Kwanini Baraza la Mawaziri lisivunjwe kwa kushindwa kumshauri Rais?

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,675
40,929
Kitendo cha Waziri wa Fedha kukiri kwamba akiba ya Taifa ya Fedha za kigeni ilichotwa na fedha kutumika kwa ujenzi wa Madarasa ni kiashiria cha dhahiri kukosekana fedha katika njia za kawaida (makusanyo ya mapato).

Foreign Reserve hutumika tu endapo kuna mkwamo wa kiuchumi na serikali huzitumia fedha hizo katika manunuzi ya bidhaa na gharama nyinginezo pindi inapobidi kufanyika hivyo.

Hivyo matumizi yake ni kwa dharura tu na SI VINGINEVYO.

Kuchota akiba inamaana kwamba hatuna fedha na tumeshindwa kukusanya mapato ipasavyo.

Kama tumeshaanza kuigusa akiba yetu haraka namna hii nini mustakabali wa Taifa hili kwa kuzingatia kwamba bado tunaendelea kukopa na bado kuna miradi mingi ya kimkakati ya kutekeleza.

Ni kwa namna gani tunaweza rejesha fedha tulizochukua katika akiba?

Je kuchota akiba ya Taifa was the only available solution??

Mimi naona kama vile kuna jambo ambalo tunafichwa kuhusiana na hali yetu ya kifedha ila sio siri tena maana hata huko mtaani kuna uhaba wa fedha za kigeni ukijaribu kununua unaambiwa hazipo , ila ukichange wanapokea.

Kwakua kuna mkwamo na Baraza la Mawaziri limeshindwa kumshauri Rais ili kuhakikisha ukali wa maisha unapungua.

Nashauri Baraza hili livunjwe.

Rais asiangalie majina aangalie matokeo ya hao wanaopewa majukumu.

Hii nchi ni yetu sote, kuendelea kubebena wakati tunaingia shimoni sio jambo sahihi.

Hapa ili tupone kuna watu inabidi waachie nafasi zao, wapishe wengine.
 
Nchi haiongozwi Kwa ushauri wa BARAZA la mawaziri pekee.

Mambo yamebadilika sana. Tunatakiwa kama Nchi tujitegemee, utegemezi utafika kikomo soon,

Vita ya Ukraine inaenda kuchukua sura mpya, Hali itakuwa mbaya zaidi, kama Si japaaan Kuna Nchi Fulani vita italipuka tena soon,

Matetemeko, njaa nk ndo muda wake kuanzia mwaka huu 2023 na kuendelea.

Tunatakiwa kama Nchi tupate kiongozi mwenye Vision, atusaidie kujitegemea Kwa kuzalisha mbolea yetu wenyewe tujiimarishe ktk KILIMO, maana imethibitika Nchi yetu backbone ni KILIMO.

Tunakoelekea tutakwama, mamlaka ziumize KICHWA tupate kiongozi mkuu atakayesaidia kukabiliana na yajayo.

Aaamen.
 
Nchi haiongozwi Kwa ushauri wa BARAZA la mawaziri pekee.

Mambo yamebadilika sana. Tunatakiwa kama Nchi tujitegemee, utegemezi utafika kikomo soon,

Vita ya Ukraine inaenda kuchukua sura mpya, Hali itakuwa mbaya zaidi, kama Si japaaan Kuna Nchi Fulani vita italipuka tena soon,

Matetemeko, njaa nk ndo muda wake kuanzia mwaka huu 2023 na kuendelea.

Tunatakiwa kama Nchi tupate kiongozi mwenye Vision, atusaidie kujitegemea Kwa kuzalisha mbolea yetu wenyewe tujiimarishe ktk KILIMO, maana imethibitika Nchi yetu backbone ni KILIMO.

Tunakoelekea tutakwama, mamlaka ziumize KICHWA tupate kiongozi mkuu atakayesaidia kukabiliana na yajayo.

Aaamen.
Kile ndio kikao cha juu kabisa cha nchi mkuu.

Sasa kama hawana mawazo chanya ndio mwanzo wa sisi kupotea maana ni watu walio karibu na Rais.

Sasa kama hawawezi kuja na solution za changamoto zetu wake pembeni tu.
 
Kile ndio kikao cha juu kabisa cha nchi mkuu.

Sasa kama hawana mawazo chanya ndio mwanzo wa sisi kupotea maana ni watu walio karibu na Rais.

Sasa kama hawawezi kuja na solution za changamoto zetu wake pembeni tu.
Ni Kweli lakini DEREVA ndo Huwa ana ramani yote juu ya DESTINATION ya safari.

Tatizo letu lipo hapo,

Tungekuwa serious, Isingewezekana Rais aende kukopa Trilions of money Halafu Zikaibwa wazi wazi na zisirudishwe na Bado tukasema tuna viongozi.
 
Dereva huwa hashauri na konda
Turejee kidogo majukumu ya Baraza la Mawaziri.

Ibara ya 54 (3) ya katiba ya nchi.

Screenshot_20230209-115918.png
 
Una uhakika gani Baraza ndilo lenye Shida na si huyo anayeliongoza............!
 
Turejee kidogo majukumu ya Baraza la Mawaziri.
Pia tujiulizi kwann DEREVA hadhibiti UPIGAJI unaotamalaki?

Wizi wa pesa za Umma ndo chanzo kikubwa Cha kutuzuia kukabiliana na kupambana na mttz ktk Nchi mf Kupanda Kwa gharama za chakula nk.
 
Kitendo cha Waziri wa Fedha kukiri kwamba akiba ya Taifa ya Fedha za kigeni ilichotwa na fedha kutumika kwa ujenzi wa Madarasa ni kiashiria cha dhahiri kukosekana fedha katika njia za kawaida (makusanyo ya mapato).

Foreign Reserve hutumika tu endapo kuna mkwamo wa kiuchumi na serikali huzitumia fedha hizo katika manunuzi ya bidhaa na gharama nyinginezo pindi inapobidi kufanyika hivyo.

Hivyo matumizi yake ni kwa dharura tu na SI VINGINEVYO.

Kuchota akiba inamaana kwamba hatuna fedha na tumeshindwa kukusanya mapato ipasavyo.

Kama tumeshaanza kuigusa akiba yetu haraka namna hii nini mustakabali wa Taifa hili kwa kuzingatia kwamba bado tunaendelea kukopa na bado kuna miradi mingi ya kimkakati ya kutekeleza.

Ni kwa namna gani tunaweza rejesha fedha tulizochukua katika akiba?

Je kuchota akiba ya Taifa was the only available solution??

Mimi naona kama vile kuna jambo ambalo tunafichwa kuhusiana na hali yetu ya kifedha ila sio siri tena maana hata huko mtaani kuna uhaba wa fedha za kigeni ukijaribu kununua unaambiwa hazipo , ila ukichange wanapokea.

Kwakua kuna mkwamo na Baraza la Mawaziri limeshindwa kumshauri Rais ili kuhakikisha ukali wa maisha unapungua.

Nashauri Baraza hili livunjwe.

Rais asiangalie majina aangalie matokeo ya hao wanaopewa majukumu.

Hii nchi ni yetu sote, kuendelea kubebena wakati tunaingia shimoni sio jambo sahihi.

Hapa ili tupone kuna watu inabidi waachie nafasi zao, wapishe wengine.
Raisi yupi unayemzumngumzia .kama ni saa 100 ngoja tu ni lale
 
Back
Top Bottom