Kwanini Chadema haiwalipi hawa?

Kwanini Chadema haiwalipi hawa?

Kuelekea ukombozi ni lazima wachache ama wengi wawe tayari kuumizwa kwa faida ya wengi.

Hii ni vita ya kuelekea ukombozi ,na ijulikane kuwa wafanayabiashara na wenye pesa hawakichangii CHADEMA kwani wanaogopa CCM.

vitu vingine tuwe tayari kusema ukweli mbona hata hapa JF inaendeshwa kwa kuchangiwa na wanachama wake wenye uwezo wa kuchangia?

Mbona hapa hamlalamiki kuwa waache kuchangia?

Nani anamlipa Invisible na JF Crew yote hapa ?mbona wao wanajitolea na kufanya bure?

Ama kujitolea CHADEMA ndio dhambi na kosa?
.CHADEMA kujitolea ni kosa kubwa.lakini sisi wa ccm tunajitolea kwani wenyeviti wa kata na matawi wa ccm wanalipwa wanajitolea kama mbowe anavyojitolea.wangwe si mwanasiasa ni mbishi nashangaa kwanini chadema walmempa madaraka yote haya.mwanzoni alikuwa akiitwa rasta.naamini hata kupata ubunge somply CCM waling'ang'ania chambili lakini wamgemuweka mtu mwingine wangwe asingeambua kitu.tarime ni wana ccm
 
2008-07-02 09:46:16

My Take:
- Kwanini Chadema isiwalipe viongozi wake? Hicho chama siyo taasisi ya dini au NGO, huu mtindo wa kulipa fedha za wao wenyewe na wengine kutolipwa ni mtindo mbaya. Hata mtindo wa Mbowe kutoa fedha yake mfukoni kwa ajili ya Chadema siyo mtindo mzuri kwani unamfanya aonekane kama ana maslahi zaidi ya mtu mwingine. Chama kiendeshwe kama Chama. Hata kama chama hakiwezi kuwalipa inavyopaswa ni muhimu kuwa na token payment hata kama Shs. 10,000 kwa mwezi kwa viongozi lazima walipwe, wasifanye kazi za chama bure.

- Kama Bajeti ya Chama ni ndogo kuliko mahitaji yake, ni lazima wajifunze kufanya mambo ndani ya bajeti. Kama ni kuanzisha miradi n.k wafanye hivyo lakini wasifanye vitu ambavyo hawana uwezo wa kuvigharimia. Katika hili wanaweza kuanzisha miradi ya Chama. Hili linawezekana kwa kuanzisha kampuni ya Chama (Holding Company) na wanaweza kuangalia ni jinsi gani chama kinaweza kumiliki kitega uchumi. Kama mnapata karibu milioni 66 kila mwezi na fedha zote zinaishia kwenye matumizi na hazizalishi basi kuna tatizo la kiuwekezaji.

- Uongozi mkuu wa chama ujitoe kwenye kusimamia fedha na badala yake waajiri watu ambao wana weledi wa mambo ya fedha. Mhasibu Mkuu, Mkaguzi wa ndani, watunza fedha n.k na wataalamu wa Boharia. Wanasiasa wabakie kufanya maamuzi ya kisiasa. Na watumishi hawa walipwe kwa kiwango cha fani zao, na wasiwe na uhusiano wowote ule wa karibu na kiongozi yeyote wa juu wa chama hicho. Kabila, mkoa, rangi, au dini na jinsia don't count.

- Ruzuku ya Chama isipokelewe na kiongozi wa kisiasa, period. Fedha za ruzuku au fedha nyingine yoyote inaenda moja kwa moja kwenye akaunti ya chama na hesabu zake zinaeleweka na zinasimamiwa ipasavyo. Lazima waweke mfumo mzuri wa usimamizi wa fedha ili saa ya yoyote ijulikane wana fedha kiasi gani, ziko wapi, na zimetumika vipi.

- Viongozi wa kisiasa warudi kwenye kuimarisha chama, kwa kupika makada wa kisiasa, kufungua matawi ya chama n.k. Sikumbuki mara ya mwisho kusikia Zitto, Slaa, au Mbowe amefungua tawi la Chadema mahali popote ilikuwa lini. Chama hakijengwi kwa hotuba za Bungeni, au maneno ya magazetini, bali kwa kushawishi watu kukikubali na kuzielewa sera zake. Na njia pekee ya kuonesha kuwa watu wanawakubali ni watu kujiunga na chama hicho.

Madai kuwa watu wanaelewa kuwa Chadema inapigia kelele ufisadi zaidi n.k ni madai tu lakini ushahidi wa watu kuelewa unaonekana kwa watu kujiunga. Je tangia mambo ya ufisadi yaanze na tangia sakata la Zitto Chadema imejipatia wanachama wangapi, na kiasi cha watu kujiunga kina tofauti gani na kabla ya hapo. Kama hakuna tofauti kubwa na inayoonekana basi kuna tatizo mahali fulani.

Mengine.. nitawaandikia in private katika kulinda "heshima ya chama" chenu.


