Kwanini CHADEMA wanauchukia Mwenge wa Uhuru?

Kwanini CHADEMA wanauchukia Mwenge wa Uhuru?

Hebu tuwaulize na ninyi CCM (tena baadhi tu wapuuzi na wajinga wa mpaka kisogoni!) kwa nini mmeng,ang'ania hii kitu mnaouita "MWENGE WA UHURU?". Si ni kwa sababu mnachangisha fedha kwa lazima kwa wananchi kwa ajili ya kujinufaisha? Mfano wa hili uko wazi sana na nakupa picha ya mambo yalivyokuwa takribani mwezi mmoja uliopita jinsi watu walivyopata adha katika maeneo ya huku ninapoishi eti kwa sababu ya mwenge;
  • Kwanza ni MICHANGO YA LAZIMA iliyosimamiwa na wakuu wa wilaya kupitia kwa watendaji wa vijiji na kata na kwa watumishi wakurugenzi waliagiza wakuu wa idara kuchangisha fedha toka kwa watumishi walio chini yao na kwa kwa hiyo;
  • Kila mtumishi alilazimishwa kuchangia Tshs 2,000/=
  • Kila taasisi zililazimishwa kuchangia fedha mfano; Tshs. 10,000/= (shule za msingi), Tshs. 20,000/= (shule za sekondari) nk nk kutegemea na ukubwa wa taasisi
  • Kila mfanyabiashara alilazimishwa kuchangia kati ya Tshs 2,000; 3,000; 5,000 na 10,000 kutemea na ukubwa wa biashara
  • Mwenge huleta usumbufu sana kuliko manufaa na kinyume na malengo unapokuwa unapita katika maeneo ya watu; mfano ni kusimama kwa shughuli nyingi za kiofisi na uzalishaji katika taasisi nyingi za umma kwa sababu wengi wa maafisa hasa katika ngazi ya wilaya hujikuta wako bize kwa shughuli za mwenge na watu kukosa huduma kwa hata wiki nzima bila sababu yoyote ya msingi zaidi ya hii kitu MWENGE WA UHURU iliyopitwa na wakati!!

KWA NINI CHADEMA WANAUPINGA MWENGE WA UHURU?
Kwanza naomba nikusahihishe kwa kukuambia kuwa you are making a big mistake unapokuwa hutaki kufanya mabadiliko ya kifikra, unapokuwa hutaki kubadili mitazamo yako (mindset) katika mambo mbalimbali kwa kudhani kuwa kila kinachopingwa/kosolewa na CHADEMA kinachotokana/asisiwa na serikali ya CCM basi ni kibaya!!.

Aidha si tu CHADEMA wanaopinga hili hata CCM wanaathiriwa sana na sera na mipango ya serikali yao wenyewe.Mfano leo ktk Bunge katika mjadala wa ishu hii ya Mwenge karibu kila Mbunge bila kujali itikadi zao za kisiasa walikuwa wanaonekana wazi kutoridhishwa na majibu ya serikali kuutetea mwenge.Na mmoja wa wabunge wa CCM waliopata nafasi ya kusema kuhusu mwenge ni mbunge Kessy nadhani ni wa huko Nkasi - Mpanda. Huyu bwana ni CCM na alionesha wazi kutoridhishwa na falsafa ya MWENGE WA UHURU kwa sasa kwani dhima nzima iliyokusudiwa imeshapitwa na wakati na badala yake mwenge ni kama vile unaongeza matatizo ambayo ulipaswa kuyatowesha mfano; umaskini, Rushwa na ufisadi,maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa njia ya ngono nk nk

Kwa hiyo basi CHADEMA hawaoni umuhimu wa Mwenge wa Uhuru kwa sasa kwa sababu logic nzima ya Mwenge ilishapotoshwa na CCM na badala yake mwenge umekuwa ukileta adha isiyo kifani kwa wananchi. Na ndiyo kusema kwamba CHADEMA wanaongea yaliyo miyoni mwa wananchi, wanawakilisha mawazo halisi ya wananchi.!!
 
hata mimi na uchukia mwenge na sio mmoja wa CDM. Unaongezea taifa gharama zisizo na sababu
 
Kwahiyo bila mwenge miradi haizinduliwi?
Wewe naona umekurupuka. Kwani umeambiwa mwenge unapeleka fedha za miradi? Mbio za mwenge hutumika kuzindua miradi iliyotekelezwa kupitia vyanzo mbalimbali vya mapato
 
Kwa mda mrefu sasa wabunge wa chadema wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru,
Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge,
Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi,
Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.

Nimepata kitu hapa.Kumbe hospili,madarasa na vingine vinavyojengwa nilidhani vinajengwa na wananchi kumbe vinajengwa na mwenge pia haviwezi kutumika mpaka vizinduliwe na mwenge.Michango inayotolewa na watumishi wa umma pamoja na wananchi kwa ajili ya mwenge ambazo zingitumika kwa ajili ya kuwasomesha watoto wao nilidhani kuwa fedha wanayotoa nifedha yao kumbe ni fedha ya Mwenge.Kumbe nchi zingine ambazo hawakimbizi mwenge ujenzi wa madarasa,Hosptali n.k pamoja na uzinduzi wake haupo.Hivyo nchi hizo hazina maendeleo kabisaa.
 


Mh.Kessy mbunge wa CCM leo amepinga Mwenge huu wa uhuru bungeni kwa kusema unarudisha maendeleo nyuma na kiini cha matumizi mabaya ya pesa.

mytake;
Mnavyozidi kuforce uwepo wa huu mwenge ndo mnazidi kutupa hari ya kuupinga na soon tutaufungia huu mwenge museum.

Mkuu, Kessy ni maoni yake. ila bado hujajibu swali. kwa nini chadema wanachukia Mwenge wa uhuru
 
Kwa mda mrefu sasa wabunge wa Chadema wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru.

Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge, Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi.

Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.

hata mie nauchukia mwenge sioni faida yake zaidi naona hasara tu
 
Mkuu umepinga nini na umekubari nini,sioni kama kuna gharama zozote za kuendesha mwenge ukilinganisha na faida zinazopatikana.

Ni kweli huwezi kuona gharama zake sababu hujawi kuusika katika kuugharamia huo Mwenge. Na wanaopinga si CDM peke ake ni wengi tu hasa wale wanaoishi vijijini ambapo fursa hawana. Kumbuka CCM tuna wanachama takribani mil 5 sasa na wapo baadhi yao hatuungi mkono mwenge huu kutokana na gharama plus kero kwa wananchi na wafanyakazi waliowengi huko mikoani!! Elfu kwa wewe waona sio gharama sababu kwa kukaa nyuma ya keyboard unaipata kule kijijini kunapopita mwenge ni balaa kuipata hiyo!

Matahalani nikiwa chipukizi mwaminifu mwaka wa mwisho shule ya Msingi maeneo ya Tanga (1988) mwenge ulizindua jengo la CCM kata kwa mwembwe nyingi. Nakuambia mleta mada mbaka leo naongea halijaisha na limebakia msingi tu. Na ndivyo miradi mingi inavyokuwa baada ya kuzinduliwa na mwenge. To me the philosopy is outdated..ile nia ya mwenge haipo kinachofanyika ni mazoea tu!!
 
Hebu tuwaulize na ninyi CCM (tena baadhi tu wapuuzi na wajinga wa mpaka kisogoni!) kwa nini mmeng,ang'ania hii kitu mnaouita "MWENGE WA UHURU?". Si ni kwa sababu mnachangisha fedha kwa lazima kwa wananchi kwa ajili ya kujinufaisha? Mfano wa hili uko wazi sana na nakupa picha ya mambo yalivyokuwa takribani mwezi mmoja uliopita jinsi watu walivyopata adha katika maeneo ya huku ninapoishi eti kwa sababu ya mwenge;
  • Kwanza ni MICHANGO YA LAZIMA iliyosimamiwa na wakuu wa wilaya kupitia kwa watendaji wa vijiji na kata na kwa watumishi wakurugenzi waliagiza wakuu wa idara kuchangisha fedha toka kwa watumishi walio chini yao na kwa kwa hiyo;
  • Kila mtumishi alilazimishwa kuchangia Tshs 2,000/=
  • Kila taasisi zililazimishwa kuchangia fedha mfano; Tshs. 10,000/= (shule za msingi), Tshs. 20,000/= (shule za sekondari) nk nk kutegemea na ukubwa wa taasisi
  • Kila mfanyabiashara alilazimishwa kuchangia kati ya Tshs 2,000; 3,000; 5,000 na 10,000 kutemea na ukubwa wa biashara
  • Mwenge huleta usumbufu sana kuliko manufaa na kinyume na malengo unapokuwa unapita katika maeneo ya watu; mfano ni kusimama kwa shughuli nyingi za kiofisi na uzalishaji katika taasisi nyingi za umma kwa sababu wengi wa maafisa hasa katika ngazi ya wilaya hujikuta wako bize kwa shughuli za mwenge na watu kukosa huduma kwa hata wiki nzima bila sababu yoyote ya msingi zaidi ya hii kitu MWENGE WA UHURU iliyopitwa na wakati!!

KWA NINI CHADEMA WANAUPINGA MWENGE WA UHURU?
Kwanza naomba nikusahihishe kwa kukuambia kuwa you are making a big mistake unapokuwa hutaki kufanya mabadiliko ya kifikra, unapokuwa hutaki kubadili mitazamo yako (mindset) katika mambo mbalimbali kwa kudhani kuwa kila kinachopingwa/kosolewa na CHADEMA kinachotokana/asisiwa na serikali ya CCM basi ni kibaya!!.

Aidha si tu CHADEMA wanaopinga hili hata CCM wanaathiriwa sana na sera na mipango ya serikali yao wenyewe.Mfano leo ktk Bunge katika mjadala wa ishu hii ya Mwenge karibu kila Mbunge bila kujali itikadi zao za kisiasa walikuwa wanaonekana wazi kutoridhishwa na majibu ya serikali kuutetea mwenge.Na mmoja wa wabunge wa CCM waliopata nafasi ya kusema kuhusu mwenge ni mbunge Kessy nadhani ni wa huko Nkasi - Mpanda. Huyu bwana ni CCM na alionesha wazi kutoridhishwa na falsafa ya MWENGE WA UHURU kwa sasa kwani dhima nzima iliyokusudiwa imeshapitwa na wakati na badala yake mwenge ni kama vile unaongeza matatizo ambayo ulipaswa kuyatowesha mfano; umaskini, Rushwa na ufisadi,maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa njia ya ngono nk nk

Kwa hiyo basi CHADEMA hawaoni umuhimu wa Mwenge wa Uhuru kwa sasa kwa sababu logic nzima ya Mwenge ilishapotoshwa na CCM na badala yake mwenge umekuwa ukileta adha isiyo kifani kwa wananchi. Na ndiyo kusema kwamba CHADEMA wanaongea yaliyo miyoni mwa wananchi, wanawakilisha mawazo halisi ya wananchi.!!
Matusi ne sehemu ya maisha ya wanachadema unadhani ukitukana unabadili mantiki ya hoja si kweli,
chadema kumekuwa na desturi ya kupinga kila kitu lakini wao hawasemi watafanya nini pale wanapopinga kitu watu kama hawa sijui tuwape jina gani ambalo linawafaa kama siyo waharibifu wa maendeleo ya jamii yetu.
 
Kwa mda mrefu sasa wabunge wa Chadema wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru.

Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge, Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi.

Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.

Binafsi japo siwajui CHADEMA sitaki hata kuusikia.... Hivi ulishakaa chini na kukokotoa ni kiasi gani cha kodi zetu kinatumika ili kufanikisha zoezi la kuukimbiza nchi nzima au upo kishabiki. Kwani hiyo miradi haiwezi kuanza kujengwa au kutumika kama mwenge haujapita kuizindua. Lazima tuwe na sera za kuwafikiria wananchi siyo kila siku tunapiga bla bla na kutafuta miradi ya kuiba fedha na raslimali za nchi. Nipe faida mbili za kimaendeleo zinazoletwa na mwenge????? Usisahau na kuongeza maambukizi ya virusi vya ukimwi.
 
mbio za mwenge wa uhuru ni muhimu kwa taifa. miradi mingi ya maendeleo huzinduliwa na watu hujumuika na kufurahishwa na ngoma za kitamaduni. mbali na miradi ya maendeleo, mwenge unakuza utamaduni hapa nchini

Kanda mmoja wa magamba ambae alikuwa mkuu wa mkoa wa lindi alipiga marufuku mikesha ya mwenge mkoani kwake eti kwa vile unasambaza ukimwi.
 
Sina uhakika na mleta mada kama amefanya utafiti wa kina na wakutosha.
Na hata wachangiaji wengi, hawajibu hoja ya msingi.

Binafsi naona twende kwa uhalisia:
1. Gharama za Mbio za Mwenge Kitaifa Vs Faida Kitaifa
2. Mwenge ukiwa katika mkoa au wilaya gharama zake ni zipi na faida ni zipi?

Tuache kuongea habari za kutunga na za kusikia mitaani.
 
