Kwanini kusiwe na chombo cha kusimamia michakato ya ndani ya vyama vya siasa, ikiwezekana kushtaki?

FPT

JF-Expert Member
Mar 23, 2017
1,201
1,839
Tumeona baadhi ya wanachama wa vyama wakikimbilia mahakamani kutafuta haki kwa nafasi zinazohusu uongozi ndani ya vyombo vya dola kama bunge na serikali kama ilivyotokea kwa wabunge 19 wa CHADEMA.

Hapa tunaona wabunge wanaweza kukimbilia mahakamani kutafuta haki ambayo pengine wasingeweza kupata kupitia kamati/vikao vya vyama vyao. Je, kwa nini usiwepo utaratibu wa kupya atikana kwa haki nje ya haki kutendwa na kamati za maadili kwa wanachama ambao nafasi zao hazitokani na vyombo vya dola?

Sitaki kukumbusha ya nyuma lakini tunaweza kuanzia kwenye suala la Membe, mzee Kinana ili tupate kwenye ufumbuzi. Binafsi ninaamini kwa masuala ya kimaadili ya mwanacham si vyema yakajadiliwa na kuamuliwa na kamati zinazohusiana na chama moja kwa moja na badala yake kiundwe chombo huru kama mahakama kwa ajili ya maamuzi na hii itaondoa uminywaji wa haki.

Kwa kinachotokea sasa kwenye kesi ya wabunge 19 was CHADEMA ni matokeo ya kutokuwa na utendaji wa haki wa kamati za maadili ya chama na ni vizuri wao wana upande mwingine wa kupata haki. Hivi inakuja akilini kweli wajumbe wa kikao kilichoniadhibu wajumbe haohao wanavaa uhusika mwingine wa kunisikiliza ?

Natambua eneo hili ndio linafanya wanachama kuumia bila kuwa na pa kusemea kama nafasi zao hazitokani na vyombo vya dola.

Tunaweza hata kuanzisha tawi mahakama kuu kwa ajili ya kusikiliza mashauri ya namna ama kukawa na chombo huru cha kusikiliza mashauri ya namna hii na sio kutegemea kamati za maadili za vyama na kwa kufanya hivi ni kama kesi ya ngendere kula mahindi amepelekewa nyani ahukumu
 
..hivi inaingia akilini Msajili wa vyama vya siasa awe mteuliwa wa Raisi na Mwenyekiti wa Ccm?

..Au vyama vya siasa vinaweza kutendewa haki na Mahakimu na Majaji ambao ni wateuliwa wa Raisi na Mwenyekiti wa Ccm?
 
Ndio mlikuwa mnashawishi Kenya kuhusu uchaguzi. Wakenya wakidhani Sisi wote ni wajima. Hizi siasa zitawaeumbua. Chedema ni very robust sana. Wakipiga shambulizi huwa mankimbia hoja mtu.
Jemgeni chama,zaidi ya chadema kutaibuka mastar WA siasa mkiwa mmelala fofofo....mtajikuta hamjajiandaa.
 
Mahakama iko huru? Nikikuteua ni lazima ufuate matakwa yangu vinginevyo nitakufukuza kazi, hili halina mjadala.
 
Mahakama iko huru? Nikikuteua ni lazima ufuate matakwa yangu vinginevyo nitakufukuza kazi, hili halina mjadala.
Katiba za vyama zikishafikia vigezo vya usajili . Zinakuwa msingi.

Fikriinie mbinu za maana kuliko kudanganyana na ushausi kichaa. Mtalipuliwa majukwaani vibaya Hadi msajili na wengine wakose nguvu kabisa ya kukemea ukweli katika jambo lingine
 
Katiba za vyama zikishafikia vigezo vya usajili . Zinakuwa msingi.

Fikriinie mbinu za maana kuliko kudanganyana na ushausi kichaa. Mtalipuliwa majukwaani vibaya Hadi msajili na wengine wakose nguvu kabisa ya kukemea ukweli katika jambo lingine
Kiswahili chako kigumu.
 
Katiba ya chama ndio msingi wa chama. Zote zitatakiwa zifikie vigezo vya Sheria za nchi. Zikifuatwa chama tawala hakiwezi ingilia ndio maana ccm wanashindwa vibaya majukwaani. Kulazimisha fanya vyama vingine houseboys wao waingilie watakavyo na ku control narrations
 
Mahakama iko huru? Nikikuteua ni lazima ufuate matakwa yangu vinginevyo nitakufukuza kazi, hili halina mjadala.
Sio lazima vyombo vya maamuzi viteuliwe na Rais na pia sio kweli Rais asipoteua chombo kinakuwa huru, ninavyoona kinachotakiwa kufanywa ni haki katika usikilizwaji wa shauri la mwanachama.

Mahakama ni chombo huru kutokana na kwamba hukumu inatolewa kwa kumsikiliza kila MTU. Je, mdee na wenzake walipatiwa nafasi ya kusikilizwa ?
 
Sio lazima vyombo vya maamuzi viteuliwe na Rais na pia sio kweli Rais asipoteua chombo kinakuwa huru, ninavyoona kinachotakiwa kufanywa ni haki katika usikilizwaji wa shauri la mwanachama.

