Kwanini Kenya wanapenda sifa sana?

Kwanini Kenya wanapenda sifa sana?

Nazdas
kusema kuwa matatizo tuliyonayo leo yamesababishwa na nyerere unakuwa unakosea.
Kwanza kipindi cha nyerere kulikuwa na viwanda vingi sana ambavyo waliofuata walishindwa kuviendeleza.
Kipindi cha nyerere thaman ya shiling ya tanzania ilikuwa iko juu tofauti na sasa.
Tatizo la tz sio nyerere bali ni ubinafsi wa viongozi wetu walioshindwa kuendeleza msingi mzuri alioacha nyerere. Viwanda walivyobinafsisha vingi havifanyi kazi. Wameingia mikatabaa ya kifisadi tu, watu wananunua mashirika ya umma halafu wanang'oa mashine wanauza kiwanda wanafufunga. Nyerere aliweza kujenga reli ya tazara lakini mpaka leo waliomfuatia wameshindwa kujenga reli nyingine mpya na zilizokuwepo wanaziua
 
Sheriff, asante kwa lugha ya picha, Kenya wako mbele sana ya Tanzania, hili halina ubishi hata kidogo!
 
kwa nini wasiwe na mkonga mmoja kama wa kwetu?

kuwa na mikonga 5 maana yake nini ?

sisi tuko wengi zaidi lakini nashangaa hatuna spidi kama hawa jamaa

Kenya plans to land 5th undersea cable | balancingact-africa.com
Sio kwamba wanapenda sifa, wanastahili sifa, ccm wakisema hatutaki tuwe kama majirani zetu mwaka 2007 walivyo twangana ni cheap politics ambazo zinaelekeza to the negative side, ukiangalia positive ni nyingi zaidi e.g, katiba mpya, barabara za mjini nairobi, data infrastructure kama uliyotolea mfano, vita ya alshabab somalia, usafiri wa reli, barabara na anga unaboreshwa kila siku etc..
what about beautiful Tanzania, tunaweka mikakati, tupo mbioni kutafta mkandarasi, tunakusanya maoni, tunasubiri development partners etc
 
Nazdas
kusema kuwa matatizo tuliyonayo leo yamesababishwa na nyerere unakuwa unakosea.
Kwanza kipindi cha nyerere kulikuwa na viwanda vingi sana ambavyo waliofuata walishindwa kuviendeleza.
Kipindi cha nyerere thaman ya shiling ya tanzania ilikuwa iko juu tofauti na sasa.
Tatizo la tz sio nyerere bali ni ubinafsi wa viongozi wetu walioshindwa kuendeleza msingi mzuri alioacha nyerere. Viwanda walivyobinafsisha vingi havifanyi kazi. Wameingia mikatabaa ya kifisadi tu, watu wananunua mashirika ya umma halafu wanang'oa mashine wanauza kiwanda wanafufunga. Nyerere aliweza kujenga reli ya tazara lakini mpaka leo waliomfuatia wameshindwa kujenga reli nyingine mpya na zilizokuwepo wanaziua

Mkuu wangu,
Sisemi matatizo tuliyonayo yamesababishwa na Nyerere, bali hoja ni kwamba Utawala wa Nyerere haukutuachia msingi mzuri wa kiuchumi kama ambavyo Kenyatta alifanya kwa Kenya. Marais wengi ambao waliingia baada ya Nyerere walilazimika kuanzia from the scratch coz' mambo mengi yalikuwa mahututi!! Historia zinatuambia kwamba, ilifikia hata kupata kipande cha sababu nchi hii ni anasa!! Kunywa chai nako kulikua ni moja ya anasa za mijini! Sasa kama vitu vya kawaida kama hivyo tu ilikuwa shughuli; what abt mambo ya msingi ambayo yangetumika kama injini za kukuza ama kuendeleza uchumi wetu?! Tuwe wakweli, tuachane na siasa za CCM na CHADEMA hapa; by 1980s, kulikuwa na barabara ngapi (in km) nchi hii ambazo zilikuwa zinapitika misimu yote?! Mimi ni mtu wa Lindi; umbali wa Lindi hadi Dar es salaam ni nusu tu ya ule umbali wa Arusha-Dar es salaam! Lakini unaambiwa watu walikuwa wanatumia zaidi ya wiki mbili kusafiri umbali usiofika hata kilometa 500!! Huo ni mfano mmoja tu wa miundombinu ambayo tulikuwa nayo!! Sasa wakati hali hiyo tumedumu nayo, Kenya walishaachana nayo tangu awamu ya Kenyatta!!

