Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 3,524
- 6,505
Tabia iliyomponza Ibilisi ni KIBURI. Baada ya kuambiwa na Mwenyezi Mungu amsujudie Adam sijida ya heshima basi yeye alikataa Kwa kujawa na Kiburi kwasababu yeye alijiona Bora sana.
Na alipoambiwa kwanini ulikataa kumsujudia Adam akasema;
Mimi ni Bora nimeumbwa Kwa Moto na yeye ameumbwa na Udongo
Kwahiyo Ibilisi akajiona yeye ni Bora zaidi ndio maana akakataa amri ya ya Mola wake.
Na Mwenyezi Mungu anasema hakika Kiburi ndio vazi lake kwahiyo yeyote ambaye analeta kiburi basi anafanya kosa kubwa Sana.
Na ili ujue Kibri ni kosa kubwa Sana mpaka Mwenyezi Mungu akamhukumu Ibilisi aende Motoni ,ebu tuangalie Ibilisi alikuwa wa namna gani.
Inasemwa Ibilisi alikuwa anafanya ibada Sana kiasi ambacho hakuna sehemu yoyote katika ardhi hakuacha Kusujudu,alisujudu kila sehemu Kwa AJILI ya kumwabudu Mola wake
Lakini
Pamoja na yote hayo basi Kiburi kikamuweka mbali na Mola wake na kuhukumiwa adhabu mbaya kabisa
Sasa baadhi yetu nasi tuna Uibilisi Fulani hivi ingawa ukitutazama machoni tunaonekana kama watu vile lakini tumejawa na Kiburi kupindukia katika Maisha yetu.
Kisa wewe ni CEO sehemu Fulani basi unajiona wewe ndio wewe, unajiona mpanaaa na wengine wote unawaona hawana maana kabisa,husikilizi shida za wafanyakazi wako,hujali mahitaji Yao kwasababu wewe ndio kila kitu hapo,usichojua ni kwamba kila kitu kina mwisho na IPO siku hiyo nafasi utaiacha, kwahiyo usitumie cheo kunyanyasa watu.
Malecture mpo? Nyie nanyi huwa mnajiona mko juu Sana kwasababu Maisha ya taaluma ya mwanachuo yapo mikononi mwenu basi mmejawa na Kiburi kuwa angamiza wanafunzi wenu tena saa nyingine kwasababu za kipuuzi Sana,machoni mnaonekana kama watu lkn mna Uibilisi Fulani hivi.
Madaktari na Manesi mpo? Nyie nanyi kwakuwa afya za binadamu wenzenu zipo mikononi mwenu basi Kiburi ni sehemu ya Maisha yenu. Mko radhi wagonjwa wafe au waendelee kupata maumivu kwasababu tu ya kiburi chenu,tena hawa manesi ndio balaa kabisa, mnayowafanyia wanawake wenzenu huko sehemu za kujifungua yaani Mungu Tu ndio anajua kwakweli, acheni Kiburi mwisho wenu utakuwa mbaya Sana.
Wana usalama kwanza nawapa Salute Kwa heshima yenu! Lakini nanyi pia huwa mnazingua Sana mnapokuwa katika majukumu yenu,kwa nafasi yenu huwa mna Kiburi Sana kwakuwa mna nguvu ambayo mmepewa na Katiba,niwakumbushe Tu ubinadamu ndio kila kitu katika Maisha IPO siku utaacha hayo majukumu na utarudi mtaani na huenda karma itafanya kazi yake.
Hiyo ni mifano michache Tu ambayo nimeitumia lkn watu viburi ambao Wana Uibilisi ndani yake wapo wengi Sana na wanakiburi Sana Kwa nafasi zao hadhi zao walizo kuwa nazo.
Niwakumbushe Tu kwamba Kiburi ni vazi la Mwenyezi Mungu kwahiyo unapokuwa Kiburi ni kana kwamba unataka kuchukua vazi lake nadhani mwisho wake unaujua utakuwaje.
Niwakumbushe nyie ni viumbe wa Allah hamna mnachokimiliki hapa duniani, kwahiyo muishi vizuri na watu na muwatendee wema daima dawamu ili muwe na mwisho mwema.
Ni hayo tu!
Kazakh destroyer
adriz
Msonjo
baby zu
reymage
To yeye
Mademoiselle
Na alipoambiwa kwanini ulikataa kumsujudia Adam akasema;
Mimi ni Bora nimeumbwa Kwa Moto na yeye ameumbwa na Udongo
Kwahiyo Ibilisi akajiona yeye ni Bora zaidi ndio maana akakataa amri ya ya Mola wake.
Na Mwenyezi Mungu anasema hakika Kiburi ndio vazi lake kwahiyo yeyote ambaye analeta kiburi basi anafanya kosa kubwa Sana.
Na ili ujue Kibri ni kosa kubwa Sana mpaka Mwenyezi Mungu akamhukumu Ibilisi aende Motoni ,ebu tuangalie Ibilisi alikuwa wa namna gani.
Inasemwa Ibilisi alikuwa anafanya ibada Sana kiasi ambacho hakuna sehemu yoyote katika ardhi hakuacha Kusujudu,alisujudu kila sehemu Kwa AJILI ya kumwabudu Mola wake
Lakini
Pamoja na yote hayo basi Kiburi kikamuweka mbali na Mola wake na kuhukumiwa adhabu mbaya kabisa
Sasa baadhi yetu nasi tuna Uibilisi Fulani hivi ingawa ukitutazama machoni tunaonekana kama watu vile lakini tumejawa na Kiburi kupindukia katika Maisha yetu.
Kisa wewe ni CEO sehemu Fulani basi unajiona wewe ndio wewe, unajiona mpanaaa na wengine wote unawaona hawana maana kabisa,husikilizi shida za wafanyakazi wako,hujali mahitaji Yao kwasababu wewe ndio kila kitu hapo,usichojua ni kwamba kila kitu kina mwisho na IPO siku hiyo nafasi utaiacha, kwahiyo usitumie cheo kunyanyasa watu.
Malecture mpo? Nyie nanyi huwa mnajiona mko juu Sana kwasababu Maisha ya taaluma ya mwanachuo yapo mikononi mwenu basi mmejawa na Kiburi kuwa angamiza wanafunzi wenu tena saa nyingine kwasababu za kipuuzi Sana,machoni mnaonekana kama watu lkn mna Uibilisi Fulani hivi.
Madaktari na Manesi mpo? Nyie nanyi kwakuwa afya za binadamu wenzenu zipo mikononi mwenu basi Kiburi ni sehemu ya Maisha yenu. Mko radhi wagonjwa wafe au waendelee kupata maumivu kwasababu tu ya kiburi chenu,tena hawa manesi ndio balaa kabisa, mnayowafanyia wanawake wenzenu huko sehemu za kujifungua yaani Mungu Tu ndio anajua kwakweli, acheni Kiburi mwisho wenu utakuwa mbaya Sana.
Wana usalama kwanza nawapa Salute Kwa heshima yenu! Lakini nanyi pia huwa mnazingua Sana mnapokuwa katika majukumu yenu,kwa nafasi yenu huwa mna Kiburi Sana kwakuwa mna nguvu ambayo mmepewa na Katiba,niwakumbushe Tu ubinadamu ndio kila kitu katika Maisha IPO siku utaacha hayo majukumu na utarudi mtaani na huenda karma itafanya kazi yake.
Hiyo ni mifano michache Tu ambayo nimeitumia lkn watu viburi ambao Wana Uibilisi ndani yake wapo wengi Sana na wanakiburi Sana Kwa nafasi zao hadhi zao walizo kuwa nazo.
Niwakumbushe Tu kwamba Kiburi ni vazi la Mwenyezi Mungu kwahiyo unapokuwa Kiburi ni kana kwamba unataka kuchukua vazi lake nadhani mwisho wake unaujua utakuwaje.
Niwakumbushe nyie ni viumbe wa Allah hamna mnachokimiliki hapa duniani, kwahiyo muishi vizuri na watu na muwatendee wema daima dawamu ili muwe na mwisho mwema.
Ni hayo tu!
Kazakh destroyer
adriz
Msonjo
baby zu
reymage
To yeye
Mademoiselle