Gyeoul
JF-Expert Member
- Jan 28, 2015
- 3,758
- 5,364
Hongera kwa Mwaka mwengine Tena Babuu.KHERI ya KUTIMIZA miaka 3 NDANI ya JF (siku ya jana)
Teh teh teh nilitaka nijaribu kuandika kwa kiingilishi lakini nimeshindwa, naogopa wazee wa ngeli wasije kunizodoa asubuhi yote hii wakanifanya nikose hamu ya kukandamiza bakuli langu la UROJO kama meok goo anapokosa bakuli la wali na supu ya mende kwa ufadhili wa hela ya European Union.
ningelikuwa ni mtenda dhambi kama ningelishindwa kuandika ujumbe huu wa shukurani kupitia thread hii ambayo nusu ya comment zangu nimeziandika humu ndani (comment 1298)
huwezi amini nakumbuka ni kama juzi tu najaza fomu ya kujiunga na JF mida ya jioni, baadae naandika ujumbe wangu wa kwanza ndani ya thread hii baada ya kuwa msomaji wa muda mrefu, nakutana na wakorea uchwara kupitia keyboard, naanzisha utani wa ajabu haliyakuwa si tabia yangu, mara paaap nakufa kwa kucheka peke yangu.
kilaza kama mimi ninayeshindwa hata kuandika sentensi nzuri zenye kubeba haiba ya matukio husika ya sherehe muhimu basi niwatakie wakorea uchwara wote pasina kuangalia asili zetu za kiimani sikukuu ya kuzaliwa mtakatifu yule wa nazareth majuma machache yajayo.
kama kuna yeyote humu ndani niliwahi kumkera na akachukia kama wanavyochukiana mashabiki wa vyura na mikia naomba anisamehe.
jamani hapa mtaani kwetu ndani ya wiki mbili hizi wameshafariki watu 5, mamamaaaaaaaaaaa nadhani huyu malaika mtoa roho ananipigia misere kwa honda ya bajajiiiiiii na toyo.
ili niwe muhenga wa kati kati ndani ya JF napaswa nitimize miaka mingapi?
nasubiria keki zangu zilizotengenezwa kwa siagi na mayai ya maneno japokuwa wale niliowakuta wamekuwa wavivu wa kutembelea humu ndani kwa sababu zisizoepukika ila kwa mamlaka niliopewa ngoja nijaribu kuwakumbuka.
kila nitakayemtaja aitikie jana na leo kama mwalimu wa kiswahili.
hahahahahahahaaa halafu walimu wengi wa darasa walikuwa wanasomesha kiswahili, on my behalf of my self (kwa sauti ya mzee wa nyoka)
daebak, niilikuta hii thread ikiwa ukurasa wa 24 lakini leo imeshafikisha ukurasa wa 402, nawaomba munipe dawa itakayoniwezesha niache kuifuatilia hii thread tafadhali.
- Nifah = huyu ahjumma mtarajiwa baada ya miaka 27 alikuwa na nguvu kubwa sana ndani ya familia hii, naogopa kusema vyuma vimelegea kiupande wake, sijui amekutwa na time travel kama do min jooon wa my love from another star.
- Prishaz = huyu ahjumma mtarajiwa baada ya miaka 30 amekutwa na shambulio la Membe, dawa yake ni kukutana na kang ji hwan.
- Khantwe = nilikuwa namuogopa huyu ahjumma mtarajiwa kama simba, kumbe ni mdhaifu kwa watu wa JF kuliko mnyama swala (gazelle), ndio mwanadamu anayeshikilia rekodi ya kuwa na wanaume wa seoul wengi kwa njia ya ndotoni.
- mkorea, @Aipolo = hawa wote tabia zao zinafanana, wanapenda historical drama kuliko wakorea wanavyoipenda historia yao
- Katavi = huyu ahjusii ni bingwa wa kuchukua drama, hachagui project ya kuangalia.
Age is an issue of mind over matter. If you don't mind, it doesn't matter. - Mark Twain.
View attachment 969576