Kuhusu viwanda, sikatai......Nyerere's government did a great job katika kuwekeza kwenye viwanda! Hata hivyo, kama nilivyosema hapo, utawala wake ulishindwa kabisa kusimamia viwanda hivi na hivyo kuwa economically not efficient! Vingi ya viwanda hivi vilikuwa mahututi tangu enzi za utawala wake, na hao wengine wamekuja kuvimalizia tu!!

Hilo la reli ya TAZARA lina historia yake na wala sina haja ya kuliongelea hapa. Na kuhusu suala la shilingi yetu kuwa na thamani si jambo la msingi kivile. In economics, kuna kitu kinaitwa DEVALUATION & OVERVALUATION! Devaluation ni kushusha kwa makusudi thamani ya fedha. Hii ni technique kwa ajili ya ku-motivate exportation. Take an example of China and Japan. INgawaje uchumi wa nchi hizi upo juu sana, lakini thamani ya pesa yao ni ndogo! OVERVALUATION, ni hali ya kuipandisha thamani pesa ya nchi husika kuliko thamani yake halisi! Hili linafanyika zaidi ili ku-favor walaji. It's PURELY POLITICAL economic decision making! Na hili la Currency Overvaluation ndilo lilikuwa enzi ya utawala wa Nyerere! Kama shilingi ingeachwa ishindane na market force, basi enzi zile thamani ya shilingi ingekuwa chini sana!
 
Nyerere kikwazo ameshakufa,waliohai wamefanya nini cha maana??au ndio tabia za kiswahili kutafuta mchawi uku tunacheza bao muda wote..

Acha kuropka wewe, kama huelewi si lazima uchangie. Hakuna uchumi wa nchi yoyote ambao hauna chanzo chake. Issue ni kwamba, haya yanayofanyika leo Tanzania wenzetu Wakenya walifanya miaka ya 60. Na kama huyaoni hayo yanayofanyika leo basi wala sina sababu ya kupoteza muda kukueleza coz' itakuwa umekalia politics!
 
Nashauri ubadilishe kidogo swali lako uulize: Hivi kwa nini Kenya wanapewa sifa sana? Hili lingeweza kutuelekeza kwenye hoja za msingi au mambo yanayowafanya wenzetu wajipambanue kimaendeleo tofauti na sisi.
 
Ok kama Kambarage alifanya madudu. Haya tueleze waliofuatia nao wamefanya nini kama sio madudu zaidi ya Kambarage?

Siasa hizi mie siziwezi!
Nakubali kabisa kwamba tangu Nyerere aondoke basi ufisadi umekuwa maradufu lakini kunitaka nitaje hao waliofuata wamefanya nini(from african political point of view, u mean hawajafanya chochote!) ni kutaka kuniangiza kwenye siasa zisizo na tija kwangu!! Hata hivyo, ukweli bado utabaki pale pale, hatua kubwa ilipigwa na Kenya imetokana na msingi wa kiuchumi ambao uliwekwa na Kenyatta; sana sana, yule ambae alimfuatia(Moi) ndo alitaka kuuharibu. Ukweli bado utabaki pale pale, kwamba hata hayo machache yanayofanyika sasa yalitakiwa yawe yameshafanyika miongo kadhaa iliyopita.
 
Hawa viongozi wetu kwa kweli ni mzigo wa misumari tumebebeshwa..Inafika mahali mtu unakuwa not proud to be Tanzanian..Unaona aibu kwa kweli..

