina.

Wataalamu watakuja na majibu zaidi!


Hekima tupu aisee bwana harusi unabahati sanaaaa
 
Furaha ilochanganyikana na hofu, uogauoga, kutoamini kama kweli anaolewa, hisia kali, umati wa watu, vigelegele, shangwe, vifijo na nderemo…………
 
Nhuuuhhhh!
Hahaha unaguna? ?? Ndio hivyo...kwangu mimi nililia nikiwaza hapo tu....nilivyokuwa najaliwa na kupendwa home na kupewa hitaji lolote..je mume atafanya km kwetu...especially km mimi ni lastborn naondoka uwiii...upweke wanaobakinao lol
 
Back
Top Bottom