Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,097
- 43,308
Sijui kuna tatizo gani katika Mkoa huo. Imekuwa ni kawaida kiongozi akienda ni lazima alalamikie matatizo ya matumizi ya fedha za Umma. Ameenda Rais, ameenda Waziri Mkuu, ameenda Jafo na hivi sasa kapita Katibu Mkuu wa CCM.
Wote kwa namna tofauti na kuhusiana na mambo tofauti tofauti wanalalamikia au kuibua matumizi mabaya ya fedha au usimamizi mbaya wa fedha. Kuna watu hadi waliondolewa lakini inaonekana kama Moro - Mji Kasoro Bahari - unaonekana kuwashinda au kushindwa!
Kuna tatizo gani Morogoro? Labda hata mikoa mingine hali iko hivyo lakini kutajwa kwa Morogoro mara kwa mara ni lazima kuwafanye watu wajiulize "kunani'?
Wote kwa namna tofauti na kuhusiana na mambo tofauti tofauti wanalalamikia au kuibua matumizi mabaya ya fedha au usimamizi mbaya wa fedha. Kuna watu hadi waliondolewa lakini inaonekana kama Moro - Mji Kasoro Bahari - unaonekana kuwashinda au kushindwa!
Kuna tatizo gani Morogoro? Labda hata mikoa mingine hali iko hivyo lakini kutajwa kwa Morogoro mara kwa mara ni lazima kuwafanye watu wajiulize "kunani'?