MKJJ: Again, a lot of sense in what you said. Lakini naogopa kusema kwamba maandishi yako yanaonyesha hujajua vizuri ugumu wa kupata fedha ya kuendesha chama cha siasa Tanzania. Ni kweli kwamba kinadharia inapaswa chama cha siasa kiendeshwe kwa michango ya wanachama, wafuasi na wapenzi wa chama hicho. Hivi ndivyo inavyofanyika katika nchi za wenzetu ikiwemo hapo ulipo, Amerika ya Kaskazini. Lakini ukweli wa mambo ni kwamba wanachama wa vyama vya siasa Tanzania na Afrika kwa ujumla hawajaanza kuwa na utamaduni wa kuchangia gharama za kuendesha vyama vya siasa, hasa baada ya mfumo wa vyama vingi kuanza. Na hili ni tatizo kwa vyama vyote sio tu vya upinzani bali pia vinavyotawala. Tatizo hili partly linasabiishwa na ukweli kwamba wananchi walio wengi hawaoni kama vyama vya siasa vipo kwa ajili yao. Wananchi wengi wanaviona vyama vya siasa kama ngazi na nyenzo za kuwafikisha watu fulani kwenye ngazi za uongozi ambako ni ulaji. Kwa hivyo wanafikiri kwamba kama ni kuchangia wachangia wale wanaotaka kuwa viongozi kupitia hivyo vyama. Ni kwa sababu hii CCM wakaibuka na jambo la ovyo kabisa la ruzuku ambalo wakijua kwamba ni wao watakaonufaika nalo kisiasa.

Kumbe basi kinachotakiwa hapa ni kubadilisha mtizamo wa wananchi juu ya kazi ya vyama vya siasa ili wafike mahala waone kwamba bila michango yao ya hali na mali hivyo vyama haviwezi hata siku moja vikasimama kama taasisi za kitaifa. Inabidi pia tutambue, kama ulivyogusia katika post yako, kuwa bila wananchi kuamua kuviendesha hivi vyama kwa michango yao ya hali na mali, vitaendelea kuonekana kuwa ni mali za watu fulani tu na sio taasisi za kitaifa.

Kwa hiyo utaona kwamba, kifedha, vyama vya siasa vinaendeshwa kwa ufadhili wa watu wachache wanaojitolea wakiwemo viongozi wa hivyo vyama. Ni kwa sababu hii, naamini, hata Rais Kikwete ameshindwa, kwa aibu, kutekeleza ahadi yake ya kuleta mswaada wa sheria wa kudhibiti matumizi ya pesa katika vyama vya siasa, hasa wakati wa uchaguzi.

Hata hivyo nakubaliana na wewe sana kwamba kuna tatizo katika namna hoja hii ilivyowasilishwa na uongozi wa chadema. Hapakuwa na sababu ya kueleza kwamba wanajitolea. Hilo tunalitambua kwa sababu ndio maana ya utumishi na ndio maana ya kazi ya siasa, hasa katika opposition.

Nisema pia kwamba sisi as opposition hatuna sababu ya kulialia kuhusu mipango ya CCM au wapinzani wetu wengine kutaka kutubomoa. Kwenye siasa bwana msiba wako ni harusi ya mpinzani wako. Ndio mana nikasema huko nyuma kwamba hili sakata la Wangwe ni tatizo kwetu lakini ni harusi kubwa kwa CCM kwa sababu katika siku mbili tatu hivi mjadala umeweza angalau kugeuka kutoka ufisadi hadi kuwa mgogoro katika CCM.

Wapiga kura wanataka viongozi na vyama imara ambavyo vinaweza kupambana. Sasa hii ya kusema kwamba kuna watu wanampango wa kuibomoa CHADEMA haitusaidii kutuonyesha kwamba sisi tupo imara kupambana bali ina-portray kwamba bado tu wanyonge. Kinachotakiwa hapa ni kujibu mapigo. Kwenye siasa hakuna mambo ya ukipigwa shavu la kushoto unageuzi la kulia. Kwenye siasa mwenzako akikupiga shavu la kulia, wewe unamtwanga la kushoto halafu unamaliza kabisa na sikio lake. Sasa kama kuna ushahidi wowote kwamba kuna watu ndani ya chadema wanatumiwa na CCM kazi yetu ni kujibu mapigo haya kama vile CUF walivyomfanya Tambwe Hiza. Hii ya kueleza vilio vetu kwa Nipashe havitusadii sana.
 
unachoshindwa kujua ni kwamba JF sio chama cha siasa chenye malengo ya kuongoza nchi siku moja kama chadema, Hii ni forums ambayo watu wachache wamejitolea kwa moyo mmoja na hata wewe hujakatazwa kufanya hivyo, lakini Chadema ni chama cha siasa na kina katiba na dhumini la kuongoza nchi yetu kama ikibahatika,we unategeme siku Mbowe akisema anataka kulipwa pesa zake zote alizo jitolea wakati wako IKulu si watauza nchi yetu , kuwa makini ndugu yangu

Mi nilidhani kujitolea si deni, I mean kujitolea hakuhitaji malipo ama marejesho ya kile ulicho jitolea, ama ni kiswahili inanipinga chenga kidogo?
 
Mkuu Slaa.
Sote tunatambua sana mchango wako wakupigana na mafisadi nchini.
Lakini tunasikitika sana kuona unatumia mtandao wa simu wa FISADI aliye kubuhu Rostam Aziz na hapa imewahi tolewa thread watu kususia huduma zote za mafisadi kama huyu.
Kwa hiyo mkuu kuendelea kutumia line ya simu ya VODA maanake unamuunga mkono RA anaye tuibia nchi yetu kwa kuwekeza kwenye hii kampuni ya VODA.
Tunaomba ubadilishe hii line ya VODA tupo tayari kukuchangia ununue TIGO au ZANTEL.
Ahsanteni.