Labda nikuuliza hiyo misumali umebebeshwa na nani? Halafu, kuhusu swala la kuwa sijui proud kuwa Mtanzania, usilikuze sana, hata wewe unaweza kufanya mambo mengi kama wewe pia yakakufanya ukawa proud, acahana na mabo ya Tanzania usiongelee kwa ujumla anza na wewe, Je umefanya nini, kukufanya uwe proud?
 
Nyerere kikwazo ameshakufa,waliohai wamefanya nini cha maana??au ndio tabia za kiswahili kutafuta mchawi uku tunacheza bao muda wote..


Umesema vizuri maana hakuna kilema kibaya katika maendeleo ya binadamu be it economiccaly, socially, culturally, religiously or in a nut shell all walks of life kama mtu anaamua kuwa mtumwa wa historia. Kama watu wangekuwa na mawazo na sababu kama za huyo mchangiaji basi leo nchi zinaziojitahidi kama Kenya wasingekuwa pale walipo. Kwa hiyo kama ulivyosema we can't blame our failure to the dead. Sisi tujiulize tumefanya nini. Maendeleo yote duniani ni through basic industries ambazo huyo Kambarage mnamulaumu alijenga vya kutosha kama kile ch zana za kilimo, vya kutengeneza nyuzi za pamaba na kuetengeza nguo, cha matairi 9general tyres0 kilichokuwa kianuza South of the SAHARA. Vyote waliofuatia wakaviua. Sasa utamlaumu Nyerere? Kama vingine vilikuwa havizalishi kwa kiwango je dawa ilikuwa kuviua? Watanzania kwenye mambo nyeti tusipende kutoa maelezo ambayo yako too cheap
 
Labda nikuuliza hiyo misumali umebebeshwa na nani? Halafu, kuhusu swala la kuwa sijui proud kuwa Mtanzania, usilikuze sana, hata wewe unaweza kufanya mambo mengi kama wewe pia yakakufanya ukawa proud, acahana na mabo ya Tanzania usiongelee kwa ujumla anza na wewe, Je umefanya nini, kukufanya uwe proud?
Unajifanya mgeni na nji hii...hujui kuwa kila mwanya wa mtu kujitoa umebana??rushwa hadi kanisani/misikitini......Unadhani ni rahisi kama unavotaka nikuamini??
 
Wewe tatizo lako ni kutafuta mchawi. Nyerere aliweka miundombinu mizuri sana ikiwepo viwanda almost kila mkoa. Tatizo ni ufisadi wenu nyinyi viongozi mkuviua viwanda vyote alivyovianzisha nyerere. Na kutokana na sera zenu mbovu viwanda vingi vimegeuzwa kuwa maghala. Je bado ni tatizo la Nyerere? Leo hii kuanzia awamu za kifisadi za tatu na nne mmeamua kutumia raslimali za nchi vibaya. Tuna raslimali nyingi kuwazidi hata Kenya lakini tangu sera za kibinafshaji zianze nchi haijanufaika na chochote ukiachilia mbali chama cha magamba na viongozi wake. Hatuwezi hata siku moja kuwafikia Wakenya kimaendeleo kama tutaendelea kuwa na utawala wa CCM. CCM imeshakufa kifikira na kwa sasa wanaongoza kwa mazoea tu. Hawana jipya. Mimi nashangaa sana hata sasa kuendelea kupigana vikumbo ili waendelee kututawala wakati hawajatufanyia lolote la maana. Labda wanataka kuendelea kututawala ili waendelee kupora raslimali zetu. Mungu ibariki Tanzania NasDaz
 
Last edited by a moderator:
NasDaz kwa hiyo nyerere ndo aliwaambia muuze madini kwa royalty ya asilimia 3? nyerere ndo amewaambia mfiche matrilion ya shilingi nje wakati watoto wenu wanakaa chini mashuleni? je nyerere anahusika na wizi wa EPA? je nyerere ndo amewaambia muingie mikataba ya gesi bila bunge kuridhia? nimetaja mambo machache tu ambayo kama umakini ungekuwepo, leo barabara zetu zote zingekua na lami
 
Last edited by a moderator:
Siasa hizi mie siziwezi!
Nakubali kabisa kwamba tangu Nyerere aondoke basi ufisadi umekuwa maradufu lakini kunitaka nitaje hao waliofuata wamefanya nini(from african political point of view, u mean hawajafanya chochote!) ni kutaka kuniangiza kwenye siasa zisizo na tija kwangu!! Hata hivyo, ukweli bado utabaki pale pale, hatua kubwa ilipigwa na Kenya imetokana na msingi wa kiuchumi ambao uliwekwa na Kenyatta; sana sana, yule ambae alimfuatia(Moi) ndo alitaka kuuharibu. Ukweli bado utabaki pale pale, kwamba hata hayo machache yanayofanyika sasa yalitakiwa yawe yameshafanyika miongo kadhaa iliyopita.


Mkuu hapo ndipo sababu uliyosimamia kuwa Nyerere hakuweka misingi mizuri unajichanganya na kuwachanganya wanaofatilia mjadala huu. Misingi ya unchumi mzuri ni ipi? Ni kile ambacho kwenye uchumi tunafundishwa economic overheads capital kama Viwanda hasa basic industries? Kama ni hivi Nyerere stands to be an icon on these maana alianzisha. Miundo mbinu ya barabara na reli alijitahidi walau ile tuliyorithi ya Mjerumani iliendelea kuwepo na kuwa tegemeo la usafiri. Na ile ya Tazara unasema isitajwe maana wengine hatujui historia. Sasa sijui unataka credit apewe nani? Najua utatwambia mambo ya bipolar system-Ujamaa na ubeapari kwa kile kinachoitwa vita baridi na kwakuwa msaada ulitoka China basi mtasema ni kwa sababu hiyo. Lakini hii ni kuififisha fikra maana your argument kama utakuwa kwenye mtazamo huu ni kuwa limited in thinking based on Erocentric or Ethnological. Na hii sio sahii maana one school of thought haijawahi kutoa majibu ambayo ni infallible. Vyanzo vya umeme alijitahi kujenga mabwawa mengi ya kuzalisha nishati hiyo mpaka leo tuko kwemye miradi ya kuungaunga. Shukrani kwa miradi ya gesi though very lidicrous sisiwenye mali tunauziwa.Mengine ya sabuni anasa na unga wa njano naona hizo ni political propaganda ambazo sio basic maana wanozishabikia hawatwambii circumstances zilizosababisha yote hayo. Na wale wanaotaka kupata credit kwamtindo wa one swallow makes summer hawatuambii madini, wanyama, na gesi ambavyo leo vinakuwa exploited ni nani alivilea mpka leo hii. Sasa tumeamua kuvuna utajiri huu mbona mikataba inakuwa siri? Mbona hatupigi maendeleo? Halafu do not say Tanzania ya walimfuatia Nyerere ilikuwa to start from scratch. Ni uwongo wa kutetea usichokijua. Viwanda kama TBL, Sigara, General Tyres kwa kutaja vichache unawezaje kusema vilikuwa ni hasara kama sio propaganda? Mnaua reli mnatenegneza vibarabara vyenye viwango duni tena kwa gharama kubwa kuliko miradi kama hiyo nchi za jirani halafu manaruhusu watu binafsi wananunua tracks na kupitisha barabara hazidumu halafu mnasema leo mmepiga maendeleo. Niachi hapa nisije nikapandwa na hasira.The bottoline don't blame our failure to the dead/gosts
 
NasDaz Oh my GOD! una maana gani kuhusu "msingi mzuri wa uchumi?" Viwanda 400? siyo msingi? Siasa iliyoweka mbele maslahi ya maskini yaani Ujamaa na kujitegemea siyo msingi?
Nyerere siyo wa kulaumu nafikiri! wa kulaumu ni watanzania wote hasa viongozi waliofuata!! Ongea vilevile by 1980 Kenya ilikuwaje! Unajua mabadiliko makuu yamefanyika Kenya katika utawala wa Kibaki!? Ninaganga njaa hapa Nairobi ninaona!! Unajua MOI aliimaliza kabisa Kenya?!! Hivyo tatizo siyo Nyerere ila maintaining and conceptualizing his thinking!!
I can agree on one thing: yale mashati yaani wasaidizi wa Nyerere "were dancing to a tune of a song they did not believed in" evidence Azimio la Zanzibar na uuzaji holela wa viwanda na mashirika aliyoacha nyerere! What should be done? tuyajadili hayo zaidi ya kurusha makombora nyuma ya historia: Nyerere, nyerere, nyerere! obselete thinking!
 
Last edited by a moderator:
Unajifanya mgeni na nji hii...hujui kuwa kila mwanya wa mtu kujitoa umebana??rushwa hadi kanisani/misikitini......Unadhani ni rahisi kama unavotaka nikuamini??

unaonekana umekata tamaa sana na maisha ya Tanzania, pole sana, lakini hata kwingineko pia sio rahisi hivyo, hiyo ndio bahati mbaya yenyewe, hivyo hatuna jinsi bali kuendelea kupambana tu, lakini bado naamini ukijituma sana bila kuchoka na kulalamika sana utafanikiwa tu, mimi ni mfano hai na wapo wengi tu kama mimi ambao tumeanzia sifuri 0 mpaka sasa tuna tunauwezo wa kumiliki kitu na kuendesha maisha yetu ndani ya Tanzania hii hii!
 
@Bigaraone Bado nasisitiza, huwezi kuilinganisha Kenya na Tanzania leo hii kwavile Kenya walianza kujenga na kuusimamia uchumi wao miaka kadhaa iliyopita!! Ingawaje ni kweli kwamba Nyerere alijenga viwanda vingi sana lakini ukweli ni kwamba viwanda vingi havikuwa na efficiency na vingi vilikufa enzi za utawala wake!! Politics ilitawala sana hata kwenye uchumi. Kungekuwa na ulanguzi wa sigara endapo kungekuwa na uzalishaji mzuri wa sigara?! Unazungumzia General Tyre; kwa magari gani ambayo Tanzania hii ilikuwa nayo hata usifie kwamba kulikuwa na General Tyre?! Unadai kuzungumzia mahindi ya njano ni political propaganda; ina maana unataka kukataa kwamba watu walikuwa hawaishi kw mahindi ya njano, tena ya msaada, au?! Ni sababu hizo ambazo unataka ku-justfy zilipelekea kula mahindi ya njano? Ina maana unataka kukataa kwamba nchi ilikosa hata vitu vya kawaida kabisa kama vile mafuta na sabuni; na hata viberiti?! Ina maana unataka kukataa kwamba nchi hii watu walikuwa wanapanga foleni kutwa mzima kwa ajili ya kupata sukari robo kilo?!! Yaani unataka kukataa kwamba mtu alikuwa anatumia karibu mwezi mzima kutoka Dar es salaam hadi Lindi; umbali usiofikia hata kilometa 500?! Yaani unataka kuktaa kwamba kwenda kwenye mikoa ya nchi yako ilitakiwa wakati mwingine upitie nchi jirani?! Niambie, wakati hayo yanaendelea nchini kwetu, Kenya ilikuwa kwenye state gani ya maendeleo?!

