Kwa wale wapenzi wa ufugaji wa Samaki, Vifaranga vya Sato vinapatikana

Jan 13, 2023
92
99
Habari za wakati huu?

Hii ni kwa wale wote wenye mapenzi au wanaovutiwa na shughuli za kilimo na ufugaji hususani ufugaji wa samaki

Tuna toa huduma ya kuuza Vifaranga/mbegu bora ya samaki aina ya Sato (Nile Tilapia)

Mbegu zetu ni nzuri Sana kwanza kabisa wana-uniform size, samaki wanakuwa haraka ndani ya muda mfupi, wanastahimili magonjwa na mabadiliko ya ubora wa maji

Bei ni Tsh 200 - 300 kwa kifaranga kimoja, chenye uzito kati ya 1g - 10g

Tunapatikana Mingoi, mbele kidogo ya Bunju B njia ya kuelekea Bagamoyo, pia tuna tuma mzigo kwa wahitaji waliyopo nje ya Dar/Pwani

Karibu

No. 0758779170

 
Ungetupa elimu ya ufugaji kwanza then ndo uje utuuzie vifaranga maana wengi wanaogopa kupata hasara
 
Ungetupa elimu ya ufugaji kwanza then ndo uje utuuzie vifaranga maana wengi wanaogopa kupata hasara
Ni sahihi nilitamani nianzie huko Ila nikaona andiko litakuwa refu sana na kimsingi andiko hili liliwalenga wale ambao wanauelewa kuhusu ufugaji samaki

NAELEZEA KWA UFUPI
Ufugaji wa samaki unahusisha kuzalisha, kulea na kuwafuga samaki nje ya mazingira yao ya asili

Ufugaji wa samaki unaweza kufanywa kwa njia ya bwawa, tank au hata ziwani kwa njia ya vizimba, muhimu ni kuwa na maji ya kutosha (maji baridi kwa Sato/kambale)

Chakula cha samaki, Kuna chakula cha aina mbili chakula cha asili cha samaki, mimea midogomidogo na wadudu (zooplanktons & phytoplanktons) Hiki uzalishwa baada ya kurutubisha maji kwa kutumia mbolea ya Ng'ombe, kuku n.k

Aina nyingine ya chakula ni chakula cha kutengenezq, Hiki akitofautiani Sana na kile cha kuku ingredients ni kama vile Pumba za mahindi/mpunga, dagaa/uduvi, mashudu ya pamba au alizeti n.k. Pia unaweza kununua chakula ambacho kipo tayari Kuna supplier wengi wanauza chakula kutoka nje ya nchi

Mambo mengine ya kuzingatia, kulisha kutwa Mara 2 hadi 4 kwa samaki wadogo, kuwalisha kulingana na uzito wao kwa wastani samaki anakula 5% ya uzito wake kwa siku, kupima uzito wao (sampling) kila mwezi ili kujua maendeleo ya ukuaji, kubadilisha maji at least mara moja kwa mwezi

Uzuri wa samaki case za magonjwa ni nadra sana, awahitaji chanjo wala madawa katika ukuaji wao, samaki ni watumiaji wazuri wa chakula unachowalisha ukimlisha let's say 1.5kg tarajia kupata samaki mwenye uzito wa 1kg na pia Samaki (Sato) ni kitoeo kizuri kinapendwa na karibu jamii yote ya Tanzania

Vitu ni vingi siwezi kuandika yote nikamaliza Ila kama unavutiwa na ulitamani kujifunza zaidi naweza kukuunga kwenye group letu ukajifunza zaidi

Karibu mjumbe wa bwana
 
Back
Top Bottom