Sema atoke kwenye mtandao ambao fisadi anayetambulika, ana share aende kwenye mtatandao ambao ni wa fisadi ambaye hajaumbuliwa (bado)
 
MMK
Nakushukuru sana kwa ushauri kuhusu uendeshaji wa fedha kwenye vyama vya siasa. Hata hivyo, Chadema ni chama kinachofanya kazi yake kwa uwazi. Hatuna la kuficha napenda kueleza ifuatavyo:
i) Uamuzi wa viongozi wakuu, tena wanaotumia muda wao wote kwa shughuli za chama, za kisiasa na uendeshaji, ni uamuzi uliofanyika kwa hiari na kupitia vikao halali vya chama. Kwa bahati mbaya maamuzi mengine hayafiki hadharani. Chadema haioni cha ajabu katika hatua hii. Mwalimu Nyerere asingejitolea enzi za uhuru, na kuchangiwa na wapenzi wachache waliokuwa na uwezo leo tusingelikuwa na Uhuru. Nadhani wenye mapenzi mema na nchi hii wataelewa kuwa mapambano tuliyonayo ni mapambano yanayohitaji kujitolea kwa kiwango kikubwa. Viongozi wakuu wa Chadema kwa kutambua hili, waliamua kwa hiari yao, kujitolea ili ruzuku kidogo iliyoko itumike kwa shughuli za uenezi. Bendera, Kadi, nyaraka mbalimbali,ujenzi wa Ofisi stahiki Makao Makuu ya Chama kama sura ya Chama, kuwekeza kwenye miradi ya muda mrefu ya kuitegemeza chama( kazi hiyo imekwisha kufanyika siyo nadharia na kwa yeyote mwenye nia ya kutaka kujua tunaweza kumpa taarifa za kina), ziara za uenezi na kadhalika.
2) Viongozi wa juu wa Chadema ni Wabunge, ukimwacha Mwenyekiti. Mishahara wanayopata ikitumika kuendeleza Chama kuna dhara gani, Chama hujengwa na wenye moyo. Hili halina maana ya wenye kuchangia chama ndio waamuzi katika maamuzi ya chama. Chama kinaendeshwa kwa Katiba, Kanuni, Maadili, na Itifaki ya Chama. Maamuzi yanapofanywa kwa imla hofu hizo hutokea. Kwa Chadema, ambayo maamuzi yake hufanyika yote na vikao halali, mipango huenda kwa kadiri ya Strategic Plan, ambayo nayo si siri, ipo wazi kwenye Mtandao wa Chama, na kila mwenye nia njema anaweza kuipata bila tatizo. iwapo kuna mwenye kuhitaji maelezo ya ziada tuko tayari kuyatoa wakati wowote, vitabu vya Hesabu ya Chama ni mali ya Wanachama na wakati wowote Mwanachama anaweza kuomba taarifa atapewa, na au anaweza kufika Makao Makuu ya Chama akaona vitabu hivyo bila gharama yeyote. Taarifa zote za fedha hutolewa kwenye vikao vya Kamati Kuu, na sijawahi kuona Taarifa ya Fedha ikikataliwa kwa ubadhirifu au kwa sababu yeyote ile. Wajumbe wa Kamati Kuu ni mashahidi. Taarifa ya Fedha hutolewa pia kwenye Baraza Kuu na Mkutano Mkuu kuendana na Ratiba ya Kikatiba ya Vikao hivyo.
3: Fedha za Chadema hukaguliwa na Wakaguzi wanaotambulika kisheria, na huwasilishwa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kwa wakati na kwa mujibu wa Sheria.
4: Ili kuepuka Wachache wenye uwezo kufanya chama kuwa mali yao, Chadema inaoutaratibu ambao sina hakika vyama vingapi unao, wa kutathmini na kutambu mchango wa kila mwanachama kwa maana ya fedha zake anazochangia kwenye chama, muda wake anaotumia kwa ajili ya shughuli za Chama ( hatua hii inafanyika kwa sasa Makao Makuu tu kwa vile Instruments za kufanya Tathmini hii kwenye mikoa na Wilaya bado inafanyiwa kazi na hata ya Makao Makuu bado inaendelea kufanyiwa kazi. Mathalan muda wa mtumishi wa Chama anayefanya kazi baada ya saa rasmi za kazi hutathminiwa na kupewa thamani ya fedha kama mchango wake kwa ujenzi wa chama. Inahitajiwa fikra mpya ili ukombozi tunaoendelea nao uweze kufanikiwa. Lakini kutegemea fedha tu hakutatufikisha mahali.

Hivyo, Tafsiri sahihi ya Kauli ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Chadema, inaweza kuhojiwa katika misingi hii. Nimeona nieleze hili kwa misingi ya uwazi kwa vile Chadema hatuna cha kuficha, chama ni cha wote wenye nia njema, na hata wasiokitakia mema kama wapo ni vema wakajua Chadema inaendeshaje shughuli zake ili wasiohoji kwa nadharia na kwa hisia. Mwenye kuhitaji Taarifa zaidi, Dr. Slaa, anapatikana kwa Simu na +255 784 666995 au +255 754 366 995 au kupitia E mail zangu slaa@chadema.net, wslaa@hotmail.com. Nafurahi kwa wote waliochangia kwa angle yeyote ile kwani licha ya kuwa kila mmoja ana uhuru wa kutoa maoni yake, pia kila mwanademokrasia halisi hutambua mchango wa kila mmoja na pia anaweza kuokoteza mawazo mazuri katika michango hiyo. Hakuna mchango uko mbovu tu, hata uliombovu sana unajambo zuri, japo dogo la kuweza kujifunzia. Naomba radhi si nia yangu kutoa mhadhara, lakini kila inapohitajika katika mada yeyote ile nitafanya hivyo kwa maslahi ya nchi yetu, wanachama wetu na wote wenye mapenzi mema.

Dr Slaa
Naamini mwalimu anapomkemea mwanae/mwanafunzi si kwamba hua na nia mbaya naye bali ni kumtaka afanye yaliyo mema zaidi.

Kufananisha CHADEMA na TAA/TANU mimi nafikiri ni upotoshaji kwanini nasema hivi Mazingira yale ya ukoloni ya TANU si haya mazingira ya CHADEMA Na japo sikuwapo wakati huo bado siamini kama TAA/TANU ilikua inapokea ruzuku ya M.66 kwa mwezi kutoka serikali ya mkoloni.

Na bado siamini wale WATUMWA kwa thamani walikua na uwezo wa kuchangia M.66 kwa mwezi kwa TAA yao.

DR Slaa
Naomba nikuchoshe kwa maelezo yanayoambatana na maswali
Nia ya CHADEMA ni nini haswa??? CHADEMA imeanzishwa lini?? Kama hujayapata maswali yangu vizuri ngoja niongeze CHADEMA na CCM kimantiki tofauti yao nini?? My God!!

Kama CHADEMA inazaidi ya miaka 15,kama CHADEMA inapata ruzuku kutoka serikalini .Lakini bado mmshindwa kuweka miradi ya CHAMA kujisimamia chenyewe chama tu mmeshindwa je SERIKALI nzima mtaweza kubuni miradi jinsi ya kutukwamua ??

Serikali bajeti yake kwa 40% inategemea kuomba omba ninyi mnapiga kelele sasa basi mbona chama chunu kinategemea omba omba kwa 100% ,Hamuoni mkiingia madarakani ndio ombaomba itakua zaidi ya 100% maana hapo Mbowe vijisenti vyake havitasaidia kitu,hapo hakuna mfanyakazi atakeyefanya kazi bure.

au na ninyi mtafanya safari nyingi badala ya US mtaelekea kwa PuTIN.

NB: Kama mimi ndio ningekua msajiri wa VYAMA VYA SIASA kabla ya kusajiriwa chama ningepropose kikopeshwe na serikali kama BILION 20. harafu wakaanzisha mradi ambao ndani ya miaka 3 kiwe kimeajili watu zaidi ya 3000 kinawalipa mshahara std ,wakifeli wanatupwa jera kifungo cha maisha,Harafu vyama vyote vilivypo ndani ya Very limited Time wawe na miradi yao inayoendesha chama na wawe wameajiri zaidi ya watu 1000.Kufeli kwa hilo inamaana chama KINAFUTILIWA MBALI.

Maana watu wamekua wasanii tu ili kujinufaisha kumbe hata mpango wa kuwaendeleza watanzania hawanao.
Nasema kufeli kubuni miradi ya CHAMA lakini ukaendelea kuhubiri kubuni miradi ya KITAIFA ni USANII MKUBWA.mtu huwezi shindwa buni miradi ya familia ya kuwapatia kipato familia ikawa inalala njaa harafu ukawa unahubiri kubuni miradi ya wanakajiji wote. USANII HUU.
 
Dr Slaa
Naamini mwalimu anapomkemea mwanae/mwanafunzi si kwamba hua na nia mbaya naye bali ni kumtaka afanye yaliyo mema zaidi.

Kufananisha CHADEMA na TAA/TANU mimi nafikiri ni upotoshaji kwanini nasema hivi Mazingira yale ya ukoloni ya TANU si haya mazingira ya CHADEMA Na japo sikuwapo wakati huo bado siamini kama TAA/TANU ilikua inapokea ruzuku ya M.66 kwa mwezi kutoka serikali ya mkoloni.

Na bado siamini wale WATUMWA kwa thamani walikua na uwezo wa kuchangia M.66 kwa mwezi kwa TAA yao.

DR Slaa
Naomba nikuchoshe kwa maelezo yanayoambatana na maswali
Nia ya CHADEMA ni nini haswa??? CHADEMA imeanzishwa lini?? Kama hujayapata maswali yangu vizuri ngoja niongeze CHADEMA na CCM kimantiki tofauti yao nini?? My God!!

Kama CHADEMA inazaidi ya miaka 15,kama CHADEMA inapata ruzuku kutoka serikalini .Lakini bado mmshindwa kuweka miradi ya CHAMA kujisimamia chenyewe chama tu mmeshindwa je SERIKALI nzima mtaweza kubuni miradi jinsi ya kutukwamua ??

Serikali bajeti yake kwa 40% inategemea kuomba omba ninyi mnapiga kelele sasa basi mbona chama chunu kinategemea omba omba kwa 100% ,Hamuoni mkiingia madarakani ndio ombaomba itakua zaidi ya 100% maana hapo Mbowe vijisenti vyake havitasaidia kitu,hapo hakuna mfanyakazi atakeyefanya kazi bure.

au na ninyi mtafanya safari nyingi badala ya US mtaelekea kwa PuTIN.

NB: Kama mimi ndio ningekua msajiri wa VYAMA VYA SIASA kabla ya kusajiriwa chama ningepropose kikopeshwe na serikali kama BILION 20. harafu wakaanzisha mradi ambao ndani ya miaka 3 kiwe kimeajili watu zaidi ya 3000 kinawalipa mshahara std ,wakifeli wanatupwa jera kifungo cha maisha,Harafu vyama vyote vilivypo ndani ya Very limited Time wawe na miradi yao inayoendesha chama na wawe wameajiri zaidi ya watu 1000.Kufeli kwa hilo inamaana chama KINAFUTILIWA MBALI.

Maana watu wamekua wasanii tu ili kujinufaisha kumbe hata mpango wa kuwaendeleza watanzania hawanao.
Nasema kufeli kubuni miradi ya CHAMA lakini ukaendelea kuhubiri kubuni miradi ya KITAIFA ni USANII MKUBWA.mtu huwezi shindwa buni miradi ya familia ya kuwapatia kipato familia ikawa inalala njaa harafu ukawa unahubiri kubuni miradi ya wanakajiji wote. USANII HUU.

wewe mawazo yako ni sawa na nguvu za giza
 
augustoos, umeonaee! sijamuelewa kabisa.
Chama si kampuni, si ngo.
Inakaribiana zaidi na madhehebu ya dini, kwani huendeshwa kwa kujitolea, au kwa hisia, au kwa msukumo wa kuongoza nchi.
si kwa faida binafsi, moja kwa moja. Japo ndani kabisa huwa kuna masilahi binafsi ikiwemo 'power'.
Kwa hali ya sasa vyama kuwa na mradi utakaokiendesha chama ni almost impossible.
 
Yaani Mkamap unataka chama cha siasa kikopeshwe bilioni 20 kiendeshe miradi ya kiuchumi? Unatumia nadharia gani za kisiasa katika kujenga hoja zako au ndio tatizo la elimu ya siasa nchini mwetu ambalo tunalo wengi? Hebu jifafanue kidogo.

Kuhusu historia ya chadema, jamani hata wewe hapa kwenye JF unataka Slaa aanze kukopi historia ya chadema kutoka kwenye website na kukuletea hapa? Naomba tusiwe wavivu wa kutafuta habari. Kwa kuwa wewe haya mambo ya teknolojia upo pazuri, huna huja ya kumsumbua Dk Slaa katika kukuelezea historia ya chadema, nenda kwenye tovutu ya chadema hasa hii section: http://www.chadema.net/maoni/kijue.php.
 
Haina haja ya Kumlipa Mbowe sababu hapo CHADEMA ni sehemu ambapo ni kijiwe chake cha kusemea.Yeye si Mwanazuoni maarufu hivyo hawezi kutumia Elimu kueleza watanzania wakamwelewa.ndiyo maaana alienda Shule hivi karibuni ili aonekane na yeye ana Elimu

Suala la Pili ni kwamba CHADEMA kama wao wameshindwa kutafuta Wafadhili wa kuendesha chama sababu hakuna watu wabunifu ambo wanaweza kuandika Proposal nzuri labda waandikiwe na kina Baregu au Zitto ila wengi wao ni watu wanotawaliwa na Emotion.

The Truth is Upinzani wa kweli utapatikana mpaka pale CCM itakapogawanyika na kupatikana wapinzani wenye uwezo wa kuongozi siyo wanaotafuta Uongozi.

Kimsingi ni kuwa Serikali yetu inashindwa kuendelea kwasabu ya watu wengi ambo wanafanya kazi serikalini ni Vilaza wa kutupwa na kila siku wanataka kushindana na watu wenye uwezo na wanalipwa vizuri na hii inasababisha Rushwa.The same as CHADEMA.

Na kwa Ushauri tu..

Mnyika arudi akamilize shule yake ya BBA pale Mlimani na wengine wajiendeleze,Naamini mkiwa na Elimu hii itasaidia nyie kujituma kwa kutumia Proffesional zenu na kukisaidia Chama
 
2) Viongozi wa juu wa Chadema ni Wabunge, ukimwacha Mwenyekiti. Mishahara wanayopata ikitumika kuendeleza Chama kuna dhara gani, Chama hujengwa na wenye moyo. Hili halina maana ya wenye kuchangia chama ndio waamuzi katika maamuzi ya chama. Chama kinaendeshwa kwa Katiba, Kanuni, Maadili, na Itifaki ya Chama. Maamuzi yanapofanywa kwa imla hofu hizo hutokea. Kwa Chadema, ambayo maamuzi yake hufanyika yote na vikao halali, mipango huenda kwa kadiri ya Strategic Plan, ambayo nayo si siri, ipo wazi kwenye Mtandao wa Chama, na kila mwenye nia njema anaweza kuipata bila tatizo. iwapo kuna mwenye kuhitaji maelezo ya ziada tuko tayari kuyatoa wakati wowote, vitabu vya Hesabu ya Chama ni mali ya Wanachama na wakati wowote Mwanachama anaweza kuomba taarifa atapewa, na au anaweza kufika Makao Makuu ya Chama akaona vitabu hivyo bila gharama yeyote. Taarifa zote za fedha hutolewa kwenye vikao vya Kamati Kuu, na sijawahi kuona Taarifa ya Fedha ikikataliwa kwa ubadhirifu au kwa sababu yeyote ile. Wajumbe wa Kamati Kuu ni mashahidi. Taarifa ya Fedha hutolewa pia kwenye Baraza Kuu na Mkutano Mkuu kuendana na Ratiba ya Kikatiba ya Vikao hivyo.

4: Ili kuepuka Wachache wenye uwezo kufanya chama kuwa mali yao, Chadema inaoutaratibu ambao sina hakika vyama vingapi unao, wa kutathmini na kutambu mchango wa kila mwanachama kwa maana ya fedha zake anazochangia kwenye chama, muda wake anaotumia kwa ajili ya shughuli za Chama ( hatua hii inafanyika kwa sasa Makao Makuu tu kwa vile Instruments za kufanya Tathmini hii kwenye mikoa na Wilaya bado inafanyiwa kazi na hata ya Makao Makuu bado inaendelea kufanyiwa kazi. Mathalan muda wa mtumishi wa Chama anayefanya kazi baada ya saa rasmi za kazi hutathminiwa na kupewa thamani ya fedha kama mchango wake kwa ujenzi wa chama. Inahitajiwa fikra mpya ili ukombozi tunaoendelea nao uweze kufanikiwa. Lakini kutegemea fedha tu hakutatufikisha mahali.


Mhe Slaa,

Nimependezwa na majibu ya hoja zilizotolewa na wachangiaji hapa JF. Nashukuru kwa kuja kutuweka sawa; nina swali la nyongeza ambalo naomba kwa faida yangu na wanabodi wengine ulipatie ufafanuzi.

Ref Jibu la 4. Huu utaratibu mliojiwekea Chadema wa kubadilisha muda wa Mwanachedema kuwa mchango wake kifedha.

Je utaratibu huo unaangalia Cheo/Majukumu ya wanachama wanaojitolea au muda unabadilishwa kuwa fedha kwa kiwango sawa? Mfano: Mhe Mbowe (Mwenyekiti) ametumia masaa 10 kwa shunguli za chama, masaa haya 10 kila saa ni Shs 10; mtayahesabu Shs 100 (10 x 10 = 100) kutoka kwa Mbowe kwenda Chadema kama mchango wake. Wakakti huo huo, J.J Mnyika amejitolea masaa 10 naye pia kwa shughuli za chama...yeye naye itahesabika kuwa amechangia Shs 100 kwa Chadema au kiwango cha kuzidisha kinatofautiana kwa nafasi aliyonayo mtu kwenye chama???

Natumai nimeeleweka, ni hayo tu.

Nashukuru.
 
Gembe + MkamaP,

baada ya kuanzisha kwa mfumo wa vyama vingi Tanzania, hivi CCM imeweza kuanzisha mradi gani haswa wenye kuweza kutuonyesha jinsi walivyomakini ama wabunifu?

Hivi SUKITA ilikufa mikononi kwa nani?
 
Gembe + MkamaP,

baada ya kuanzisha kwa mfumo wa vyama vingi Tanzania, hivi CCM imeweza kuanzisha mradi gani haswa wenye kuweza kutuonyesha jinsi walivyomakini ama wabunifu?

Hivi SUKITA ilikufa mikononi kwa nani?

Kumbe lengo la Chama chako CHADEMA ni kuona wapi CCM imeteleza nyie ndipo mtokeo hapo?

huo ni kukosa ubunifu,na ndiyo tatizo kubwa amblo liko katika watendaji wetu serikalini.Kila siku wanapandisha Bei za BIA,SODA na SIGARA utazani hakuna jambo lingine amblo wanaweza kufanya kuongeza mapato ya Serikali,na kinanikera mimi ni kila mara nikiwa nje ya nchi naktana nao sana ila hawajifunzi chochote kutoka huko zaidi ya kwenda kula starehe..This is a shame.
 
Gembe + MkamaP,

baada ya kuanzisha kwa mfumo wa vyama vingi Tanzania, hivi CCM imeweza kuanzisha mradi gani haswa wenye kuweza kutuonyesha jinsi walivyomakini ama wabunifu?

Hivi SUKITA ilikufa mikononi kwa nani?

CCM walibuni RUZUKU ya KILA MWEZI toka kodi za WaTZ.
 
Ukitaka kuona tofauti ya Chadema na CCM njoo hapa JF. Dr Slaa anakuja hapa kujadiliana na watanzania mambo muhimu kabisa ya nchi na kujibu maswali yao.

Wakati ccm inakwiba pesa za nchi na kuunda kamati zisizoisha na kukataa kutolea maelezo chochote wanachofanya kwa visingizio vya usalama wa taifa, Dr Slaa, Zitto na Kitila wako hapa wazi kabisa wakijadiliana na watanzania wenzao cha kufanya ili kuinusuru Tanzania.

MUNGU wa mbinguni wabariki chadema, Dr Slaa, Zitto, Kitila na wana JF wote wenye kuipenda nchi yao kwa moyo mkubwa kiasi hiki.

Amen
 
Mwafrika wa kike hapa mie nipo hapa kwa Niaba ya CCM,Nipo hapa kuwaonyesh ni yapi mabaya wanatakiwa kuyafanya.Siyo lazima kila Mtu aje hapa ajisajiri ,Kuna waheshimiwa kibao na viongozi ambao ni Mawaziri na Ni Member hapa..I can Tell you na hautaweza kuamini.

Zitto check PM yako
 
Kumbe lengo la Chama chako CHADEMA ni kuona wapi CCM imeteleza nyie ndipo mtokeo hapo?

huo ni kukosa ubunifu,na ndiyo tatizo kubwa amblo liko katika watendaji wetu serikalini.Kila siku wanapandisha Bei za BIA,SODA na SIGARA utazani hakuna jambo lingine amblo wanaweza kufanya kuongeza mapato ya Serikali,na kinanikera mimi ni kila mara nikiwa nje ya nchi naktana nao sana ila hawajifunzi chochote kutoka huko zaidi ya kwenda kula starehe..This is a shame.

lengo la chama chochote cha siasa ni kushika hatamu za nchi. Kama chama cha siasa hakina lengo la kuongoza nchi basi hicho chama sio cha siasa.

Kwa sasa ccm wamefeli na ni zamu ya chadema au cuf kuonesha mapungufu ya ccm na kuomba ridhaa ya watanzania kuongoza.
 
MMK
Nakushukuru sana kwa ushauri kuhusu uendeshaji wa fedha kwenye vyama vya siasa. Hata hivyo, Chadema ni chama kinachofanya kazi yake kwa uwazi. Hatuna la kuficha napenda kueleza ifuatavyo:
i) Uamuzi wa viongozi wakuu, tena wanaotumia muda wao wote kwa shughuli za chama, za kisiasa na uendeshaji, ni uamuzi uliofanyika kwa hiari na kupitia vikao halali vya chama. Kwa bahati mbaya maamuzi mengine hayafiki hadharani. Chadema haioni cha ajabu katika hatua hii. Mwalimu Nyerere asingejitolea enzi za uhuru, na kuchangiwa na wapenzi wachache waliokuwa na uwezo leo tusingelikuwa na Uhuru. Nadhani wenye mapenzi mema na nchi hii wataelewa kuwa mapambano tuliyonayo ni mapambano yanayohitaji kujitolea kwa kiwango kikubwa. Viongozi wakuu wa Chadema kwa kutambua hili, waliamua kwa hiari yao, kujitolea ili ruzuku kidogo iliyoko itumike kwa shughuli za uenezi. Bendera, Kadi, nyaraka mbalimbali,ujenzi wa Ofisi stahiki Makao Makuu ya Chama kama sura ya Chama, kuwekeza kwenye miradi ya muda mrefu ya kuitegemeza chama( kazi hiyo imekwisha kufanyika siyo nadharia na kwa yeyote mwenye nia ya kutaka kujua tunaweza kumpa taarifa za kina), ziara za uenezi na kadhalika.
2) Viongozi wa juu wa Chadema ni Wabunge, ukimwacha Mwenyekiti. Mishahara wanayopata ikitumika kuendeleza Chama kuna dhara gani, Chama hujengwa na wenye moyo. Hili halina maana ya wenye kuchangia chama ndio waamuzi katika maamuzi ya chama. Chama kinaendeshwa kwa Katiba, Kanuni, Maadili, na Itifaki ya Chama. Maamuzi yanapofanywa kwa imla hofu hizo hutokea. Kwa Chadema, ambayo maamuzi yake hufanyika yote na vikao halali, mipango huenda kwa kadiri ya Strategic Plan, ambayo nayo si siri, ipo wazi kwenye Mtandao wa Chama, na kila mwenye nia njema anaweza kuipata bila tatizo. iwapo kuna mwenye kuhitaji maelezo ya ziada tuko tayari kuyatoa wakati wowote, vitabu vya Hesabu ya Chama ni mali ya Wanachama na wakati wowote Mwanachama anaweza kuomba taarifa atapewa, na au anaweza kufika Makao Makuu ya Chama akaona vitabu hivyo bila gharama yeyote. Taarifa zote za fedha hutolewa kwenye vikao vya Kamati Kuu, na sijawahi kuona Taarifa ya Fedha ikikataliwa kwa ubadhirifu au kwa sababu yeyote ile. Wajumbe wa Kamati Kuu ni mashahidi. Taarifa ya Fedha hutolewa pia kwenye Baraza Kuu na Mkutano Mkuu kuendana na Ratiba ya Kikatiba ya Vikao hivyo.
3: Fedha za Chadema hukaguliwa na Wakaguzi wanaotambulika kisheria, na huwasilishwa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kwa wakati na kwa mujibu wa Sheria.
4: Ili kuepuka Wachache wenye uwezo kufanya chama kuwa mali yao, Chadema inaoutaratibu ambao sina hakika vyama vingapi unao, wa kutathmini na kutambu mchango wa kila mwanachama kwa maana ya fedha zake anazochangia kwenye chama, muda wake anaotumia kwa ajili ya shughuli za Chama ( hatua hii inafanyika kwa sasa Makao Makuu tu kwa vile Instruments za kufanya Tathmini hii kwenye mikoa na Wilaya bado inafanyiwa kazi na hata ya Makao Makuu bado inaendelea kufanyiwa kazi. Mathalan muda wa mtumishi wa Chama anayefanya kazi baada ya saa rasmi za kazi hutathminiwa na kupewa thamani ya fedha kama mchango wake kwa ujenzi wa chama. Inahitajiwa fikra mpya ili ukombozi tunaoendelea nao uweze kufanikiwa. Lakini kutegemea fedha tu hakutatufikisha mahali.

