Kwaheri utumishi wa Umma

Kwaheri utumishi wa Umma

Nguva Jike

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2018
Posts
1,285
Reaction score
1,853
Habari za jioni.

Nipo mbioni kukusanya vilago vyangu kwenda kijijini kulijenga Taifa. Nimefanya kazi Kwa miaka 14 sasa.

Nakumbuka msemo wa kisicho riziki hakiliki. Nimepambana vya kutosha kusalia kazini lakini mikono ya kupora riziki yangu imekuwa mingi na Kwa kasi kubwa.

Cha kushangaza wafanyakazi wenzangu nilikuwa nikiwaona wakifanya uhalifu na kuihujumu Serikali bila woga na nilikaa kimya kuogopa kuwaharibia kazi zao.

Lakini hao hao wamekuwa wakali na wepesi sana katika kufuatilia vikosa vidogo sana nilivyofanya hadi kufikia kuniharibia kwa mwajiri.

Moyo wangu bila kushawishiwa na nikiwa na akili timamu unaniambia nipumzike nifanye mengine kwa maana furaha yao mimi nikose kazi. Sina option inabidi niache tu nisiwe kero kwa wengine.

Kwaherini my friends.
 
Habari za jioni.

Nipo mbioni kukusanya vilago vyangu kwenda kijijini kulijenga Taifa. Nimefanya kazi Kwa miaka 14 sasa.
Kuna dada mmoja aliniharibia kazi mwaka 2017 ila nikafanikiwa kupata kwingine. Mpaka leo mwaka wa 5 ndani ya ndoa hana mtoto. Mkuu, karma is real. Kuna siku, baada ya miaka 3 hao hao watatafuta namba zako za simu kutaka kukuomba radhi. Mark my words.
 
Daaah, mkuu umeandika kwa uchungu mpaka na mimi najisikia vibaya. Watu wa aina hii wapo sana maeneo ya kazi. Mkuu, usiache kazi kutokana na kero za watu. Acha kazi kwa mapenzi yako.

Ukiacha kazi bila maandalizi, utakuja kujuta muda sio mrefu. Komaa na hao wanaokuwekea kauzibe huku ukiweka mazingira sawa ya kuacha kazi. Dunduliza mshahara wako halafu weka kitega uchumi, na ukisimamie ukiwa kazini.

Wazo la kufanya shughuli binafsi, bila kutegemea ajira ni zuri sana, kwani licha ya kujiajiri mwenyewe, utatengeneza pia ajira kwa watu wengine. Hivyo utaondokana na manyanyaso hayo unayopata sasa hivi, na kuwa na uhuru wa kufanya utakavyo wewe nwenyewe.

Lakini kwanza jipange mpaka uridhike na sio mtu mwingine akushinikize. Wewe uliomba kazi peke yako, nao waliomba kazi kivyao, kwahivyo hakuna mtu wa kukufanya uharakishe kuacha kazi. Pambana nao.
 
Umefukuzwa? Au unajifukuzisha? Sio lazima kila mtu akupende hapa duniani, just mind ur business, kama umeacha mwenyewe na sio kwamba unanyanyaswa na boss, huo sio uamuzi mzuri.
 
Habari za jioni.

Nipo mbioni kukusanya vilago vyangu kwenda kijijini kulijenga Taifa. Nimefanya kazi Kwa miaka 14 sasa.

Nakumbuka msemo wa kisicho riziki hakiliki. Nimwpambana vya kutosha kusalia kazini lakini mikono ya kupora riziki yangu imekuwa mingi na Kwa kasi kubwa.

Cha kushangaza wafanyakazi wenzangu nilikuwa nikiwaona wakifanya uhalifu na kuihujumu serikali bila woga na nilikaa kimya kuogopa kuwaharibia kazi zao.

Lakini hao hao wamekuwa wakali na wepesi sana katika kufuatilia vikosa vidogo sana nilivyofanya hadi kufikia kuniharibia Kwa mwajiri. Moyo wangu bila kushawishiwa na nikiwa na akili timamu unaniambiwa nipumzike nifanye mengine Kwa maana furaha yao mm nikose kazi. Sina option inabidi niache tu nisiwe kero kwa wengine.

Kwaherini my friends.

Ulifanya kosa kubwa sana kujifanya msabato kwenye kundi la mbwa mwitu. Ilikuwa uibe nao ama uwachome sio kukaa tu.
 
Kuna dada mmoja aliniharibia kazi mwaka 2017 mpaka leo mwaka wa 5 ndani ya ndoa hana mtoto. Mkuu, karma is real. Kuna siku, baada ya miaka 3 hao hao watatafuta namba zako za simu kutaka kukuomba radhi. Mark my words.
Katika kitu ambacho sitafanya ni kumharibia mtu kazi. Hiyo laana siitaki kabisa. Unafaidika na nini mtu akiachishwa kazi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom