Kwa wenye "WAKE" wanao drive

Kwa wenye "WAKE" wanao drive

Maisha yana changamoto nyingi sana. Changamoto sio kukosa mlo tuu, kila mtu ana changamoto yake.

Changamoto yangu mimi ni wife akitoka na gari. Huwa roho inaniuma hadi atakapokuwa amerudi nyumbani salama.

Maana huwa nakuwa standby kusubiri simu kuwa kapata majanga au laaah

Yani huo muda huwa nakuwa siwezi kufanya kitu, huwa nakuwa karibu na simu zangu mbili.

Na kama kaondoka na dada wa kazi na mtoto hapo ndo huwa nalia kabisa. Roho haitulii kabisa.

Nawaza kama watarud salama au laah hasa nikizingatia mabodaboda yalivyo mengi na uendeshaji wa ovyo, maroli makubwa na changamoto nyingine za barabarani.

Kumkoma nyani geradi
Huna haja ya kuwa na wasiwasi mkubwa mpaka ukose raha.

Cha msingi ni kuhakikisha yupo vzr barabarani na asipende ushindani muda wote akubali kushindwa atakuwa salama mengine tumuachie Mungu.

Mm woga wangu ni pale inapomuhusu safari ndefu lkn namuamini mno yuko vzr barabarani.
 
Yaani vijanaume vya siku hizi! Issue ya limke lako unataka kuharibu na wake za wengine . Bumbafuuu
 
Maisha yana changamoto nyingi sana. Changamoto sio kukosa mlo tu, kila mtu ana changamoto yake.

Changamoto yangu mimi ni wife akitoka na gari. Huwa roho inaniuma hadi atakapokuwa amerudi nyumbani salama.

Maana huwa nakuwa standby kusubiri simu kuwa kapata majanga au laaah

Yaani huo muda huwa nakuwa siwezi kufanya kitu, huwa nakuwa karibu na simu zangu mbili.

Na kama kaondoka na dada wa kazi na mtoto hapo ndo huwa nalia kabisa. Roho haitulii kabisa.

Nawaza kama watarudi salama au laah hasa nikizingatia mabodaboda yalivyo mengi na uendeshaji wa ovyo, malori makubwa na changamoto nyingine za barabarani.

Kumkoma nyani geradi
Asante kwa kutujuza una gari na mke wako anaweza ku drive
 
Hapo Kuna mawili.
1. Unadharau Sana kwa mkeo.
2. Hilo gari NI la mkopo na bado mkopo haujaisha.
 
Sasa kwanini unamruhusu achukue gari, acha kujambajamba
 
Nilishapokea na kusolve issue zake kama tatu. Sasa kwanini nisiwe na wasiwasi???

Kumkoma nyani geradi

Basi ndo maana!yuko rough?...mimi pia naambiwa niko very rough road!/ila huwa sielewj ..maana niko makini vibaya sana!ila wanawake wengi sana ni makini barabarani!..acha mawazo potofu!
 
Mkuu wewe ulimfundisha hiyo gari?

Au alisomea chuo ambacho hakina walimu wazuri?.


Baadhi ya wanawake ni madereva wazuri sana wakipata mtu sahihi wa kumfundisha gari huwa wako makini na ukijumlisha na uoga wao basi wanakuwa wako wapo na asilimia chache za kupata ajali za mara kwa mara.

Wengi mtalipinga hili ila ukweli sisi wanume kwa sababu ya kujiamini sana huwa tunapata ajali sababu ya kupuuza baadhi ya vitu.

Wapo wanawake wengi tu uoga wao wanakuwa wazito kufanya maamuzi sahihi barabarani na hii ndio utofauti na wanaume na baadhi ya madereva wanawake.


Ngumu sana ke kusababisha ajali!.
 
Nakua sina wasiwasi kwenye gari nikiwa naendeshwa na mwanamke kuliko mwanaume.. Hawa viumbe wapo makini barabarani sijawah kuona, ni mara chache sana mwanamke kupata ajali za kizembe.
Huwa ninakuwa na wasiwasi sana nikiendeshwa na mtu mwingine, yaani auamini udereva wangu tu
 
Back
Top Bottom