Mahakama ni chombo huru kutokana na kwamba hukumu inatolewa kwa kumsikiliza kila MTU. Je, mdee na wenzake walipatiwa nafasi ya kusikilizwa ?
Uhuru unaousema ni wa kesi zisizohusu wanasiasa wa upinzani, kumbuka viongozi wengi wa Chadema walifungwa bila kosa na wakatolewa kwa agizo la rais baada ya kutumikia sehemu ya vifungo.
 
Sio lazima vyombo vya maamuzi viteuliwe na Rais na pia sio kweli Rais asipoteua chombo kinakuwa huru, ninavyoona kinachotakiwa kufanywa ni haki katika usikilizwaji wa shauri la mwanachama.

Mahakama ni chombo huru kutokana na kwamba hukumu inatolewa kwa kumsikiliza kila MTU. Je, mdee na wenzake walipatiwa nafasi ya kusikilizwa ?

Mahakama inapaswa kuwa huru, lakini kwa sasa ni nadra kupata haki mahakamani kwani mifumo karibia yote ni uozo. Na sababu hasa ni CCM kukaa madarakani muda mrefu kwa shuruti, matokeo yake hata taasisi za kimamlaka zinabeba uchovu wa CCM.
 
Mahakama inapaswa kuwa huru, lakini kwa sasa ni nadra kupata haki mahakamani kwani mifumo karibia yote ni uozo. Na sababu hasa ni CCM kukaa madarakani muda mrefu kwa shuruti, matokeo yake hata taasisi za kimamlaka zinabeba uchovu wa CCM.
Kukaa madarakani kwa CCM haimaanishi kimechoka kimawazo kwa sababu kila baada ya kipindi Fulani wanaingia wapya uongozini na hiyo inamaanisha mawazo mapya yanaingia. Tujiulize kwa miongo miwili aliyokaa mbowe madarakani CHADEMA wategemee jipya lipi kutoka kwako?

Mifumo inabadilishwa na watu wapya na sio vyama vipya na ndio maana CCM kimeendelea kuchaguliwa kutokana na kuweza kujibadilisha kupitia kubadilisha watu. CHADEMA ndio imeonyesha uchovu kwa kushindwa kuwa na mawazo mapya kutoka kwa watu wapya.
 
Kukaa madarakani kwa CCM haimaanishi kimechoka kimawazo kwa sababu kila baada ya kipindi Fulani wanaingia wapya uongozini na hiyo inamaanisha mawazo mapya yanaingia. Tujiulize kwa miongo miwili aliyokaa mbowe madarakani CHADEMA wategemee jipya lipi kutoka kwako?

Mifumo inabadilishwa na watu wapya na sio vyama vipya na ndio maana CCM kimeendelea kuchaguliwa kutokana na kuweza kujibadilisha kupitia kubadilisha watu. CHADEMA ndio imeonyesha uchovu kwa kushindwa kuwa na mawazo mapya kutoka kwa watu wapya.

Nimecheka kwa nguvu, eti CCM kinaendelea kuchaguliwa. Huko kuchaguliwa kwenyewe ni kama ule uchaguzi wa 2020? Kwani Mbowe ndio alikuwa anagombea urais hadi useme hakuna sura mpya? Tunataka uchaguzi huru na box la kura liheshimiwe ili tupime CDM kukataliwa na watu. Sio mnasema CDM imechokwa, lakini kwenye uchaguzi wakurugenzi wanakimbia ofisi ili wasipokee fomu za CDM, au kuwaengua wagombea wao ili CCM wapite bila kupingwa.
 
Nimecheka kwa nguvu, eti CCM kinaendelea kuchaguliwa. Huko kuchaguliwa kwenyewe ni kama ule uchaguzi wa 2020? Kwani Mbowe ndio alikuwa anagombea urais hadi useme hakuna sura mpya? Tunataka uchaguzi huru na box la kura liheshimiwe ili tupime CDM kukataliwa na watu. Sio mnasema CDM imechokwa, lakini kwenye uchaguzi wakurugenzi wanakimbia ofisi ili wasipokee fomu za CDM, au kuwaengua wagombea wao ili CCM wapite bila kupingwa.
Wagombea wote wa CHADEMA kama wangeshinda Urais wangekuwa kivuli cha Mbowe tu. Kwa siasa zetu hususani za CHADEMA Rais ana nguvu zaidi akiwa mwenyekiti sasa fikiri Slaa, Lowassa na Lissu wangewezaje kuchezea sharubu?

Kumbuka Mbowe alijitangaza kuteuliwa uwaziri mkuu kama Lissu angeshinda
 
Wagombea wote wa CHADEMA kama wangeshinda Urais wangekuwa kivuli cha Mbowe tu. Kwa siasa zetu hususani za CHADEMA Rais ana nguvu zaidi akiwa mwenyekiti sasa fikiri Slaa, Lowassa na Lissu wangewezaje kuchezea sharubu?

Kumbuka Mbowe alijitangaza kuteuliwa uwaziri mkuu kama Lissu angeshinda

Labda hujui nguvu aliyo nayo rais kwa katiba hii. Kwa post hii nimejua uwezo wako katika uga wa siasa.
 
Back
Top Bottom