Kwanini Kenya wanapenda sifa sana?

Kwanini Kenya wanapenda sifa sana?

kwa nini wasiwe na mkonga mmoja kama wa kwetu?

kuwa na mikonga 5 maana yake nini ?

sisi tuko wengi zaidi lakini nashangaa hatuna spidi kama hawa jamaa

Kenya plans to land 5th undersea cable | balancingact-africa.com
NBO
4-jomo-kenyatta.jpg


DAR
DarEsSalaam-Airport.jpg
kenya_airways.jpeg
kenya-map1.gif


ATCL%20acc(3).jpg
air_tanzania_de-haviland_crash.jpg
Air-Tanzania-Flight-Route-Map.jpg



Nairobi_Skyline_650.jpg
560px-Dar_es_Salaam_before_dusk.jpg



systemmap_lrg.png
railways.jpg
_64118728_insidetrain.jpg




Hotel_Baobab_Inn-Dar_Es_Salaam.gif


trc-dar-es-salaam-train-10.jpg
trc-dar-es-salaam-train-6.jpg
VICTOR-WANYAMA-CELTIC.jpg



Rainford-Kalaba-of-TP-Mazembe~5.jpg

Kenyan-shillings.jpg
tanzania2.jpg
 
Kenya wako mbele sana na mambo mengi wametuacha nafikiri ndio maana tunawaona kama wanapenda sifa sana.......
 
Huo ni msimamo na mizingi mizuri ya kujenga uchumi iliyoyoachwa na Kenyatta na marehemu TOM Mboya. Kenya ikimsaidia mkimbizi kupata uhuru basi hiyo nchi lazima itaingiza karibia bidhaa zote za viwanda zitokazo kenya au made in kenya. Ona Sudani ya kusini na sasa ngoja wasomali wajitawale vizuri utaona kila kitu made in kenya.

Sisi tukiwasaidia wakimbizi kupta uhuru, lazima hiyo nchi eitha itafuata ukomunisti au kujiunga na umoja usio fungamana na upande wowote. hapo tumemaliza!!!Huo msimamo wa kenya unasaidia sana kupunguza ukosefu wa ajira na viwanda kuzidi kupanuka.

Msimao wa sisi ni pale raisi wetu anapoambiwa asante mzee!
 
Pesa zile tulizokuwa tunapata kutoka kwa serikali ya sweeden ili kutuletea maendeleo, kama zingetumika kwa ajiri ya maendeleo. basi kenya tungekuwa nao sambamba au kuwapita.

Lakini hizo pesa kutoka sweeden zilitumika vibaya sana katika kuimalisha chama, kusomesha makada, kughalimia mikutano kama ile ya kizota, semina za wajumbe wa NEC na kujenga Chimwaga kwa ajiri ya kuwanoa wanasiasa tuu!

Kweli kabisaa, kipindi cha Chama chashika hatamu kilikuwa kibaya sana kuliko hata madhara ya kutawaliwa na mkoloni.
 
Mwanangu Sam Seborn acha wivu. Kwani hao Kenya wametuzuia kuwa na mikonga mingi au hata zaidi yao? Hapa tatizo si Kenya bali utawala wa kifisi na kifisadi unaokutawala na kukula wewe. Badala ya kuwapongeza unawaponda! Kweli kuna watu wana mawazo ya ajabu!
 
Mwanangu Sherrif Alpio umeua. Umenifurahisha kwani comparison yako ni tekenyeshi na elimishi so to speak. I love it.
 
Tuache unafiki, tusijifanye hatufahamu chanzo cha Tanzania kuwa hapa ilipo hata baada ya miaka 50 ya Uhuru! Chanzo cha haya yote ni utawala wa Nyerere ingawaje wapo wasiotaka ukweli huu usemwe na kwamba yeyote atakayesema basi mtu huyo ana chuki na Nyerere!!! Mbaya zaidi, wapo wengine ambao wanafikia kiwango cha juu kabisa cha kushindwa kuficha upumbavu wao kwa kudai eti "Nyerere anachukiwa kwavile ni Mkristo!" RABISH!

Kiuhalisia kabisa, hivi sasa Kenya wapo kwenye second phase ya maendeleo yao. First phase, walishaifanya soon after uhuru wa nchi yao. Wakati wenzetu walianza mapema baada ya Uhuru, Tanzania ikatumia kipindi hicho katika kujishughulisha na ya wenzetu kwa kile tulichoita Kuhakikisha Ukombozi wa Afrika!!

Hata kama hilo nalo si jambo la kubeza, lakini tulitumia raslimali nyingi mno katika suala hilo. Mbaya zaidi, suala la Ukombozi Kusini mwa Afrika tulilisimamia vizuri zaidi kuliko tulivyoweza kuyasimamia mambo yetu wenyewe! Kwani, ingawaje utawala wa Nyerere ulijitahidi kufanya uwekezaji hapa nchini, lakini bado utawala huo ulishindwa kabisa kusimamia yale iliyoyaanzisha!!

Utawala wa Nyerere ulikuwa very efficiency katika kusimamia suala la ukombozi lakini ulikuwa very poor katika kusimamia mambo yake yenyewe! Matokeo yake, nchi ikageuka kuwa omba omba wa aibu, yaani hadi kufikia kuomba omba chakula na kuishia kuletewa hadi mahindi ya njano yanayosemekana yalikuwa ni chakula cha mifugo huko yalikotoka!

Wakati sie tukiitumia first phase kwa staili hiyo, wenzetu Kenya wakajikita kujenga uchumi wao! Wakatumia every available opportunity (including human resources, entrepreneurs) katika kujenga uchumi wao!! Wakajenga mashule, vyuo, viwanja vya ndege, barabara and almost every possible and necessary infrastructure. Pamoja na ugonjwa wa ufisadi uliopo in almost every African Country, lakini bado Kenya waliweza kuyasimamia waliyoyaanzisha; jambo ambalo sie lilitushinda!

Baada ya Nyerere kuondoka madarakani 1985, ndipo Tanzania ikaanza kufanya kile ambacho ilitakiwa kifanywe 20 years back!! And in fact, real move ikaanza baada ya Mkapa kuingia madarakani in 1995; huku ikiwa imeshapita zaidi ya miaka 30 ya uhuru! Kila ambacho Mkapa alijaribu kukifanya, tayari Wakenya walikuwa wameshakifanya more than 20 years back!!

Watu leo hii wanajaribu kudhihaki Treni ya Mwakyembe kwavile tu Kenya wamezindua Treni ya kisasa zaidi! So what did you expect?! Haya yanayofanywa na Mwakeymbe leo hii yalikuwa yawe yamefanyika more than 20 years back!

Ingekuwa ni kichekesho leo hii kufikiria kuwa na treni za kisasa kabisa wakati hata barabara za kupita magari ya kawaida hamna!! Itakuwa ni kichekesho kuwa na Super Highway wakati hata ordinary roads ambazo zilitakiwa kujengwa zaidi ya miaka 30 iliyopita bado hamna!

So, tu cut story short, haya yaliyopo sasa ni matunda ya sera za Nyerere! Wakati Kenya ipo kwenye second phase, or innovation phase, sie ndo kwanza tunaanza! Hata hivyo, am very sure kwamba, sooner or later tuna kila sababu ya kuiacha Kenya.
 
NasDaz Nyerere kikwazo ameshakufa, waliohai wamefanya nini cha maana?? au ndio tabia za kiswahili kutafuta mchawi uku tunacheza bao muda wote..
 
Last edited by a moderator:
Hawa viongozi wetu kwa kweli ni mzigo wa misumari tumebebeshwa..Inafika mahali mtu unakuwa not proud to be Tanzanian..Unaona aibu kwa kweli..
 
Back
Top Bottom