Kwanini DSTV ni ghali sana?

Kwanini DSTV ni ghali sana?

DSTV ni level nyingine kabisa huwezi fananisha na vinga'muzi vingine aisee. Mfano Ukiwa na PVR EXPLORA aisee mkuu utajua nini nakwambia japo ndio hivyo kununua hiyo decoder na kufugiwa ni 1,000,0000 tsh na malipo ya mwezi kwa premium ni 159,000 tsh but uta enjoy sana na features zilizopo humo.

Explora haifiki millioni, tumefunga kwa mzee juzi 720,000 Total, dish, explora na installation.
 
hivi hawa jamaa wa dstv kwanini bei zao ziko juu sana...ni kodi wanayolipa au nini ? Kama ni kodi wale GTV walikuwa hawalipi kodi ? Mimi sio mpenzi wa mpira na sisemi hivi kwa sababu nimeshindwa kulipia dstv.. basi tu nimekuwa nikijiuliza kwa nini hawa ghali sana..na wanaenda na dola kila siku wanaangalia rate ya dola.. nawaonea huruma wapenzi wa mpira wanavyoteswa na hawa dstv..kila chenye mwanzo kina mwisho ..itafikia tu siku watatafuta wateja na wasiwapate kama ilivyo mabenki sasa na mpesa ,tigopesa...yaani dstv ni kampuni kubwa sio tu tz africa nzima...nadhani hata wakifanya elfu 50,000 tshs kwa kila mteja na bado itawalipa..lakini bei zao za kubagua wasionacho...
Bei zipo juu kwa kuwa raw materials zao ni ghali pia. Kupata haki ya kuonyesha La liga,EPL,Sirie A etc ni gharama kubwa sana,so ili wajiendeshe sufficiently ni lazima watoze gharama za juu,
 
Explora haifiki millioni, tumefunga kwa mzee juzi 720,000 Total, dish, explora na installation.

Aliyetoa milioni alipitia kwa dalali. Dar wajinga na wavivu wa kufikiri ni wengi.
 
Bei zipo juu kwa kuwa raw materials zao ni ghali pia. Kupata haki ya kuonyesha La liga,EPL,Sirie A etc ni gharama kubwa sana,so ili wajiendeshe sufficiently ni lazima watoze gharama za juu,

Mbona nchi zingine za africa gharama zipo chini ? Au tz shamba la bibi ?
 
Siyo kweli,niliwahi kuangalizia mpira Nairobi kwa rafiki yangu,bei ni zile zile. Kumbuka pia thamani ya pesa inatofautiana kwa nchi tofauti,

Usiwatetee...bei zao ziko juu...na haziko fixed kila mda zinapanda.. ghali sana kwa mtanzania ambaye si FISADI
 
Usiwatetee...bei zao ziko juu...na haziko fixed kila mda zinapanda.. ghali sana kwa mtanzania ambaye si FISADI

Angalia table iliyobandikwa hapo juu, TZ, Kenya na Zambia bei ni ile ile na hata Nigeria umepungua kama dola 10, nchi za Southern Africa ndo kuna angalau, hii inaweza kutokana na mambo mengi ikiwemo gharama za kurusha kama South Africa na TZ wanatumia Satelite tofauti angani, kodi etc.

Anyway ni soko huria na DSTV sio essential service, wanaodai serikali iingilie hawajui biashara.
 
Bei zipo juu kwa kuwa raw materials zao ni ghali pia. Kupata haki ya kuonyesha La liga,EPL,Sirie A etc ni gharama kubwa sana,so ili wajiendeshe sufficiently ni lazima watoze gharama za juu,

Hiyo Mkuu ni nadharia, nchi Zingine hata south Africa ni rahisi zaidi kuliko Tanzania. Ingia kwenye mtandao utaoni. DSTV wanatuibia watanzania; wajinga ndio waliwao
 
kwa anayejua nikweli DSTV wamepunguza gharama yavifurushi vyao hadi chachini kabisa kufikia elfu50?kwamwenyekujua Msaada Tafadhali.
 
Nunua startimes decoder kwa shs.4,000/= pamoja na kifurushi kikiwa kimeungwa tayari.
 
Kwa dstv sahau kabisa kushuka gharama. Na hivi rate za shilingi zinavyozidi kuporomoka very soon premium package itakuwa laki 3.
 
kwa anayejua nikweli DSTV wamepunguza gharama yavifurushi vyao hadi chachini kabisa kufikia elfu50?kwamwenyekujua Msaada Tafadhali.

Gharama za vifurushi au za kisambuzi chao??
Maana kama niko sahihi wana kifurushi cha 17,000Tshs!
 
Nahisi mleta mada angeelimishwa nini maana ya dstv,,bei ya kingamuzi,na malipo yake kwa mwezi,kwanini nasemahivi aliposema vifurushi vyao vimeshuka mpaka 50,000 ambapo kuna hadi cha 17,000 mwaka sasaa,,akielekezwa atarudi naswali vizuri else tukonjiani kukuletea cha 9000 mwakan
 
Hawa wametukamata kwenye EPL. Bila hiyo hata elfu ishirini wasingepata watu.
 
Back
Top Bottom