Kwanini Askari hawalipi naulu kwenye usafiri?

Kwanini Askari hawalipi naulu kwenye usafiri?

Hawalipi kutokana na tamko la aliyekuwa Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi. Ndg. Augustine Liyatonga Mrema na kwa makubaliano ya pamoja kati yake na wamiliki wa mabasi (daradara) wakati huo. Kwamba Askari akiwa amevaa sare wakati wowote aidha wa kwenda au kurudi kazini hatolipa NAULI full stop
 
Hawalipi kutokana na tamko la aliyekuwa Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi. Ndg. Augustine Liyatonga Mrema na kwa makubaliano ya pamoja kati yake na wamiliki wa mabasi (daradara) wakati huo. Kwamba Askari akiwa amevaa sare wakati wowote aidha wa kwenda au kurudi kazini hatolipa NAULI full stop
Ahsante sana.. ila kumb JWTZ ni wizara ya ulinzi na si mambo ya ndani
 
Nadhani kazi yao ndiyo sababu yakutolipa nauli na pia wengi hasa JWTZ huwa wanapanda malori au magari ya watu binafsi.

Naunga mkono kutokulipa,hawa jamaa ile kazi si mchezo anaweza kuwa amepumzika na mkewe ndani,ghafla wakaitwa haraka na kuondoka hata week nzima.

Nimewahi kuishi kikosi fulani,ile kazi ningumu sana
 
Hawalipi kutokana na tamko la aliyekuwa Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi. Ndg. Augustine Liyatonga Mrema na kwa makubaliano ya pamoja kati yake na wamiliki wa mabasi (daradara) wakati huo. Kwamba Askari akiwa amevaa sare wakati wowote aidha wa kwenda au kurudi kazini hatolipa NAULI full stop
Ebwana hii habari niliwahi kuipata hivyo hivyo. Mwanzoni mwa miaka ya 90 chama cha wamiliki wa daladala walikubaliana wawape offer askari polisi wasilipe nauli.

Ilikua ni kwa polisi hawa usalama a raia na mali zetu. Majeshi mengine yote wameiga tu na ubabe wao. Yaani wanajeshi, Magereza hawakuwa kwenye mpango huo.

Kwa hiyo jambo hilo sio sheria ni makubaliano ya zamani hata hivyo imezoelela tu hivyo
 
Acha tu wasilipe, ila wawe wanapanda mmoja mmoja sio kujaa gari moja hasa wale wa pale Lugalo, utadhani wanashukia Bunju tu kumbe mpaka Bagamoyo,
 
Ebwana hii habari niliwahi kuipata hivyo hivyo. Mwanzoni mwa miaka ya 90 chama cha wamiliki wa daladala walikubaliana wawape offer askari polisi wasilipe nauli.

Ilikua ni kwa polisi hawa usalama a raia na mali zetu. Majeshi mengine yote wameiga tu na ubabe wao. Yaani wanajeshi, Magereza hawakuwa kwenye mpango huo.

Kwa hiyo jambo hilo sio sheria ni makubaliano ya zamani hata hivyo imezoelela tu hivyo
Ni kweli hoja ilianzia kwa Askari Polisi na ndo walikuwa walengwa, ila kwasababu tamko lilisema Askari kwahiyo likawahusu wote. Tamko halikusema askari Polisi tu.
 
Mkuu huu mjadala ulishaongelewa sana humu pamoja na kwenye mkutano mkuu wa wamiliki wa vyombo vya usafirishaji Dsm.

Majibu yaliishawekwa wazi, kwamba askari wa kada yoyote Dsm atapanda bure akiwa amevaa kikazi, isipokuwa akiwa kwenye nguo za nyumbani atatozwa, mbona utaratibu huo upo tangu enzi za Mwinyi?

Hoja hii imekuwa ikifukuta kama volcano. Inaripuka na kusinyaa na maisha yanaendelea.
Hoja hii hata ingelifikishwa kwa Magufuli, utapata jibu 'simple' sana na utashindwa kuamini masikio yako.

Wenzetu hao wana sacrifice sana maisa yao kwa ajili yetu sisi raia.
Wana magari yao kweli, lakini kwa mazingira ya Dar ni vigumu kuwakidhi.
Acha tu wapande bure, maana hakuna namna.
 
Labda daladala, kama huamini mwambie askari akapande Dar Lux kwenda mwanza uone kama kuna cha bure
 
Kwa nini hamuwadai nauli kama abiria wengine?!
Wakidaiwa huwa wanasema "subiri unapewa" wakifika mwisho wa safari wakiulizwa wanamtishia kondakta!! Hii nimeona sana!halafu afadhali Jwtz huwa wana adabu kidogo!polisi ndiyo hawana adabu hata kidogo,konda anauliza nauli polisi anamfokea eti "utakula makofi sasa hivi"
 
Nachoelewa askar wakizid zaid ya wawili hyo no lazima kulipa, lkn mmoja sio tatizo!
Huyo mmoja kwa nini asilipe? Yeye ni mfanyakazi tu! Mbona Doctors wanalipa na ndiyo wa maana kielimu na kiumuhimu kuliko hata hao askari? Mbona wanafunzi wasio na kipato chochote wanalipishwa nauli?hawa askari wanaishi bure na bado wanawanyonya wanyonge!! Hawa ni makupe tu!
 
Kwanza niweke wazi mimi sio Askari wa Jeshi lolote lile..

Ila kuna hii tabia ya Askari wengi hasa JWTZ kutolipa nauli katika magari mbalimbali ya usafirishaji..

Nimeona wamefikia hatua sasa mpaka safari ya km hadi 100 mtu mzima halipi nauli. Unakuta askari anatoka Kimara hadi KIBAHA maili moja na Sare zake afu hataki kulipa nauli..

Naomba kuwasilisha....
Akipanda gari yako we mdai tu akikataa mpige kabali au mkabe kwenye uniform yake mpeleke kituo cha polisi.

Usisahau kuleta mrejesho jamvini.
 
Huyo mmoja kwa nini asilipe? Yeye ni mfanyakazi tu! Mbona Doctors wanalipa na ndiyo wa maana kielimu na kiumuhimu kuliko hata hao askari? Mbona wanafunzi wasio na kipato chochote wanalipishwa nauli?hawa askari wanaishi bure na bado wanawanyonya wanyonge!! Hawa ni makupe tu!
Wadai nauli mkuu.
Unakwama wapi??
 
Hawajapewa elimu kwamba wanapaswa kulipa nauli lkn kukiwa na kazi maalumu raia tunapaswa kuwasaidia kwani kazi zao ni masaa 24 na siyo kwa safari binafsi.
 
Back
Top Bottom