Nadhani hapa kuna hoja nzuri. Tusitake vyama vingine vifuate utaratibu wa CCM wa kujiendesha kwa kulipana mishahara. Siasa lazima iwe utumishi, na utumishi uwe wa watu kujiolea, siyo kuchuma. Kabla ya Mbowe na Dk. Slaa kuwa viongozi kwa nyadhifa walizonazo leo, utendaji wa wakati ule, chini ya Dk. Aman Kabourou, ulikuwa unalipana mishahara, na chama hakikukua mikoani.
Mbowe alipopiga vita hii tabia ya viongozi kula ruzuku kwa kujilipa mishahara, ilikuwa sababu ya kwanza ya Dk. Kabourou kutafuta mlango wa kutokea hasa baada ya Mbowe kuwa mwenyekiti. Sababu hizi hiiz za ulaji ndizo zilimuondoa Paul Kyara aliyekuwa mweka hazina na aliyeshirikiana kwa karibu na Dk. kabourou kutumbua ruzuku.
Sasa, kwa vyama visivyo na ruzuku kubwa, visivyoungwa na wafanyabiashara wengi (maana waliopo wanachangia CCM), kuna kosa gani kwa kina Mbowe na Ndesamburo kukichangia chama chao? Kuwataka wasichange pesa nyingi wakati wanazo ni mbinu nyingine ya kutaka kukidhoofisha chama hicho. Tuwatendee haki katika hili....Chadema hakina wahindi wa kukichangia, lakini hata CCM yenye Wahindi bado inategemea pesa za EPA! Shame!