Kwanini idadi kubwa ya wanawake wasomi hawaolewi?

Kwa hiyo hao wanaume watawajua wanawake gani? Wake za watu au?
Machangu Kona baa na kwa wahaya
Kuna mdau aliwahi leta uzi wa wanaume kutafuta experience ya ngono kwa makahaba,then umri ukienda ndo wanafanya maamuzi kuoa
Inatia kinyaa binti kajitunza huko ni bikra halafu anakuja olewa na mteja wa kudumu wa makahaba agrrrrhhhh
 
Wanawake waliosoma soma na wenye kazi nzuri huwa ni "much know" sana. Hilo ndio linalowaponza kutoolewa. Hujifanya kutaka haki sawa 50/50 ndani ya nyumba.
 
Wanawake waliosoma soma na wenye kazi nzuri huwa ni "much know" sana. Hilo ndio linalowaponza kutoolewa. Hujifanya kutaka haki sawa 50/50 ndani ya nyumba.
Shaur yao wasipo jirekebisha na kurudi kwenye msingi aliouweke muumba wataishia kutumika kama viti vya kukodishwa kwenye masherehe * sherehe & harusi zikiisha wanarudi stoo kupigwa vumbi .
GWALA KWAO PIA !
 
Well said.
 
Hawa viumbe ni shida tupu!
 
Mkuu, bila shaka mnaposema mwanamke anavyozidi kuelimika ndivyo anavyozidi kuwa mjinga mnamaanisha kwamba ndiyo anazidi kufunguka akili kuhusu unyanyasaji wa mwanaume kitu ambacho ninyi hamtaki mwanamke awe aware nacho ndiyo maana mnaona kama kuelimika kwao ni tatizo.

Imagine mwanaume anataka akichepuka mke wake asimuulize chochote bali avumilie tu kitu ambacho hata mwanaume hawezi kukifanya endapo mke wake akichepuka, mwanaume anataka akichelewa kurudi nyumbani mke wake asimuulize chochote avumilie tu kitu ambacho hata mwanaume hawezi kukifanya endapo mke wake akichelewa kurudi nyumbani.

Kuna wanaume wengi tu huwa nawasikia wanasema eti "kuoa mwanamke asiye na elimu raha sana yaani unamdanganya tu kwamba unasafiri unaenda kufanya (anataja neno lolote la kiingereza hapa ambalo anajua mke wake hatalielewa) halafu mke anakubali tu kumbe unaenda kwa mchepuko unashinda naye wiki nzima", sasa hebu ona tu ni jinsi gani huyo mwanaume anavyojisifia upumbavu.

Tunajua wanaume wengi wanapenda kuoa wanawake wasio na elimu sababu wanawake wa aina hiyo hawana uwezo wa kuhoji chochote hata kama ni haki yao maana wanachojua wao ni kwamba mwanaume ni mungu akikosea hatakiwi kuambiwa chochote anatakiwa kuchekewa na kuachwa afanye anachotaka hata kama anachofanya ni kosa, lakini mwanamke akikosea anatakiwa apigwe au atalikiwe.
 
Swala siyo kushindana ila tuambiane ukweli kwanini wanaume mjihalalishie makosa??

Halafu sijui kwanini mnapenda kutumia hiyo kama sababu yaani mfano eti mwanaume kuchepuka ni sawa na mwanamke hatakiwi kusema chochote eti kwa sababu tu mwanamke hatakiwi kushindana na mwanaume??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…