mtoto wa mchungaji
JF-Expert Member
- Oct 24, 2020
- 279
- 480
Nawapongeza sana Mkonda na Dr. Bashiru kwa kuwa waungwana hasa wakinata na ile methali isemeyo mtu mzima akivuliwa nguo uchutama. Wahishimiwa hawa waungwana na watu ambao walifanya kazikubwa sana wanaweza kuwa vijana wa mfano wa kuigwa na vijana wengine kutokana na upepo ambao ulikuwa ukisuma tanga zao kukata ghafla kutokana na kuwa dunia inajizungusha na kuzunguka jua, wamekuwa na hikima na kutambua kuwa hizo ni nguvu za asili.
Hari hii imekuwa tofauti kabisa kwa ndugu yangu na jamaa yangu huyo kwani baada tu ya upepo kukata na jaazi kusimama yeye amevua shati na kuanza kupepea tanga kwa mikono yake. Tumemshuhudia akituma kripu za kucheza shoo na kujichekesha kanakwamba anabadilisha gia angani kuwa mcheza shoo na kina Dimond na wenzake.
Licha ya kuwa tayari anaitwa katika kamati mbali mbali za maadili na nidhamu kujitetea, tayari anaandaa makongamano kanakwamba upepo hajui kama ulishakata.
Huyu jamaa anaubunge wa kuteuliwa ambao ni raisi kutenguliwa, ingependeza kama na yeye angechuchumaa chini kidogo atafakari. Hata hivyo mimi kama mtoto wa mchungaji narudisha lawama zote kwa viongozi waandamizi wa Chama Cha Mapinduzi kwa kumwacha kijana wao bila kunfanyia kanseli, na kibaya zaidi hata kuniita mimi mtumishani wa Mungu kwenda kumkanseli.
Kijana huyo ambaye aliwai kufanya mambo makubwa wakati upepo ulipokuwa ukivuma nadhani ifike wakati tutambue mchango wake hasa kwa kipindi hiki kigumu cha upepo kukata kwa kumfanyia tu kanseli na si kumpeleka katika vikao vya maadili na kumjadili wakati tatizo mnalijua.
Nachuku fursa hii kuwahasa vijana na wazee pia kuwa uongozi ni upepo tu au pepo zinakataga, na wakati mwingine zinakata upo katikati ya bahari na hujui kuogelea utafanyaje. Vyeo ni dhamana na pia nawahasa kuto kutuiga sisi watu wa kanisa kwani sisi tumepewa kibari na Mungu kukusanya sadaka mpaka kifo na si watu wa siasa.
Nawasilisha.
Hari hii imekuwa tofauti kabisa kwa ndugu yangu na jamaa yangu huyo kwani baada tu ya upepo kukata na jaazi kusimama yeye amevua shati na kuanza kupepea tanga kwa mikono yake. Tumemshuhudia akituma kripu za kucheza shoo na kujichekesha kanakwamba anabadilisha gia angani kuwa mcheza shoo na kina Dimond na wenzake.
Licha ya kuwa tayari anaitwa katika kamati mbali mbali za maadili na nidhamu kujitetea, tayari anaandaa makongamano kanakwamba upepo hajui kama ulishakata.
Huyu jamaa anaubunge wa kuteuliwa ambao ni raisi kutenguliwa, ingependeza kama na yeye angechuchumaa chini kidogo atafakari. Hata hivyo mimi kama mtoto wa mchungaji narudisha lawama zote kwa viongozi waandamizi wa Chama Cha Mapinduzi kwa kumwacha kijana wao bila kunfanyia kanseli, na kibaya zaidi hata kuniita mimi mtumishani wa Mungu kwenda kumkanseli.
Kijana huyo ambaye aliwai kufanya mambo makubwa wakati upepo ulipokuwa ukivuma nadhani ifike wakati tutambue mchango wake hasa kwa kipindi hiki kigumu cha upepo kukata kwa kumfanyia tu kanseli na si kumpeleka katika vikao vya maadili na kumjadili wakati tatizo mnalijua.
Nachuku fursa hii kuwahasa vijana na wazee pia kuwa uongozi ni upepo tu au pepo zinakataga, na wakati mwingine zinakata upo katikati ya bahari na hujui kuogelea utafanyaje. Vyeo ni dhamana na pia nawahasa kuto kutuiga sisi watu wa kanisa kwani sisi tumepewa kibari na Mungu kukusanya sadaka mpaka kifo na si watu wa siasa.
Nawasilisha.