NasDaz Nyerere ndio aliyejenga Reli ya TAZARA, reli hii kwakweli ilikua ya kisasa kweli enzi zile, mara ya mwisho nilipanda mwaka 1994 nilipokua nasoma kule Iringa, enzi ya Nyerere huyo huyo ndie aliyeongeza kipande kilicho achwa na mkoloni cha reli ya kati kuja Ubungo maziwa, mahali ambapo Mwakyembe amezindua huo unaoitwa mradi kuondoa kero za Barabarani jijini Dar, Kenye wame copy mfumo wa elimu bure toka kwa Nyerere ambaye wakati huo (enzi za Moi) walikua wanatudharau sana kwakusema, kama unapenda vitu vya bure, hamieni Tanzania, leo hii hata ccm nao wanataka kurudi kule, kama tumewahi kupewa chakula cha bure, kama nitakosea, watu wazima naomba mnisahihishe, ilikua ni mwaka 1982 nafikiri, hii ni mara baada ya ukame mkubwa kuikumba nchi yetu, enzi za Nyerere kulikua na akiba ya chakula cha kutosha kabisa, kuna vihenge vilijengwa pale Iringa, Dar, Mbeya na hata mashirika kama NAFCO yalifanya vizuri sana, enzi za Nyerere, (naomba mwongozo wako hapa) pembejeo gani za kilimo tulikua tunanunua toka nje? Nakumbuka tulikua na viwanda kama UFI Dar pale, ZZK Mbeya, kiwanda cha madawa ya mifugo na mazao Moshi /Arusha, Pareto Mafinga, Karatasi Mgororo-Iringa, Mbolea Tanga n.k Kama sikosei, wakulima wa Pamba wa Kanda ya Ziwa hasa Maswa, Bariadi n.k, walikua wanauwezo wa kufanya vitu vingi tu kwa kutegemea Kilimo sababu, soko lilikuwepo, viwanda vya nguo vilikuwepo karibu kila mkoa unaozalisha Pamba, Wahaya waliweza kusomesha vijana wao kwa kilimo cha Kahawa.
Nataka niseme hivi, enzi za Nyerere, vitega uchumi vilikua vichache sana na vipaumbele vilizingatiwa, nikiwa mdogo, niliona huo ujenzi wa Barabara unaousema ulifanyika pia enzi hizo, Barabara ya tokea Makambako to Songea, ulifanyika enzi za mzee huyu, Bwawa la Mtera, Kidatu n.k. Yote haya Nyerere alikua akifanya ilihali akipata upinzani mkubwa sana toka nchi za Magharibi na Africa ya Kusini, inawezekana siasa ya Ujamaa ndio tatizo, lakini tujiulize, hivi mara baada ya kuingia Ubepari huu leo, nchi inasonga au inarudi nyuma? Thamani ya Tsh dhidi ya Dola ilikua 1:40, karibu kila kinacho sababisha pesa leo, kilianzishwa na Nyerere, aliweka msingi, tena Imara but mchwa wamekuja, wanatafuna kweli, hiki kinacho onekana kama wamefanya ni tone tu la kile tulichotakiwa kukiona!
I am also an Independent thinker and not pro anybody!