Bongo Movie's si ilikufa na Kanumba?.
Baadhi ya sababu;..
Ngono; Hii ni sababu mama ya kutokutizama Bongo Movies. Rushwa ya ngono imekuwa sababu kuu ya mtu kuingia kwenye Tasnia ya Filamu Nchini. Yaani bila umbo, makalio, nyonyo za kuamsha hisia, sura nzuri huigizi. Hakuna kutizama vigezo vingine. Sijui kipaji, uwezo mzuri kiakili (Up-stairs medula), Elimu nzuri na orodha inaendele... Ukiwa na hivi vigezo unaonekana mshamba kweli.
Bonde la Ufa vichwani; Pia ni sababu ya kutotizama Filamu za hapa nyumbani. Waigizaji wengi, waongozaji nk ni weupe mno vichwani. Ubunifu hakuna, yaani ni kama vile mtu kushindwa kuuza Ubuyu na kuona Bongo movie ndio mpango mzima. Huwezi kufanikiwa kama kichwani haupo vizuri. Ni kanuni ya Dunia.
Kutumika kisiasa/ Ki-soka; Ukishakubali kutumika, basi ni lazima ukubali kudharaulika. Bongo movies wengi wanatumika vibaya na wanasiasa. Kugawa mashabiki ni kosa kubwa mno kwa muigizaji. Hifadhi mhemko wako. Kwani kuna ulazima wa Kujionesha kuwa U-CCM, CHADEMA, ACT-Simba, Yanga, Azam na kadhalika?. Ukimgawa shabiki basi tegemea kula mabua.
Madawa ya kulevya/drug's; Madawa ya kulevya ni hatari mno kwa Maisha ya msanii. Kama una uwezo mdogo kimapato basi tegemea kuwa kile kidogo utakachokipata utakielekeza kwenye madawa na mwishowe kuishia kuporomoka ki-tasnia, kiafya na mengine mengi. Bongo Movies wengi ni wabwia Unga. Ukibwia unga, mashabiki lazima wakupike.
Hizi ni baadhi tu ya sababu. Unaweza kuongeza mpaka zifike Mia.