Hujajibu swali kwa nini chadema wanaupinga mwenge wa uhuru hata sababu wanazotoa hazina maana.

Jibu: Mwenge ni ushirikina unaotumiwa na watawala ili kupumbaza watanzania washindwe kutambua haki zao na wao kutawala bila kupingwa. Ndio maana hata wewe umekuwa zoba/zombi sababu ya mwenge. Unaona kabisa kwa macho maovu wanayofanya watawala lakini kwako ni sawa tu. Ukiambiwa unapotea unatoa matusi yaani ni kama mwanaume aliyewekewa dawa(limbwata) na mkewe ili hata akiingiza bwana ndani ya nyumba basi mmewe ampishe kitanda.
 
Kuthibitisha kuwa chadema wanamatatizo ni pale wanapopingana hata wao kwa wao,
kama mnakumbuka wenje aliwahi kukana bungeni kuwa wao siyo walaberali lakini jana mtei akiwa anachanga hapa jf alithibitisha kuwa chadema na uliberali ni damu damu kwa hiyo wao wapo kupinga kila kitu.
 
Jibu: Mwenge ni ushirikina unaotumiwa na watawala ili kupumbaza watanzania washindwe kutambua haki zao na wao kutawala bila kupingwa. Ndio maana hata wewe umekuwa zoba sababu ya mwenge. Unaona kabisa kwa macho maovu wanayofanya watawala lakini kwak6 ni sawa tu. Ukiambiwa unapotea unatoa matusi yaani ni kama mwanaume aliyewekewa dawa(limbwata) na mwanamke ili hata akiingiza bwana ndan ya nyuma basi mmewe ampishe kitanda.
Kwani menge unatoa hotuba za kupumbaza watu au kunakazi gani inayofanywa na mwenge ya kufunika watu wasijue kinachoondelea au umekurupuka kuchangia bila kujua msingi hoja yenyewe.
 
Mkuu, Kessy ni maoni yake. ila bado hujajibu swali. kwa nini chadema wanachukia Mwenge wa uhuru

Wanachadema na uyo Kessy wa ccm wanaupinga mwenge kwa capacity ya utanzania wao.
nimekutolea mfano wa mbunge wa ccm anaepinga mwenge ili upanue wigo wa kufikiri na ubadili title.
 
Wewe naona umekurupuka. Kwani umeambiwa mwenge unapeleka fedha za miradi? Mbio za mwenge hutumika kuzindua miradi iliyotekelezwa kupitia vyanzo mbalimbali vya mapato

Kwa hiyo isipozinduliwa na hiki kibatari basi ina maana miradi hiyo haipo na haitafanya kazi kwa wananchi?....Fikiri kwa kutumia akili zilizofichwa ndani ya kichwa chako chenye nywele hizo!!

Halafu niwaambie kitu nyie wapenzi na wana CCM? Ni rahisi sana iwapo mnataka ku-win support ya wananchi kwa sasa. Ni kwa kusikiliza sauti za wananchi wanachokitaka. Moja ya kero kubwa kwa wananchi kwa sasa ni ishu hii ya hiki kibatari - MWENGE WA UHURU. Ni kero,kero,kero mpaka baaasi!!

Hebu fikiria hii kidogo labda utaelewa na kuzinduka; Umeshawahi kuona wapi kwamba kijijij ambacho barabara yake haijawahi kuchongwa kwa miaka mi5 hadi 10 na kwa sababu mwaka huu kipo ktk ratiba ya kipitiwa na mwenge, basi ma CCM kupitia serikali yao dhaifu yanapitisha greda na kufumua vumbi ambalo mwenge ukipita tu basi sahau tena mpaka baaada ya miaka mi5 au 10 tena!!!....Sasa jiulize katika mtindo huu wa utendaji unaweza kuwahadaa wananchi hadi lini??

Tatizo si CHADEMA hapa, tatizo ni sera na mipango mibovu ya serikali ya CCM. Hivi kama kweli mwenge unawaletea maendeleo wananchi na hayo maendeleo kila mwananchi anayaona, anayahisi na anayagusa; CHADEMA watasema nini sasa mbele ya wananchi hawa? Si itakuwa ni sifa kwa CCM na serikali yao tu?

TUMIENI AKILI, ONGEENI LUGHA YA WANANCHI kinyume cha hapo mtagombana sana na CHADEMA na in reality mtakuwa hampmbani na CHADEMA bali mtakuwa na mpambana na wenye nchi wenyewe....WANANCHI!!
 
Back
Top Bottom