Hivyo, Tafsiri sahihi ya Kauli ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Chadema, inaweza kuhojiwa katika misingi hii. Nimeona nieleze hili kwa misingi ya uwazi kwa vile Chadema hatuna cha kuficha, chama ni cha wote wenye nia njema, na hata wasiokitakia mema kama wapo ni vema wakajua Chadema inaendeshaje shughuli zake ili wasiohoji kwa nadharia na kwa hisia. Mwenye kuhitaji Taarifa zaidi, Dr. Slaa, anapatikana kwa Simu na +255 784 666995 au +255 754 366 995 au kupitia E mail zangu slaa@chadema.net, wslaa@hotmail.com. Nafurahi kwa wote waliochangia kwa angle yeyote ile kwani licha ya kuwa kila mmoja ana uhuru wa kutoa maoni yake, pia kila mwanademokrasia halisi hutambua mchango wa kila mmoja na pia anaweza kuokoteza mawazo mazuri katika michango hiyo. Hakuna mchango uko mbovu tu, hata uliombovu sana unajambo zuri, japo dogo la kuweza kujifunzia. Naomba radhi si nia yangu kutoa mhadhara, lakini kila inapohitajika katika mada yeyote ile nitafanya hivyo kwa maslahi ya nchi yetu, wanachama wetu na wote wenye mapenzi mema.

Dr.
Unaongea siasa nyiiiiiiiiingi, lakini sikushangai kwa sababu hiyo ndio kazi uliyopewa na CHADEMA na umeilia kiapo.

Nyinyi CHADEMA kila kukicha mnakandia kila jambo linalofanywa na CCM badala ya kuangalia nini cha kujifunza kama unavyosema mwenyewe hapa.
CCM wameanza utaratibu wa kufungua matawi nje ya nchi, msaidizi wako Zitto Kabwe ameita hatua hiyo kuwa ni upuuzi.Hivi nyinyi mnaoingia bungeni kushiriki katika maamuzi ya taifa zima mnashindwa kutathmini kiasi gani CHADEMA inaweza kuchangiwa na wanachama wa nje ya nchi iwapo mtafungua matawi??? Ukifungua tawi Kigoma la wanachama 50 na lingine Houston la wanachama 50 unadhani kiuchumi mchango wa wanachama hawa ni sawa???
Ukweli ambao hutaki kuukubali ni kwamba Mbowe hapotezi chochote kwa kutoa pesa kwa CHADEMA na hiyo ndio inampa kiburi cha kuchagua nani wa kufanya naye kazi.Ndio maana anakodisha helkopta kumbe pesa ya kadi za wanachama hamna!
Nakupa siri moja, kwa watanzani walio nje ya nchi upinzani in general ni more popular than the ruling CCM.Iwapo mtaendelea na ushamba wa kukandia kila kinachofanywea na CCM mtaendelea kuitwa upinzani mpaka wewe utastaafu.
 
Kwa sasa ccm wamefeli na ni zamu ya chadema au cuf kuonesha mapungufu ya ccm na kuomba ridhaa ya watanzania kuongoza.


MWafrika wa kike

Kwanini CHADEMA Au CUF na iswe UDP ,DP ,TLP na NCCR-Mageuzi??hii ndiyo inayoenyesha Lengo lenu CHADEMA ni kutaka Madaraka tu ni siyo kututoa hapa tulipo.

Kama Manataka kushinda,Naomba muungane kama WApinzani na siyo kujibahgua kama hivi.Now i know why mlimfukuza CHACHA Wangwe
 
Suala la Pili ni kwamba CHADEMA kama wao wameshindwa kutafuta Wafadhili wa kuendesha chama sababu hakuna watu wabunifu ambao wanaweza kuandika Proposal nzuri labda waandikiwe na kina Baregu au Zitto ila wengi wao ni watu wanotawaliwa na Emotion.

The Truth is Upinzani wa kweli utapatikana mpaka pale CCM itakapogawanyika na kupatikana wapinzani wenye uwezo wa kuongozi siyo wanaotafuta Uongozi.

Gembe,

unazungumzia CHADEMA kukosa wafadhili, hivi "mfadhili" ni nani? Kwa maelezo ya Dr Slaa, viongozi wa juu wa CHADEMA wameamua kufadhili chama, sasa mfadhili gani mwingine wamekosa? au kwako wewe mfadhili mpaka awe yule mwenye asili ya "uarabu" au mwenye mkopo wa EPA?

Suala la kukosa wabunifu, Dr Slaa amezungumzia kuwa CHADEMA wamefanikiwa kuanzisha miradi sio ya kinadharia bali miradi kweli.

Swali langu kuhusu ubunifu: je kuna mradi gani ulioanzishwa na CCM (baada ya mfumo wa vyama vingi) ili tuwaone wao ni wabunifu na watu makini? Na ili tuutolee mfano kwa vyama vingine. Na nikauliza vipi SUKITA?

Kwa ufupi nakubaliana na wewe kuwa CCM na serikali yake kwa ujumla sio wabunifu, na niwepesi kutafuta pesa kwa njia za mkatisho (shortcut)!
 
lengo la chama chochote cha siasa ni kushika hatamu za nchi. Kama chama cha siasa hakina lengo la kuongoza nchi basi hicho chama sio cha siasa.

Kwa sasa ccm wamefeli na ni zamu ya chadema au cuf kuonesha mapungufu ya ccm na kuomba ridhaa ya watanzania kuongoza.

Mrema akikusikia atajinyonga!!!
 
Back
Top Bottom