Naona hapa umechanganya. Asha Rose ni CCM.
Asha Rose ni Asha Rose Migiro. CCM ni CCM (Chama cha Mafisadi) Hivyo Asha Rose si Chama cha Mafisadi. Wewe ndie uliyechanganya. Anachoweza kuwa ni mwanachama wa Chama cha Mafisadi. Upo?
Naona hapa umechanganya. Asha Rose ni CCM.
Kumbe na wewe ni katika wale wanaomchukia huyu mama..!!!!
Nilijua wewe ni mleta mada tu, lakini kumbe uliuleta huu uzi ili upate kumchafua vizuri. Nadhani nia yako imetimia.
Wenzake akina nani??? Koffi Anani sio mwenzake. Koffi Anani alikuwa SG, naye Dr.Migiro alikuwa DSG. Hata kuingia kwao hao watu wawili miamala yao ni tofauti kabisa. Mkuu fikiria kwanza kabla ya kuandika kwani humu huongei na watoto wadogo wasiofahamu mambo.
Kwa nafasi aliyokuwa nayo Migiro ya DSG yeye ndie kaweka historia ya kukaa kwa muda mrefu kuliko wote kwenye hiyo post katika historia ya UN. Je na hao waliopita waliboronga???? kama ni kweli waliboronga basi we have to be proud for Migiro kwa sababu yaonyesha kuwa yeye ana afadhali angalau amemaliza muhula mmoja.
i knew you was coming to me. Kuna kufanana kokote kati ya kumaliza muda wa uongozi na kustaafu? Tena kuna uhalali wowote wa Migiro kuambatana na uongozi wa kiserikali katika itifaki zake?
Lema ana cheo gani Chadema saizi mbona anachangisha pesa.
Hujajibu swali! Koment yako ya hapo mwanzo ulisema Asha hajaperfom sawasawa.
Kama katbu mkuu wa sasa wa UN anatumikia kipindi chake chote (5yrs+5yrs=10yrs) kama ilivyokuwaga kwa watangulizi wake, kwanini Asha rozi nae asimalizie kipindi chote cha miaka 10?.Hata hapa nyumbani pia Uraisi ni kila baada ya miaka mitano lakini wengi humalizia vipindi vyote viwili 10yrs.Pungufu ya hapo lazima unamatatizo!
Asha Rose ni Asha Rose Migiro. CCM ni CCM (Chama cha Mafisadi) Hivyo Asha Rose si Chama cha Mafisadi. Wewe ndie uliyechanganya. Anachoweza kuwa ni mwanachama wa Chama cha Mafisadi. Upo?
Kwa hiyo wewe unaongea kinadharia na sio reallity. Mkuu, kufikiria tu kwamba kwa vile mtu hajamaliza kipindi chake cha uongozi basi ame-under perform sio hoja yenye mashiko.
Hali ya kuwa kauli ya Bosi wake katika hafla ya kumuaga inaashiria tofauti na maelezo yako.
"Ms Migiro's experience in responding as UN Deputy Secretary General, combined with her many years as an advocate for health and social justice in Africa, make her uniquely qualified for this important role," said Mr Ban.
Mr Ban ndie mtu pekee anaeweza kutuaminisha juu ya utendaji wa Dr. Migiro.
Inaniwia vigumu kukuelewa kwa jinsi unavyotaka umma wa watanzania tuamini kwa hizo kauli zenu humu ndani ya JF juu ya utendaji wa Migiro na tuache kuamini kauli ya Mr.Ban tena aliyoitoa mbele ya public na mbele ya vyombo vya habari vya ulimwengu mzima.
Watanzania tubadilikeni, majungu tuacheni, hio sio mila yetu wala ya mababu zetu.
Mr Ban ilibidi amfariji tuu.We ulitaka aongee mbovu. Migiro hamna kitu!TZ inawanawake wengi vichwa, ila sio Migiro.
Arudi kwenye ualimu akafundishe tuu.Kama nchini mwake hajawahi kufanya kitu akakumbukwa, Kimataifa atawezaje?
Can you prove her failure????
Kama unatabia ya kumsifia mtu kiunafiki, is not the same applied to the international level.
Wenzetu wakimsifia mtu wanamaanisha kweli, na hata kama umeboronga na hawataki kusema mabaya yako kwa kukulindia heshima, watakaa kimya na katu hawatokupa sifa zisizokustahiki. The same applied to Migiro, hata kama kuna upungufu katika performance yake, well, she is a human being. Lakini kwa mazuri tuliyoyasikia kuhusu yeye ni kweli tupu na ni stahiki yake. Soma kauli ya Mr.Ban hapo chini.........
" Kama ni kuvaa viatu vyake, naweza kusema ningechekesha sana, kwa ufupi siwezi kuvaa viatu vya Migiro, amekuwa msaada mkubwa sana kwangu, ameniwakilisha vema kila mahali nilipomtuma hata katika mazingira magumu na ya hatari, kote ameniwakilisha vema sana, kama mwalimu wangu, na kama profesa wangu anastahili alama ya juu sana............Siyo rahisi kuelezea yale aliyoyafanya nyuma ya pazia, namna gani alivyochapa kazi kwa nguvu, yapo mengi makubwa ambayo Migiro ameyafanya na kuyakamilisha kwa uadilifu wa hali ya juu. Migiro ni mwanadiplomasia aliyebobea lakini ni mtu wa vitendo, vitendo ambavyo lazima utaona matunda yake.......Migiro amefanya kazi na viongozi wagumu, kiwamo aliyekuwa Rais wa Libya Muammar Quadaff aliyethubutu hata kumrushia katiba ya Umoja wa Mataifa, amezikuna nyonyo za watu wengi wakiwamo watu wanyonge na wenye matatizo mbalimbali. Migoro unaondoka, lakini Umoja wa Mataifa hauta sahau mchango wako. Hapa ni nyumbani kwako, na nitaendelea kuomba msaada wako na ushirikiano wako, bado nitaendelea kukuhitaji"
........................Mwisho wa kunukuu.
Nataka humu ndani ya JF mniambie na tuache unafiki wa kimajungu:
"Ni nani ataweza kutuaminisha juu ya utendaji wa Migiro zaidi ya bosi Mr.Ban?? Yeye ndie alikuwa supervisor wake ambae Migiro alikuwa anaripoti kwake. Kauli yoyote ile inayohusu utendaji wa Migiro itakayokwenda kinyume na kauli ya Mr.Ban basi hayo yatakuwa ni majungu ya kupikwa ambayo ni kawaida kwa mfanyakazi bora kazini kupikiwa majungu.
Lema ana cheo gani Chadema saizi mbona anachangisha pesa.
Jaribu kupunguza kiherehere. Binafsi sina tofauti zozote na migiro. Cha msingi tujue uhalali wa uhusika wake katika siasa za tz kwa sasa.
nimekupenda mkuu Kibunago.
Anaandaliwa mazingira ya uraisi, wakiwezeshwa wanaweza.
:nono: