Kwanini hatupendi kuwaomba ushauri watu masikini?

Kwanini hatupendi kuwaomba ushauri watu masikini?

Okay.....sijajibu mada bali maswali yako.

Maskini akikupa ushauri anatofauti gani na Inspiration Speaker ambaye anakupa mbinu ambazo yeye hazijamsaidia?
Maskini anapotoa ushauri, anashiriki hekima inayotokana na majaribu ya maisha halisi, sio tu nadharia.

Unadhani ni kweli mtu anayeweza kutoa ushauri bila kupitia majaribu ya dhati ya changamoto anaweza kuelewa kwa kina matatizo ya maskini?
 
Ila kwa waganga wa kienyeji mnaenda

Unakuta kijana kaendelea kimaisha ila wazazi wake ni masikini, lakini hawaulizi ushauri bali ataenda kwa mganga choka mbaya
Najaribu kufikiria uhusiano wa masikini na mganga wa kienyeji, je ni lazima mganga wa kienyeji awe masikini?
 
Maskini ni kama Inspiration Speaker anashauri vitu ambavyo yeye mwenyewe hafanyi.

Au mganga anayekupa utajiri wakati Watoto wake ni maskini wa Kutupwa.
Si kila ushauri huleta faida, Maskini akikushauri hutapenda na hata ukifanikiwa utanyuti kudhani ni fedheha kumshukuru kwa ushauri wake ila ukiangukia pua ushauri wa Tajiri utaugulia maumivu kimya kimya kuhofia akikusikia atakufyekelea mbali 🤣

Ubinadamu ni kazi/The humanity is work
 
Katika ukuaji wangu huu sijawahi kuona mtu yeyote yule akienda kuomba ushauri kwa maiskini.

Sababu kuu itakuwa ni nini?​
  • Tunawadharau,​
  • Hawana mawazo,​
  • Hawana dira,​
  • Ubongo wao haufanyi kazi au​
  • Sababu inaweza kuwa ipi?​
Labda wanaogopa tusije tukawaibia Mali zao
 
Kwenye vikao vya familia vijijni, wengine wanapark ma v8 na wengine wanapark majembe ya mkono ili kikao kikiisha tu wawahi shambani. Sasa hao watakushauri wakuletee mkungu wa ndizi na mahindi ya kuchoma wakati wewe unaweza mamilioni. Ndege wenye manyoya yasiyofanana hawaruki pamoja.
 
Back
Top Bottom