Kwanini hamuangalii Bongo Movie?!

Kwanini hamuangalii Bongo Movie?!

Bongo Movie's si ilikufa na Kanumba?.

Baadhi ya sababu;..

Ngono; Hii ni sababu mama ya kutokutizama Bongo Movies. Rushwa ya ngono imekuwa sababu kuu ya mtu kuingia kwenye Tasnia ya Filamu Nchini. Yaani bila umbo, makalio, nyonyo za kuamsha hisia, sura nzuri huigizi. Hakuna kutizama vigezo vingine. Sijui kipaji, uwezo mzuri kiakili (Up-stairs medula), Elimu nzuri na orodha inaendele... Ukiwa na hivi vigezo unaonekana mshamba kweli.

Bonde la Ufa vichwani; Pia ni sababu ya kutotizama Filamu za hapa nyumbani. Waigizaji wengi, waongozaji nk ni weupe mno vichwani. Ubunifu hakuna, yaani ni kama vile mtu kushindwa kuuza Ubuyu na kuona Bongo movie ndio mpango mzima. Huwezi kufanikiwa kama kichwani haupo vizuri. Ni kanuni ya Dunia.

Kutumika kisiasa/ Ki-soka; Ukishakubali kutumika, basi ni lazima ukubali kudharaulika. Bongo movies wengi wanatumika vibaya na wanasiasa. Kugawa mashabiki ni kosa kubwa mno kwa muigizaji. Hifadhi mhemko wako. Kwani kuna ulazima wa Kujionesha kuwa U-CCM, CHADEMA, ACT-Simba, Yanga, Azam na kadhalika?. Ukimgawa shabiki basi tegemea kula mabua.

Madawa ya kulevya/drug's; Madawa ya kulevya ni hatari mno kwa Maisha ya msanii. Kama una uwezo mdogo kimapato basi tegemea kuwa kile kidogo utakachokipata utakielekeza kwenye madawa na mwishowe kuishia kuporomoka ki-tasnia, kiafya na mengine mengi. Bongo Movies wengi ni wabwia Unga. Ukibwia unga, mashabiki lazima wakupike.

Hizi ni baadhi tu ya sababu. Unaweza kuongeza mpaka zifike Mia.
doh bonge la thread/povu
asante
sa unaishaurije tasnia ya movie tanzania?
 
zina changamoto nyingi bongo movie kama sio story nzuri basi waigizaji sio wazuri. Tatizo watu hawagawani kazi huwezi wewe ukaandaa story harafu wewe mwenyewe ukawa final editor ....lets say wewe ni fundi nguo ukishona next person aseme umeshona vizuri na sio wewe useme nimeshona vizuri.....ideally kazi ya kutengeneza movie ni kazi ya watu wengi sana tena sana na na ndio maana wenzetu mbele wanaandaa movie kwa miaka kadhaa
hilo nalo neno
 
=story nyingi visa ni vile vile pia mikasa (like mapenzi sijui fumanizi ).

=creativity zero.

tunajua movie ni act, lakini hawawezi kufanya hiyo act iendane na uhalisia.. mfano
-mtu ameamka asbh usoni make up, kavaa hereni
-jambazi lazima avae koti refu jeus na ni lazima awe kauzu
-mlinzi wa getini lazima dishi liwe linacheza(lofa fulani hivi)
-jambazi wanaenda kuvamia sehem wanavua viatu ndio waingie ndani ? .

=haka kamchezo ka part one na two kanakera, alafu ni uzamani

=matangazo almost dakk karibia 20 mwanzoni mwa movie(japo sio zote).

kwa kifupi zina mapungufu mengi sana, licha ya kuiga unaijeria lakini bado. hizi picha niliacha kuangalia kitambo sana, kabla hata ya king wao kanumba hajafariki. huwa sijui chochote khs bongo movie kwa sasa.
ahahahahaha nimecheka mpaka mume kaamka!
 
Story zao idea ni ile ile,yaani mtu unatazama muvi mpya hujawahi kabisa kuiona lakini unajua mwisho wake itakavyokua.
Muvi za mapenzi idea zao ni kwamba mwanzon wapenz walipendana,akaingia kidudu mtu kuvuruga(hapa sasa unakuta rafiki alifanya njama akamuiba bwana wa mwenzie,au ndugu wa mume hawamtaki mke)basi story itaenda na manyanyaso na mwisho watagundua ukweli na kuishi kwa furaha

Kingine unakuta muvi ni ya dk 180,lakini dk 30 muigizaji atazitumia kuchagua vitu supermarket au kuendesha gari barabaran,dk 45 waigizaji watakua club watacheza dk 45 ztaisha...sasa unakuta mtu unaangalia mpaka muvi yenyewe inakukinai sasa...
Wangejitahidi kuongeza ubunifu zaidi ili kulirudisha soko la bongo movie kwa watz
 
Story zao idea ni ile ile,yaani mtu unatazama muvi mpya hujawahi kabisa kuiona lakini unajua mwisho wake itakavyokua.
Muvi za mapenzi idea zao ni kwamba mwanzon wapenz walipendana,akaingia kidudu mtu kuvuruga(hapa sasa unakuta rafiki alifanya njama akamuiba bwana wa mwenzie,au ndugu wa mume hawamtaki mke)basi story itaenda na manyanyaso na mwisho watagundua ukweli na kuishi kwa furaha

Kingine unakuta muvi ni ya dk 180,lakini dk 30 muigizaji atazitumia kuchagua vitu supermarket au kuendesha gari barabaran,dk 45 waigizaji watakua club watacheza dk 45 ztaisha...sasa unakuta mtu unaangalia mpaka muvi yenyewe inakukinai sasa...
Wangejitahidi kuongeza ubunifu zaidi ili kulirudisha soko la bongo movie kwa watz
doh masikini!
 
Mimi nilikua mpenzi wa kuangalia bongo movie mpaka DVD zao nilinunua sana . Lakini sasa nimeacha baada ya kuona movie moja bibie kaudhiwa na mpenzi wake akaamua kujiua . Alikwenda moja kwa moja dukani akanunua sumu ya panya , baada ya kutoa fedha na kupewa sumu hiyo , akasubiri chenchi !
Hahahahaha
 
bongomuvi noma sana, scene inaonyesha ni usiku mtu na mpenziwe wapo chumbani kitandani......halafu kwa nje unasikia sauti ya mtu akitangaza kuuza mboga mboga... "nauza mchicha".

hivi ni kweli kwa mazingira ya mijini, kuna mtu anatembeza mboga mboga usiku?.

pumbavu kabisa hawa...acha niendelee kuwa mtumwa wa kutazama movie za hollywood.
 
bongomuvi noma sana, scene inaonyesha ni usiku mtu na mpenziwe wapo chumbani kitandani......halafu kwa nje unasikia sauti ya mtu akitangaza kuuza mboga mboga... "nauza mchicha".

hivi ni kweli kwa mazingira ya mijini, kuna mtu anatembeza mboga mboga usiku?.

pumbavu kabisa hawa...acha niendelee kuwa mtumwa wa kutazama movie za hollywood.
Hahahahahah nimecheka jamani Mpaka mume kaamka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom