IsangulaKG
JF-Expert Member
- Oct 14, 2010
- 706
- 386
Umewahi kujiuliza kwa nini nchi za Ulaya zinaendelea kutajirika kila kukicha huku za kwetu zikiendelea Kumasikinika?
Umewahi kujiuliza kwa nini wakati Life Expectancy kwao Ikiongezeka kwetu ndiyo inapungua zaidi?
Umewahi kujiuliza kwa nini idadi ya watu kwao inapungua wakati kwetu ndo kwanza tunazaliana?
Umewahi kujiuliza kwa nini 'vijiji' vyao vinakua kwa kasi wakati vya kwetu ndo Vinachakaa?
Kwa miaka mingi sana nimekuwa na fikra tofauti na wengine kuhusu umasikini na hali duni ya maisha na afya katika nchi zetu za bara la tatu. Japo hadi sasa bado ni mwanafunzi wa HUMAN MIND lakini maarifa ambayo nimejikusanyia hadi sasa yananitosha kuandika makala hii.
Acha tuanze kutafakari hivi:
Kukata tamaa kwa Haraka
Kwa muda mrefu nimesoma na kufanya kazi na wajapan. Kimsingi wengi wao nilikuwa nawazidi katika ufaulu na hata katika kufikiria mambo kwa haraka. Baada ya kupitia baadhi ya vitabu vya historia ya ujapan na life style yao , nimetambua kuwa hawa jamaa wanaendelea kwa kuwa wako PERSISTENT, hapa namaanisha si watu wa kukata tamaa kirahisi.
Mifumo ya familia za kijapan na maisha yao toka utotoni yanamjenga mtoto wa kijapani kutokukubali kushindwa hasa kunapokuwa na imani kuwa lile jambo analolifanya lina manufaa kwake na kwa taifa kwa ujumla, hata kama imani hiyo ni ndogo. Wajapan na rafiki zao wachina, kwa mfano wako radhi kufanya kazi hadi usiku wa manane pasipo kulalamika kwa sababu hali hiyo imejengeka toka utotoni, ni kama mila kwao, kuwajibika!
Nakumbuka wakati wanajenga daraja la mto Mara pale 'Kirumi' inaaminika walikuwa wakijenga usiku wa manane na wenyeji wa maeneo yale wakaishia kufikiria kuwa pengine ni washirikina. Kwa nchi zetu mfano Tanzania sisi ni wepesi wa kukata tamaa hasa unapoona kuwa manufaa ya jambo unalolifanya yako mbali. Mara nyingi tunahangaika na manufaa ya muda mfupi ambayo siyo sustainable badala ya kuhangaika na manufaa yanayochelewa kuja lakini ni sustainable.
Tunataka tuanze biashara leo kesho tupate faida, Tupande leo kesho tuvune. Tunataka tuajiriwe leo kesho tupate nyumba na gari na pale unapoona kuna kuchelewa kiasi basi unakata tamaa na kuanza kutafuta shortcuts. Hali hii imetuathiri sana kwani shortcut hizi tunazotafuta ndizo zinazozaa roho za Rushwa na Ufisadi. Matokeo yake yako dhahiri.
Fikra Finyu
Miaka ya Nyuma kidogo nchi kama Marekani ilipoteza watu wengi sana kutokana na Vita ya pili ya dunia. Uingereza ilipoteza watu wengi sana kutokana na magonjwa kama tauni, kipindupindu n.k, Spanish flu miaka ya karne iliyopita ilifyeka idadi kubwa ya watu huko Ulaya. Mbali na matukio haya makubwa ya kiafya, bado nchi za Ulaya zinaongoza kwa kuwa na huduma nzuri za afya...kwa nini? Kwa sasa wao manonjwa yao yamehama toka kwenye 'Infectious disease' kwenda kwenye 'Chronic Disease' na 'Uzee'. Kitaalamu Chronic disease kama Hypertension na magonjwa ya moyo yanatokana na lifestyle hasa kwa watu wenye uchumi mkubwa. Life expectancy yao imeongezeka na wazee wanaishi umri mrefu kutokana na kuboreka kwa huduma ya Afya. Wakati nchi zetu 'infectious disease' kama Ukimwi, Malaria n.k. ndo 'store' yake.
Mfano mwingine Marekani, ina disparity kubwa sana kwa weusi na weupe. Weusi wamewekewa misingi mingi sana ya kuboresha afya zao, wamepewa nafasi nyingi sana za kimasomo , lakini je wanazitumia? Hadi leo hii bado weusi wa marekani wana viwango vibovu vya afya Ukilinganisha na weupe japo wana nafasi kubwa ya Kuboresha afya zao japo kuwa hali zao bado haziwezi kulinganishwa na nchi zetu hizi zisizo makao ya 'malaika'. Baada ya kuishi Marekani kwa Muda niliweza kuona Kuwa tatizo kubwa linalotusumbu sisi ni fikra finyu. Tunapenda kila kitu tufanyiwe na tufurahie mafanikio. In short tunapenda kufurahia mafanikio ambayo hatujachangia kuyatafuta.
Ni mara ngapi umepanda katika gari na kufikiria lilivyotengenezwa na kufikiria unawezaje kutumia rasilimali zilizo katika mazingira yako ukatengeneza lenye matairi matatu tofauti na hilo ulilopanda? WE LACK CREATIVE THINKING! Tunafikiri kama maboya tu! Unakula chakula pasipo kujiuliza kimepikwaje, Unavaa nguo pasipo kujiuliza imetengenezwaje. Kila jambo jipya tunaloliona 'WE IGNORE'
Unatumia Kijiko pasipo kujiuliza Kimetengenezwaje. Mfano mzuri ni yule Mwanasayansi aliyegundua law of gravitation. Alikuwa kanisani akaona taa inayoning'inia darini inacheza wakati hakuna upepo, akatoka nje akakaa chini ya mwembe, embe likamponda kichwani wakati hakuna upepo., hapo akaanza mfululizo wa fikra mpaka akagundua law of gravity.
Au mfano wa yule daktari aliyegundua kile kifaa cha Madaktari 'Stethoscope' Alikuja mgonjwa mnene sana na kwa kuwa wakati huo walikuwa wanasikiliza mapigo ya myo kwa kuweka sikio kifuani kwa mgonjwa, akapata wazo kukunja karatasi ili kutengeneza kama 'tube' iliyomwezesha kusikia mapigo ya moyo wa yule mgonjwa mnene. Je sisi wataalamu wetu wanapokosa vifaa hospitalini wanakuwa na akili ya kufikiria njia mbadala au ndo hukumu ya kifo inatolewa kwa mgonjwa hapo hapo?
Ni Mambo au matukio mangapi yanayotutokea na kushindwa kuyafikiria kisayansi na kuwa wagunduzi? Bahati mbaya kabisa twatanguliza ushirikina au kwa anayesali saana huishia kusema ni mpango wa Mungu! Ili tuwe ni wagunduzi twahitaji kuhoji kila kitu kinachotutokea maishani.
Mfumo huu wa kutokuhoji kila kitu umetufanya tuwe wana mapokeo. Mfano hatuwezi hata kuhoji kwa nini hospitalini hakuna dawa, kwa nini serikali haitekelezi huduma muhimu kwa wananchi badala yake tunaishi kwa kuwa tunaishi.
Moja wapo ya kitu kinachochangia kuboresha afya katika nchi za wenzetu ni kitu kinachoitwa 'Service Demand" Kwetu huku twaishia kulalamika tu kuwa hakuna vifaa na dawa hospitalini pasipo kudai kwa nguvu zote. Kwa mfano mtu mwenye Medicaid Insurance aliyopewa na serikali kule Marekani ana haki ya kuishitaki serikali au kituo cha afya kama hakupata huduma fulani ambayo ni haki yake. Ni mara ngapi ndugu zetu wanafariki mahospitalini kwa uzembe au kukosa huduma za msingi na tunaishia kusema 'ni mpango wa Mungu? Ni mara ngapi watoto wetu wanakosa chanjo kwa kuwa dawa zimeisha na tunajiendea nyumbani kwa Amani?
Ili afya zetu ziimarike tunahitaji kudai Huduma ambazo ni Haki yetu. Kwa nini ukose umeme na Unalipa Kodi? Kwa nini ukose dawa Hospitali na Umekatwa zaidi ya Asilimia 20 ya Mshahara? Mambo haya yanajitokeza pia hasa katika mifuko yetu ya Bima, una Bima ya afya, unaenda hospitalini hakuna dawa, kwa nini usidai na kwenda mahakamani? Kwa nini wanakijiji wanakubali shule isiyo na Madawati? Kwa nini wasidai?Kwa nini? Kwa nini?
Tuna matatizo katika fikra, hatujajikomboa, si wagunduzi, twaishi kwa kudra za mwenyezi Mungu na mambo ya 'hewala'
Moyo hafifu wa kujituma
Ni mara ngapi umeenda dukani ukakuta limefunguliwa na Muuzaji hayumo? This how we are! We are not serous in whatever we are doing! Mfanyakazi serikali hakai ofisini, Mwendesha mitambo kiwandani anatega, Daktari hospitalini hayupo, Mwalimu shuleni hayupo, Mkulima hayuko shambani, Mwanafunzi hayuko Darasani. Hebu tembelea sehemu za wengine kama Taiwan, Engineer yuko barabarani au juu ya Magorofa anajenga kila siku. Daktari yuko hospitalini anatibu kila siku, Mfanya biashara yupo katika eneo lake kila siku...Kila mtu anawajibika, Kila mtu anajituma ,kwa nini sisi pia tusijitume?
Mtu pekee atakewasaidia watanzania kujiuondoa katika maisha ya sasa ni yule atakayegundua jinsi ya kuwakomboa kifikra. Kuwabadili fikra za uzembe, kutokuwajibika, kutokuhoji ili kuwajengea fikra madhubuti. Tofauti na hapo hatutapata maendeleo kamwe!
Pengine kizazi hiki kimeshindwa, basi naamini ni vema angalau tutimize wajibu wa kuwekeza katika wanetu:
Anza kubadili maisha yako sasa!
Umewahi kujiuliza kwa nini wakati Life Expectancy kwao Ikiongezeka kwetu ndiyo inapungua zaidi?
Umewahi kujiuliza kwa nini idadi ya watu kwao inapungua wakati kwetu ndo kwanza tunazaliana?
Umewahi kujiuliza kwa nini 'vijiji' vyao vinakua kwa kasi wakati vya kwetu ndo Vinachakaa?
Kwa miaka mingi sana nimekuwa na fikra tofauti na wengine kuhusu umasikini na hali duni ya maisha na afya katika nchi zetu za bara la tatu. Japo hadi sasa bado ni mwanafunzi wa HUMAN MIND lakini maarifa ambayo nimejikusanyia hadi sasa yananitosha kuandika makala hii.
Acha tuanze kutafakari hivi:
Kukata tamaa kwa Haraka
Kwa muda mrefu nimesoma na kufanya kazi na wajapan. Kimsingi wengi wao nilikuwa nawazidi katika ufaulu na hata katika kufikiria mambo kwa haraka. Baada ya kupitia baadhi ya vitabu vya historia ya ujapan na life style yao , nimetambua kuwa hawa jamaa wanaendelea kwa kuwa wako PERSISTENT, hapa namaanisha si watu wa kukata tamaa kirahisi.
Mifumo ya familia za kijapan na maisha yao toka utotoni yanamjenga mtoto wa kijapani kutokukubali kushindwa hasa kunapokuwa na imani kuwa lile jambo analolifanya lina manufaa kwake na kwa taifa kwa ujumla, hata kama imani hiyo ni ndogo. Wajapan na rafiki zao wachina, kwa mfano wako radhi kufanya kazi hadi usiku wa manane pasipo kulalamika kwa sababu hali hiyo imejengeka toka utotoni, ni kama mila kwao, kuwajibika!
Nakumbuka wakati wanajenga daraja la mto Mara pale 'Kirumi' inaaminika walikuwa wakijenga usiku wa manane na wenyeji wa maeneo yale wakaishia kufikiria kuwa pengine ni washirikina. Kwa nchi zetu mfano Tanzania sisi ni wepesi wa kukata tamaa hasa unapoona kuwa manufaa ya jambo unalolifanya yako mbali. Mara nyingi tunahangaika na manufaa ya muda mfupi ambayo siyo sustainable badala ya kuhangaika na manufaa yanayochelewa kuja lakini ni sustainable.
Tunataka tuanze biashara leo kesho tupate faida, Tupande leo kesho tuvune. Tunataka tuajiriwe leo kesho tupate nyumba na gari na pale unapoona kuna kuchelewa kiasi basi unakata tamaa na kuanza kutafuta shortcuts. Hali hii imetuathiri sana kwani shortcut hizi tunazotafuta ndizo zinazozaa roho za Rushwa na Ufisadi. Matokeo yake yako dhahiri.
Fikra Finyu
Miaka ya Nyuma kidogo nchi kama Marekani ilipoteza watu wengi sana kutokana na Vita ya pili ya dunia. Uingereza ilipoteza watu wengi sana kutokana na magonjwa kama tauni, kipindupindu n.k, Spanish flu miaka ya karne iliyopita ilifyeka idadi kubwa ya watu huko Ulaya. Mbali na matukio haya makubwa ya kiafya, bado nchi za Ulaya zinaongoza kwa kuwa na huduma nzuri za afya...kwa nini? Kwa sasa wao manonjwa yao yamehama toka kwenye 'Infectious disease' kwenda kwenye 'Chronic Disease' na 'Uzee'. Kitaalamu Chronic disease kama Hypertension na magonjwa ya moyo yanatokana na lifestyle hasa kwa watu wenye uchumi mkubwa. Life expectancy yao imeongezeka na wazee wanaishi umri mrefu kutokana na kuboreka kwa huduma ya Afya. Wakati nchi zetu 'infectious disease' kama Ukimwi, Malaria n.k. ndo 'store' yake.
Mfano mwingine Marekani, ina disparity kubwa sana kwa weusi na weupe. Weusi wamewekewa misingi mingi sana ya kuboresha afya zao, wamepewa nafasi nyingi sana za kimasomo , lakini je wanazitumia? Hadi leo hii bado weusi wa marekani wana viwango vibovu vya afya Ukilinganisha na weupe japo wana nafasi kubwa ya Kuboresha afya zao japo kuwa hali zao bado haziwezi kulinganishwa na nchi zetu hizi zisizo makao ya 'malaika'. Baada ya kuishi Marekani kwa Muda niliweza kuona Kuwa tatizo kubwa linalotusumbu sisi ni fikra finyu. Tunapenda kila kitu tufanyiwe na tufurahie mafanikio. In short tunapenda kufurahia mafanikio ambayo hatujachangia kuyatafuta.
Ni mara ngapi umepanda katika gari na kufikiria lilivyotengenezwa na kufikiria unawezaje kutumia rasilimali zilizo katika mazingira yako ukatengeneza lenye matairi matatu tofauti na hilo ulilopanda? WE LACK CREATIVE THINKING! Tunafikiri kama maboya tu! Unakula chakula pasipo kujiuliza kimepikwaje, Unavaa nguo pasipo kujiuliza imetengenezwaje. Kila jambo jipya tunaloliona 'WE IGNORE'
Unatumia Kijiko pasipo kujiuliza Kimetengenezwaje. Mfano mzuri ni yule Mwanasayansi aliyegundua law of gravitation. Alikuwa kanisani akaona taa inayoning'inia darini inacheza wakati hakuna upepo, akatoka nje akakaa chini ya mwembe, embe likamponda kichwani wakati hakuna upepo., hapo akaanza mfululizo wa fikra mpaka akagundua law of gravity.
Au mfano wa yule daktari aliyegundua kile kifaa cha Madaktari 'Stethoscope' Alikuja mgonjwa mnene sana na kwa kuwa wakati huo walikuwa wanasikiliza mapigo ya myo kwa kuweka sikio kifuani kwa mgonjwa, akapata wazo kukunja karatasi ili kutengeneza kama 'tube' iliyomwezesha kusikia mapigo ya moyo wa yule mgonjwa mnene. Je sisi wataalamu wetu wanapokosa vifaa hospitalini wanakuwa na akili ya kufikiria njia mbadala au ndo hukumu ya kifo inatolewa kwa mgonjwa hapo hapo?
Ni Mambo au matukio mangapi yanayotutokea na kushindwa kuyafikiria kisayansi na kuwa wagunduzi? Bahati mbaya kabisa twatanguliza ushirikina au kwa anayesali saana huishia kusema ni mpango wa Mungu! Ili tuwe ni wagunduzi twahitaji kuhoji kila kitu kinachotutokea maishani.
Mfumo huu wa kutokuhoji kila kitu umetufanya tuwe wana mapokeo. Mfano hatuwezi hata kuhoji kwa nini hospitalini hakuna dawa, kwa nini serikali haitekelezi huduma muhimu kwa wananchi badala yake tunaishi kwa kuwa tunaishi.
Moja wapo ya kitu kinachochangia kuboresha afya katika nchi za wenzetu ni kitu kinachoitwa 'Service Demand" Kwetu huku twaishia kulalamika tu kuwa hakuna vifaa na dawa hospitalini pasipo kudai kwa nguvu zote. Kwa mfano mtu mwenye Medicaid Insurance aliyopewa na serikali kule Marekani ana haki ya kuishitaki serikali au kituo cha afya kama hakupata huduma fulani ambayo ni haki yake. Ni mara ngapi ndugu zetu wanafariki mahospitalini kwa uzembe au kukosa huduma za msingi na tunaishia kusema 'ni mpango wa Mungu? Ni mara ngapi watoto wetu wanakosa chanjo kwa kuwa dawa zimeisha na tunajiendea nyumbani kwa Amani?
Ili afya zetu ziimarike tunahitaji kudai Huduma ambazo ni Haki yetu. Kwa nini ukose umeme na Unalipa Kodi? Kwa nini ukose dawa Hospitali na Umekatwa zaidi ya Asilimia 20 ya Mshahara? Mambo haya yanajitokeza pia hasa katika mifuko yetu ya Bima, una Bima ya afya, unaenda hospitalini hakuna dawa, kwa nini usidai na kwenda mahakamani? Kwa nini wanakijiji wanakubali shule isiyo na Madawati? Kwa nini wasidai?Kwa nini? Kwa nini?
Tuna matatizo katika fikra, hatujajikomboa, si wagunduzi, twaishi kwa kudra za mwenyezi Mungu na mambo ya 'hewala'
Moyo hafifu wa kujituma
Ni mara ngapi umeenda dukani ukakuta limefunguliwa na Muuzaji hayumo? This how we are! We are not serous in whatever we are doing! Mfanyakazi serikali hakai ofisini, Mwendesha mitambo kiwandani anatega, Daktari hospitalini hayupo, Mwalimu shuleni hayupo, Mkulima hayuko shambani, Mwanafunzi hayuko Darasani. Hebu tembelea sehemu za wengine kama Taiwan, Engineer yuko barabarani au juu ya Magorofa anajenga kila siku. Daktari yuko hospitalini anatibu kila siku, Mfanya biashara yupo katika eneo lake kila siku...Kila mtu anawajibika, Kila mtu anajituma ,kwa nini sisi pia tusijitume?
Mtu pekee atakewasaidia watanzania kujiuondoa katika maisha ya sasa ni yule atakayegundua jinsi ya kuwakomboa kifikra. Kuwabadili fikra za uzembe, kutokuwajibika, kutokuhoji ili kuwajengea fikra madhubuti. Tofauti na hapo hatutapata maendeleo kamwe!
Pengine kizazi hiki kimeshindwa, basi naamini ni vema angalau tutimize wajibu wa kuwekeza katika wanetu:
- Tuhakikishe Mimba za kuwazaa zinapatikana kwa haki, wapate malezi yanayowajenga fikra (siyo kutegemea tuisheni kufaulu)
- Tuwatengenezee mifumo ya elimu 'competitive' inayowafundisha kufikiri siyo 'kulishwa' kila kitu. Tuwe na waalimu wanaochochea ufikiri siyo wanaochochea 'ukariri'
- Tuwe na jamii inayowajibika kila mtu na nafasi yake , siyo jamii inayotafuta shortcuts na mafanikio ya haraka. Tukiwekeza katika mafanikio ya muda mrefu, tunaongelea mafanikio ya wanetu, kizazi kijacho...
- Serikali ianze kuwekeza katika miradi mikubwa si kama sasa ambapo hakuna Miradi yoyote mikubwa, japo itachukua muda mrefu lakini kizazi kijacho kitafaidi..
- Ili kufanikisha haya naamini tunahitaji kukubali kuwa TUMESHINDWA ili tufumue mifumo yetu ya KISIASA, KIUCHUMI, KIELIMU, KIAFYA isukwe upya si kwa ajili yetu (Tuna miaka michache ya Kuishi) bali kwa Kizazi kijacho.
- Na kadhalika na kadhalika
Anza kubadili maisha yako sasa!