Mnyamwezi wa Urambo
JF-Expert Member
- Dec 7, 2011
- 927
- 274
Huyu ndiyo LAIGWANAN a.k.a the next Presidaaaahhh!!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna anayebishaaaaaa??
Huyu ndiyo LAIGWANAN a.k.a the next Presidaaaahhh!!
Siku atakapoongelea ufisadi -- hasa ufisadi wa ngazi za juu (siyo rushwa za matrafiki na manesi) nitampa kura yangu bila kufikiri mara mbili -- iwapo atagombea urais.
Nimekuwa nafuatilia kwa ukaribu sana hotuba na kauli za Lowassa akiwa sehemu mbali mbali hapa nchini na kuonyesha kero zake katika masuala mbali mbali katika jamii ambayo anayaona hayaendi vizuri. Mfano ni ajira kwa vijana, elimu duni na kadhalika.
Yote hayo ni sahihi, lakini mwanasiasa huyu mkongwe inabidi ajiulize kwa nini masuala hayo yamekuwa ni chagamoto kubwa kwa jamii ya Tanzania. Jee hataki kukubali kabisa kwamba ufisadi katika ngazi za juu za uongozi wa serikali inayoongozwa na chama chake ndiyo kwa kiasi kikubwa unachangia serikali hiyo kushindwa kutatua masuala hayo?
Haamini kwamba sehemu kubwa za bajeti zinazopangiwa sekta mbali mbali za maendelea zinaishia mifukoni mwa wachache? Haamini kwamba mikataba ya siri ya makampuni ya uchimbaji wa madini, mafuta na gesi ni ufisadi mtupu na ndiyo maana iko siri?
La mwisho: Lowassa haziamini kabisa habari kwamba wapo vigogo wachache waliowekewa fedha katika mabenki ya Uswisi na makampuni ya nje yanayojishughulisha na utafutaji/uchimbaji wa gesi hapa nchini -- na kwa nini hata siku moja hazungumzii suala hilo ambalo wananchi wengi wanachukizwa nalo? Haoni kwamba serikali inapiga danadana tu katika kuwabaini akina nani hao na kudai kuzirejesha?
hahaha, umemchana mno aisee, hata mkewe atakuwa anamuwaza lowasa....hahahamkuu umelala unamuwaza lowassa,kila utakacho gusa nchi hii ni lowassa,lowassa!hata mkeo atakuwa anamuwaza lowassa