Kwanini Askari hawalipi naulu kwenye usafiri?

Kwanini Askari hawalipi naulu kwenye usafiri?

Wakidaiwa huwa wanasema "subiri unapewa" wakifika mwisho wa safari wakiulizwa wanamtishia kondakta!! Hii nimeona sana!halafu afadhali Jwtz huwa wana adabu kidogo!polisi ndiyo hawana adabu hata kidogo,konda anauliza nauli polisi anamfokea eti "utakula makofi sasa hivi"
Polisi akikwambia utakula makofi mwambie sili makofi nimekula chakula home hapa nilipo nimeshiba, mkabe akupe nauli.
Usisahau mrejesho
 
Aisee huo upumbavu sifanyi nilipe ili iweje?
Wewe konda Njoo nishushe km unaweza
 
Kwanza niweke wazi mimi sio Askari wa Jeshi lolote lile..

Ila kuna hii tabia ya Askari wengi hasa JWTZ kutolipa nauli katika magari mbalimbali ya usafirishaji..

Nimeona wamefikia hatua sasa mpaka safari ya km hadi 100 mtu mzima halipi nauli. Unakuta askari anatoka Kimara hadi KIBAHA maili moja na Sare zake afu hataki kulipa nauli..

Naomba kuwasilisha....
Katika yote unakumbana nayo kila siku hilo ndio lililokukera?
 
Pamoja na yote waliyonayo

Kazi wanayoifanya ya kuhakikisha amani ipo muda wote sio ndogo

Mshahara wengi wapatao ni kidogo hauwatoshi mahitaji yao ya kila siku

Kwa hili acheni wasaidiwe kuwapunguzia ukali wa maisha japo 400 inaweza onekana ndogo ila kwao ina maana kubwa sana
Waalimu waseme nini mkuu?
 
Mkuu huu mjadala ulishaongelewa sana humu pamoja na kwenye mkutano mkuu wa wamiliki wa vyombo vya usafirishaji Dsm.

Majibu yaliishawekwa wazi, kwamba askari wa kada yoyote Dsm atapanda bure akiwa amevaa kikazi, isipokuwa akiwa kwenye nguo za nyumbani atatozwa, mbona utaratibu huo upo tangu enzi za Mwinyi?

Hoja hii imekuwa ikifukuta kama volcano. Inaripuka na kusinyaa na maisha yanaendelea.
Hoja hii hata ingelifikishwa kwa Magufuli, utapata jibu 'simple' sana na utashindwa kuamini masikio yako.

Wenzetu hao wana sacrifice sana maisa yao kwa ajili yetu sisi raia.
Wana magari yao kweli, lakini kwa mazingira ya Dar ni vigumu kuwakidhi.
Acha tu wapande bure, maana hakuna namna.
Upuuzi mtupu!! Walimu wanafanya kazi ngumu na nzito kila siku asubuhi na mchana lakini hawajawahi kupata hii "favor" ya kisiasa!! Ndio shida ya majeshi ya kisiasa siasa haya, kila kitu kinaendeshwa kisaniii kwa malengo ya kisiasa!
 
Akipanda gari yako we mdai tu akikataa mpige kabali au mkabe kwenye uniform yake mpeleke kituo cha polisi.

Usisahau kuleta mrejesho jamvini.
Huku ni kukosa busara! Vijana wa watu wanahangaika wapate chakula halafu wanakuja watu na ubabe wa kishamba hawataki kutoa nauli kwa sababu gani?
 
Upuuzi mtupu!! Walimu wanafanya kazi ngumu na nzito kila siku asubuhi na mchana lakini hawajawahi kupata hii "favor" ya kisiasa!! Ndio shida ya majeshi ya kisiasa siasa haya, kila kitu kinaendeshwa kisaniii kwa malengo ya kisiasa!
Mkuu tusitofautiane sana kwa sababu mada inayoongelewa hapa ni kwa 'base' ya Dar es salaam tu, ambapo hata walimu mh. Mkuu wa mkoa aliweka utaratibu wapande bure.

Nje ya Dsm askari ama kada yoyote ya mfanyakazi, wanalipia nauli kwa usafiri wa aina yoyote.
 
Mkuu tusitofautiane sana kwa sababu mada inayoongelewa hapa ni kwa 'base' ya Dar es salaam tu, ambapo hata walimu mh. Mkuu wa mkoa aliweka utaratibu wapande bure.

Nje ya Dsm askari ama kada yoyote ya mfanyakazi, wanalipia nauli kwa usafiri wa aina yoyote.
Sawa. Lakini kwanini wasilipe nauli? na kwanini iwe Dar es salaam pekee? Mantiki ni ipi hasa? Kuna watu wanaofanya kazi za suluba kama walimu wa nchi hii? madaktari? mbona hatukuwahi kusikia wakipewa huu upendeleo wa kisiasa!!?

Na ikumbukwe usafiri wa daladala ni ajira kwa vijana wanaohangaika usiku na mchana kupata chochote! Senti yoyote hata moja ndio chakula chao! Huko jeshini wanapewa marupurupu na mapesa kibao kwanini wasilipe mia nne tu!!?
 
Wajeda wanapenda sana kulipa nauli tatizo konda hawataki kudai nauli hapo ndio tatizo lilipo
 
Pamoja na yote waliyonayo

Kazi wanayoifanya ya kuhakikisha amani ipo muda wote sio ndogo

Mshahara wengi wapatao ni kidogo hauwatoshi mahitaji yao ya kila siku

Kwa hili acheni wasaidiwe kuwapunguzia ukali wa maisha japo 400 inaweza onekana ndogo ila kwao ina maana kubwa sana
Mwanajeshi na Mwalimu nani ana msoto wa maisha? Kumbuka pia hao huwana magari yanayowabeba pia.
 
Anzeni kwanza mjengoni kwa nini bajeti yao inapitishwa tu bila kupingwa ndio mje huku
 
kipindi wao wanapambana kuhakikisha wanapata kazi wewe ulikuwa wapi....? ata wewe ungekuwa kama wao usingelipa nauli...au wewe ni konda....?
 
Back
Top Bottom