Unadai kwamba kulikuwa na vyanzo vya kutosha vya umeme!!!! Kulikuwa na vyanzo vya kutosha vya umeme au hakukua na matumizi ya kutosha ya umeme?! Ikiwa mtu kuwa na redio tu ilikuwa ni serious issue; sasa ingeshindikana vipi kwa vyanzo vilivyokuwepo kutosheleza?! Wangapi walikuwa na redio zinazotumia umeme? Wangapi walikuwa na Televesheni? wangapi walikuwa na majiko ya umeme?! Wangapi walikuwa na pasi za umeme?! Wangapi walikuwa na mashine za kufulia zinazotumia umeme?! BUT all in all, wangapi nyumba zao zilikuwa zimeunganishwa na umeme?! Kulikuwa na shughuli gani za kimaendeleo nchi hii ambazo zilikuwa zinatuma sana umeme?! Kwahiyo ni kichekesho kusema kulikuwa na umeme wa kutosha wakai ukweli ni kwamba hakukua na shughuli zinazotumia umeme!! Kulikuwa na Kiwanda cha kutengeneza viatu cha Bora; lakini mamilioni ya Watanzania walikuwa wanatembea pekupeku, achilia mbali mavazi duni!

Leo tunavyozungumzia uchumi wa Ulaya, tunazungumzia mapinduzi ambayo yalitokea Ulaya zaidi ya miaka 200 iliyopita! Leo tunapozungumzia uchumi wa China; tunazungumzia misingi imara ambayo iliwekwa miaka kadhaa iliyopita! The same apply to many other countries!! Wakati leo Kenya ikifikiria kujenga Flyovers; Tanzania lazima tuzungumzie ujenzi wa barabara kwani barabara hazikuwepo ingawaje unashangaza kwa kiasi cha kutisha kusema eti Utawala wa Nyerere ulijenga barabara!!

Na kama mtu utataka kuwa mkweli, endapo tutataka kuangalia economic gap kati ya Tanzania na Kenya; kwa kuangalia wakati wa Waasisi wa Matataifa haya mawili(Nyerere na Kenyatta) na baada ya wakati wao; ukweli ni kwamba economic gap kati ya Kenya na Tanzania hivi sasa dogo ukilinganisha miaka ya 80!!
By the way; nyie watu vipi?! Hamna hoja, au?! Mbona issue ya Nyerere mnachukulia too personal?! Wakati mara nyingi nimekuwa nikisisitza UTAWALA WA NYERERE, akina nyie mnang'ang'ana na NYERERE!!! Ndo tatizo la kuwa na hisia fulani in advance dhidi ya jambo fulani!! Narudia, Utawala wa Nyerere ulijenga uchumi na kuuharibu vile vile to the point that, tawala zilizofuata zililazimika kuanza mwanzo!
 
unaonekana umekata tamaa sana na maisha ya Tanzania, pole sana, lakini hata kwingineko pia sio rahisi hivyo, hiyo ndio bahati mbaya yenyewe, hivyo hatuna jinsi bali kuendelea kupambana tu, lakini bado naamini ukijituma sana bila kuchoka na kulalamika sana utafanikiwa tu, mimi ni mfano hai na wapo wengi tu kama mimi ambao tumeanzia sifuri 0 mpaka sasa tuna tunauwezo wa kumiliki kitu na kuendesha maisha yetu ndani ya Tanzania hii hii!

Hongera...Lakn nimekutolea mfano wa wasukuma guta wanaopiga mzigo 24/7 na bado wanakwamishwa na mfumo mbovu wa kimasikini tulionao hapa TZ...
Kukatishwa tamaa na hali iliyopo hiyo ni Given kwa sababu ndio hali halisi na siwezi hata siku moja nikachekelea au kufurahia mambo jinsi yanavyoenda...
Majority ya watanzania wanakuwa duni kila siku wakati wachache wananufaika..Kodi tunazotoa zinaishia kwa wajanja wachache na kazi haionekani..Lazima tuwasifie Kenya kwa sababu at least vitu vinafanyika vinaonekana...
 
Chondechonde msinitie uchungu na kunipa hasira mimi bure. Sitaki kuangalia sifa za hawa jamaa wakenya. Nia yao ni kutaka kututambia sisi. Si wangetusubiri twende pamoja. Wakenya si watu wazuri ni wapenda sifa sana wanameniuzi sana. Yaani wanataka kutuambia hata kama tanzania ina madini ya kila aina na wanachimba na wao kenya hawana na hata ardhi yao ni nusu jangwa eti bado wako mbele yetu na hatuwawezi.
 
Back
Top Bottom