kwa wanandoa tu!

kwa wanandoa tu!

Mimi huwa nashangaa wanawakewanaowapa waume za watu mapenzi
hao wake zao ni wa nini? K

hahahah wake zetu wanakuwa wasumbufu kama tigo ilivyozingua leo kama huna mbada kimeo... tigo zingua unatulia na zain presha inapungu.. unaendelea kuwa hewa!! (kwa mwanaume unaendelea kuwa active)
 
wanandoa, ebu tuelezane ukweli hapa, hivi ni kwa lipi hasa linatufanya baadhi yetu tuwe tunatoka nje ya ndoa zetu ilhali tuna wenza wetu tunaowapenda kwa dhati? hivi ina maana pale mnapofunga ndoa mmoja wenu huwa anadanganya au anajaribu ndoa au? tunaweka mazingira yasiyovutia hasa kwa wale wasio kwenye ndoa kutotamani kuingia huko kwa kuwa kila kukicha wanachokisikia kuhusu ndoa ni bad news. jamani karibuni tujuzane ni kwa nini hali hii imekithiri sana siku hizi, na ni namna gani tutajaribu kuelimishana ili basi tuachane na mambo hayo na kuheshimu ndoa zetu.
nawasilisha.

Kubwa zaidi ni tamaa na kutokuwajibika ipasavyo ndani ya ndoa. Wengi tulio ndani ya ndoa tunajisahau sana na kukosa ubunifu ...
 
hili nalo neno...pia naona ni kuzoeana kutokana na kutokuwa wabunifu katika suala zima la mapenzi na kulinda ndoa na kila mmoja kuwa commited na uhusiano huo..duh, sasa suluhu sijui ni gani maana changamoto ni nyingi sana!
Kubwa zaidi ni tamaa na kutokuwajibika ipasavyo ndani ya ndoa. Wengi tulio ndani ya ndoa tunajisahau sana na kukosa ubunifu ...
 
hili nalo neno...pia naona ni kuzoeana kutokana na kutokuwa wabunifu katika suala zima la mapenzi na kulinda ndoa na kila mmoja kuwa commited na uhusiano huo..duh, sasa suluhu sijui ni gani maana changamoto ni nyingi sana!

Kubwa zaidi ni wanandoa kukaa pamoja na kukubali kufunguka kwa kutoa maelezo ya nini kinawakera na nini wanakifurahia zaidi. Ila ni ndoa chache sana zilizofikia hatua hizo ...
 
Mtasema mengi...na theory kibao lakini nature ina baki pale pale u cant fight it.
mke mmoja mme mmoja mpaka kifo kiwatenganishe haitekelezeki.

wewe utakuwa unamatatizo yako, inawezekana sana. na ukaishi kwa furaha tele.
 
ni kweli iron lady
kwangu mimi hii ishatokea sana,na nishaongea nae sana
atleast now mambo yanaenda vizuri

sasa si tunaambiana hali halisi?
na ukijua kuwa kuambiana na kuelekezana ni kuzuri kamwe hutataka kutoka nje maana hakuna mkamilifu. na hicho unachopata huko nje ukikipata nyumbani utafurahi zaidi, hakuna asiyefundishika si mwannaume wala mwanamke. ndoa ni tamu na ndoa ni chungu kama tu nyinyi wawili hamtajua namna ya kuishi changamoto za kawaida zipo. ila sababu ya kutoka nje kwa visingizio hivi si nzuri.
tujifunze kufundishana na kukubaliana na kukamilishana maisha yataenda na ndoa itastawi.
 
hahahah wake zetu wanakuwa wasumbufu kama tigo ilivyozingua leo kama huna mbada kimeo... tigo zingua unatulia na zain presha inapungu.. unaendelea kuwa hewa!! (kwa mwanaume unaendelea kuwa active)

sasa kama unafananisha wanawake na mitandao huna haja ya kuoa maana kuona ni kujifunga huo uhuru wa kubadilibadili ulishatoka pale uliposema ni huyu tu. usioe kaa tu uwe huru ubadilibadili kama mitandao ya simu.

halafu kiongozi, hata sisi wanawake ukituuliza nasi tunasema kuwa nyinyi ni wasumbufu sana tunawavumilia tu. somo hapa ni kujuana na kuvumiliana na kurekebishana.
 
sasa kama unafananisha wanawake na mitandao huna haja ya kuoa maana kuona ni kujifunga huo uhuru wa kubadilibadili ulishatoka pale uliposema ni huyu tu. usioe kaa tu uwe huru ubadilibadili kama mitandao ya simu.

halafu kiongozi, hata sisi wanawake ukituuliza nasi tunasema kuwa nyinyi ni wasumbufu sana tunawavumilia tu. somo hapa ni kujuana na kuvumiliana na kurekebishana.
naomba kukiwa na ile get together ya jf dar uje tushauriane kwa pamoja na kwa mapana

Nilipobold umenena ila kuna wengine wagumu...
 
wanaume wanasumbuliwa sana na tamaa hasa ukizingatia mabinti wa siku hz nao ni warembo sana ndo baasi tena wanaume hawatulii na wake zao.
 
naomba kukiwa na ile get together ya jf dar uje tushauriane kwa pamoja na kwa mapana

Nilipobold umenena ila kuna wengine wagumu...[/QUOTE]

kadri mnavyoishi utamlainisha tu kdri unavyojua weakness zake na strength zake utajua wapi pakumpatia na hapohapo ndio utatumia kumbadilisha kumfundisha nakumuelekeza. mwisho mtaendana tu. ni kweli ni ngumu lakini inawezekana.
 
Hili swala ni mtambuka sana kwa Dunia ya leo nikisema hivyo nitakuwa nimeeleweka. wiki tatu nyuma nilitoa uzi wangu humu jukwaani nilieleza kwamba semina za ndoa ni zaidi ya ndoa kwa ufahamu wangu na kwa elimu inayotolewa ktk hizi semina unafundishwa kila kitu jinsi ya kuishi wawaili kati ya mume na mkee na mkiweza kuyashika vizuri never swala la usaliti litakuwa ni hadithi kati yenu.
 
pia jamani tunatakiwa kumtegemea Mungu katika maisha ya ndoa ili atuongoze tuifurahie maana siku hizi watu tunamsahau sana Mungu wetu.
 
ndoa ni complicated sana tena inahitaji uvumilivu wa hali ya juu, naweza kusema m2 kutoka nje ya ndoa ni tabia yake,wengine yamewashinda ndani ya ndoa wanaamua kutoka. kama unyumba hamna ndani ya ndoa we unategemea nini!!? yaani inawezekana kabisa mafarakano yasiyokuwa na suluhisho kwa mda mrefu yakapelekea m2 akapendwa nje na akajiachia kwa raha zake. lakini nashauri bure tu, WANANDOA WAWE NA MUDA WAKUYAONGEA MAMBO YAO NA KUSULUHISHA. HAKUNA JAMBO ZURI KAMA HILO, UPENDO UNAONGEZEKA SIKU HADI SIKU. Lakini kama ni udhaifu upo kwa mmoja wao katika tendo la ndoa basi pia waangalie namna ya kurekebisha hapo. NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE ASEMA BWANA MUNGU.
 
Fanyeni mabadiliko upande wenu na haya yote yataisha.

Wamama wetu waliwezaje unakuta mama yupo bize ana watoto nyumbani kama 6 na anaenda shambani kulima kama baba anavyolima akirudi anaanza kutwanga mpunga hadi unakuwa mchele. Na bado ana keep ndoa yake intact miaka inakwenda. Lakini siku hizi mkishakuwa bize kidogo tu baaas housegirl anakuwa in charge...

ni kweli mkuu... nikiolewa nitajitahidi!!!!
 
na ukijua kuwa kuambiana na kuelekezana ni kuzuri kamwe hutataka kutoka nje maana hakuna mkamilifu. na hicho unachopata huko nje ukikipata nyumbani utafurahi zaidi, hakuna asiyefundishika si mwannaume wala mwanamke. ndoa ni tamu na ndoa ni chungu kama tu nyinyi wawili hamtajua namna ya kuishi changamoto za kawaida zipo. ila sababu ya kutoka nje kwa visingizio hivi si nzuri.
tujifunze kufundishana na kukubaliana na kukamilishana maisha yataenda na ndoa itastawi.

well said mdada... nimekukubali, tatizo ni kwamba wanaume wenhi wanaamini kuwa na mwanamke mmoja haiwezekani...
 
kuna pahala nilisoma pameandikwa..........if you are afraid of loneliness, do not marry
sasa sijui kuna ukweli hapo....manake people do really cheat ( kasoro mume wa natalia tu)
 
nimeipenda hiyo kaka lakini pia sio tu kuhamisha mapenzi kwa watoto shida ni wao kutoona kwamba anaweza kunivutia tena,from there sasa anaanza kujiwekea mazingira ya mm kutomtamani ni kama unarudi nyumbani umechoka unakota amekaa hajaoga as alikua anafanya ukiwa nae gheto hanukii vizuri tena and many.ila zaidi ni sisi wanaume wenyewe mazingira ya kuendekeza mfumo dume,huwezi hata mwambia mkeo kwamba "baby uwe unapendeza basi nifanye nikutamani eeeeh mpenz" sasa wewe zamani unamuita baby saa we nani .....ahhhhh tubadilike bana ndoa zina raha yake
 
Taarifa baada ya habari!!!!!!
Kucheat kunaruhusiwa kimtindo especially mamaa anapokuwa amejifungua na analea ila ndomu kama kawaida na usiruhusu nyumba ndogo itawale familia yako bana. mamaa akipona rudi nyumbani bana na nyumba ndogo piga chini!!!!!the most important thing is that do whatever you can mamaa asijue ulicheat!!!!!!
 
Tatizo la hii topic, nikijib hapa hata akina nivea watashtukia natoka nje... no, wataamini natoka nje...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom