Kwanini mahusiano/ndoa nyingi hazidumu?

Fanya kile moyo wako unataka, fanya kitu kinachoufurahisha moyo wala si vinginevyo. Mke kakaa kwenye TV mpaka saa 8 usiku akitizama bongo movie kamuacha mume kalala peke yake, uzungu mwingi huku Tanzania. Tanzania tunapenda sana kuigiza kuliko kufanya mambo kihalisia, ha ha haaaa!
 
Kinachoniboa ni hii culture ya michango jamannii,si tulage dinner tu hivi watu wachache afu basi
watu wanakodi magari ya wazi yenye maspika na watu wanaserebuka mji mzima. kuoa kumekua complex mno. kwanza sendofu na utoaji wa mali ni harusi tosha kwa jinsi wanavyozikocompleksisha.
 
Hata ukikaa na kufikiri miaka mia, haibadilishi changamoto zilizopo kuhusu maisha ya wawili.
..niwaze kuhusu watoto, kwani anayeleta watoto ni mimi au Mungu? Nitafanya lillilo chini ya uwezo wangu :) then Mungu atanipa kwa kadri apendavyo.
..niwaze kuhusu maradhi, hata nikiwa peke yangu, bado naweza kuumwa au kupata changamoto ya kiuguza ndugu au mzazi.

Kupata mtu anayefikiria ndoa zaidi ya sherehe ndio changamoto mliyonayo vijana ambao hamjaoa/kuolewa, mtu anayedhani kuwa maisha kwa ujumla wake ni "rollercoaster", kuwa kuwa na pesa, magari na nyumba "as you call it bonus" ni utimilifu wa ndoa. Maisha ya ndoa is more than that. Again even the one you think is your soul mate can put you to h3ll, hata muishi miaka mia kwenye uchumba, majaribu ni LAZIMA!!
 
Nakubaliana na wewe mkuu kwa asilimia zote,watu wanafikiria Ndoa ni lele mama,mie ningejua mwanzo Ndoa ikoje mbona ningesema basi staki tena,kama hukujikaza wallah hukai hata miezi 6,manake baada ya ndoa tuu ndio ma buzi ndio yatakua mengi mpaka unajiuliza jamani mlikua wapi mwanzo,kwa upande wa mume nae Totoz wanajileta mpaka unasikia kichefuchefu,upande wa pili kuna ma wifi na na mashemeji wana midomo na maneno makali utadhani wao hawana watoto au hawana mume/mke, lakini chamsingi bora hizo hela za mchango ukalipie japo kodi ya nyumba na usitake harusi kubwa
kwanza hapo kwenye harusi unaweza ukapa mtu akakutonya "yule alovaa nguo ya red anaecheza sana ndio mwanamke wake
na yeye ndio kamualika aje akuone tena kaja na wapambe wake wakuthamini kama unamfikia uzuri" hapo bi harusi picha lazima zitoke kama analia...
Asante kwa mawazo mazuri.
 
Hata ukikaa na kufikiri miaka mia, haibadilishi changamoto zilizopo kuhusu maisha ya wawili.
..niwaze kuhusu watoto, kwani anayeleta watoto ni mimi au Mungu? Nitafanya lillilo chini ya uwezo wangu :) then Mungu atanipa kwa kadri apendavyo.
..niwaze kuhusu maradhi, hata nikiwa peke yangu, bado naweza kuumwa au kupata changamoto ya kiuguza ndugu au mzazi.

Kupata mtu anayefikiria ndoa zaidi ya sherehe ndio changamoto mliyonayo vijana ambao hamjaoa/kuolewa, mtu anayedhani kuwa maisha kwa ujumla wake ni "rollercoaster", kuwa kuwa na pesa, magari na nyumba "as you call it bonus" ni utimilifu wa ndoa. Maisha ya ndoa is more than that. Again even the one you think is your soul mate can put you to h3ll, hata muishi miaka mia kwenye uchumba, majaribu ni LAZIMA!!
Asante kwa maoni.
 
Kati ya vtu ninavoviogopa ni ndoa nikiona watu walioolewa na kuoa wanavoteseka. Mwanaume anaoa michepuko daily migogoro. Nadhani before entering kwenye marriage lazima kujiandaa kiakili kimwili na kiroho na kuacha mambo yote na kuwa committed haswa pia kuwa na hofu ya Mungu bila hivo aisee
Usiogope ndoa.
 
Ndoa ni makubaliano na kudumu au kutokudumu kunategemeana na msimamo wa nyie wote wawili. Over
 
Unapoingia kwenye ndoa tambua kwamba kutakuwa na matokeo chanya na hasi hivyo jiandae kukabiliana nayo yote.Ila kwa kweli kama hujajipanga kisaikolojia,ndoa ipe shikamoo yake alafu wewe pita hiviiiiii......
 
NDOA KWANINI HAZIDUMU SIKU HIZI

Ndoa hazidumu kwa sababu kabla ya kufunga ndoa watu wanakuwa obssesed na wedding ceremony imaginations, bila kujua ndoa inaenda mbali zaidi!
Kuna ndoa na kuna harusi...

Wengi mnapenda zaidi harusi, na mnapowaza ndoa picha inayowajia ni suti kali, boonge la shela kutoka Uturuki, make up ya ukweli ya bibi harusi kutoka Maznat Mikocheni, mashosti kuingia ukumbini na wimbo wa selfie,wanafiki kukomeshwa kwa jinsi pati yako itakavyokuwa kali pale Karimjee Hall.

Je, Umewahi kuwaza?

1. Mmeo au mkeo akiumwa miaka 5 mfululizo utaweza kumvumilia?

2. Watoto watakapozaliwa na ulemavu utawa-care namna gani?

3. Mtakapokosa watoto miaka 6 ya ndoa utahimili maneno ya mama mkwe na mawifi kwamba unawajazia choo cha kaka yao na huna kizazi?

Ndoa ni zaidi ya sherehe ya harusi. Baada ya yale matarumbeta kuzimika usiku kifuatacho ni majukumu mazito na kiapo kisichovunjika.

Achana na fantasy za kwaito,waza mbali kidoogo.

Je, Uko tayari kuwa mme au mke wa mtu mmoja tu au Ma-Ex watarejea kidogo kidogo kama hupati satisfaction ya kutosha kama ya Ex wako?

Huwa mnawaza hayo au mnawaza zawadi ya kamati itatoa Verossa ya kuanzia maisha?

Sidhani kabla ya kuoa na kuolewa jiulize,unatamani ndoa au ni tamaa ya sherehe ya harusi?
Well said mkuu
 
Kimsingi ndoa ni jambo jema na lenye kuleta faraja kubwa sana maishani kwa wana ndoa. Mambo sio mabaya kama hivyo yanavyotiwa chumvi, kuna ndoa nyingi zimedumu kwa upendo, furaha na amani. Asiliamia kubwa ya wana ndoa wana maisha bora zaidi kuliko waliyokuwa nayo kabla kuoa au kuolewa. Ndoa zimewafanya wamekua kiakili na kutambua majukumu kimaisha katika jamii. Kuoa au kuolewa kunatimiza misingi mikuu ya maisha ya mwanadamu. Ndio kuna changamoto za hapa na pale hazikosekani lakini hiyo ni kawaida ya maisha, bila changamoto hakuna maisha, changamoto zinatufundisha kukomaa na kujenga ukaribu wa wanandoa, hata ukiishi na wazazi, ndugu lazima mikwaruzano ya hapa na pale ijitokezee, huwezi kuacha kuishi kwsabababu kuna matatizo katika ndoa. Ndoa moja ya ndugu au rafiki kuwa mbaya au kuvunjika haina maana kwamba 'Ndoa Hazidumu Siku Hizi' na kupelekea kuchochea mawazo mabaya kuhusu ndoa. Inasikitisha kuona vijana wengi wakiwa na mawazo hasi kuhusu ndoa wakati wala hawajaingia katika ndoa. Ni faraja ilioje unaporudi nyumbani kwako jioni baada ya siku ndefu na ngumu kazini unakuta angalau kuna mwenzako wa kumshirikisha jinsi siku yako ilivyoenda leo. Tuitazame ndoa kwa mapana na marefu na sio kirahisi rahisi tu na kejeli. Wanaokejeli ndoa hebu wajiulize wao wangekuwa wapi leo kama taasisi hii ya ndoa isingekuwepo.
Asante sana kwa maoni mazuri.
 
Habari za muda huu wapendwa......bila shaka Mungu katujaalia uzima.....na wenye maradhi Mungu awajaalie afya njema.....

Kwa kawaida Ndoa ni tukio lenye furaha sana....lakini kwa bahati mbaya imekuwa sio furaha yenye kudumu......ambapo mwisho wake huwa ni majuto ya kwanini niliamua kuoa au kuolewa.......

Sababu hizi zinaweza kuwa chanzo cha migogoro au kuvunjika kwa ndoa nyingi sana....au mahusiano.....

>Matarajio yaliyopitiliza.....
Kwa kawaida kila mmoja wetu hutazamia mambo makubwa kutoka kwa mwenzie....katika mahusiano......matarajio hayo wakati mwingine hupitiliza na hata kumuona mwenza wake kama malaika.........matarajio yaliyopitiliza kwenye mahusiano yanaweza kukufanya ukakosa amani na kushindwa kulifurahia pendo......

> Fikra HASI juu ya mwenzio.....
Kawaida mahusiano yenye furaha na amani hayaji automatically bali hujengwa.....unapokuwa na fikra hasi au na wasi wasi juu ya mienendo ya mwenzio.....na ukaamua kukaa kimya juu ya hilo ni wazi kuwa badala ya kujenga.....unabomoa utamu wa penzi lako wewe mwenyewe....kwa hisia zako mbaya.......inawezekana unavyowaza sivyo ambavyo mwenzio alivyo......

Vile vile kati yenu hakuna mkamilifu....kwa hiyo kukosea au kutoka nje ya mstari ni mambo ya kawaida....ambayo yanawezekana kuwekwa sawa kwa maongezi tu ya kawaida kwa wapendanao.....

> Usiri uliopitiliza......
Ni ajabu kuona kuwa wapenzi wa siku hizi wanaweza wakaishi hata miaka mitano....lakini bado wakawa hawafahamiani kabisa....hii inatokana na ukweli.....kuwa wanandoa wengi hawapo huru......wanafichana mambo mengi sana.......hata yale ambayo ni ya kawaida kabisa......mwisho mambo yatakapoanza kujulikana hadharani.....inashusha kiwango cha uaminifu baina yao....na hatimaye mikwaruzano isiyokwisha na ndoa kukosa amani......

Kuwa muwazi kwa mwenzio ili kuondoa mashaka kwa mwenzio......

> Hali ya kiuchumi.....
Hakuna asiyejua nguvu ya pesa kwenye mahusiano kwenye nyakati hizi......

Na bila ya shaka kuna nyakati mambo yetu kiuchumi.....huyumba.....na ndio kipindi ambapo migogoro mingi huzuka kwenye Ndoa kukosa amani.......ni kipindi UPENDO baina ya wanandoa unawekwa kwenye mizani.....kuwa uzito unaanekana wakati wa furaha ni original au ni fake.....!!!

> Uongo.......
Bila ya shaka uongo ni kitu chenye kukera sana.....lakini mwanzo unapoutumia kufanikisha mipango yako unakuwa ndio silaha kuu........
Lakini bila ya kujua kuwa silaha hiyo hiyo ndio itakayokuja kukuhukumu......

Mahusiano au ndoa iliyojengwa katika misingi ya UONGO na ulaghai....huwa haiwi imara na haishiwi na migogoro....kwani uongo hauna sifa ya kudumu bali maisha yake ni mafupi sana.....

Kuishi ndani ya dimbwi la uongo ni kazi....kwa kuwa tangu siku utakayoongopa ndipo utakapoanza vita ya kuulinda uongo.....hakika ni maisha ya mashaka sana...kama sio ya wasi wasi......
DAIMA UKWELI UTAKUWEKA HURU........
Sema kweli japo inauma......

>Kutokutimiza wajibu...
Kama nilivyosema kuwa ndoa imara au mahusiano mazuri hujengwa wenyewe waliopo kwenye mahusiano....na wanaobomoa ndoa ni wanandoa wenyewe....
Lakini pia ndoa imara inajengwa na kila mwanandoa kutimiza wajibu wake kwenye ndoa.......

Kama dhumuni la ndoa ni kuwa na furaha na kuleta amani basi kila mmoja wetu na apiganie hilo....kwa nafasi yake.....na sio kutegemea mwenzio akutimizie hilo.....kama wewe una haki ya kupata furaha kwenye ndoa....basi vile vile una wajibu wa kuhangaikia furaha.....hiyo.....

> Uelewa finyu juu ya NDOA......
Nimeona ndoa nyingi za vijana zikivunjika na nyingi kukosa amani na furaha.....lakini ukiwasikiliza malalamiko yao.....utagundua kuwa wana uelewa mdogo sana wa jambo hilo.....na ndio maana wanashindwa kuwajibika nalo.....misukumo inayowafanya waingie kwenye ndoa ni ya kijinga sana.....ambapo naweza kusema kuwa ni ya kitoto.....

Hivyo ni vyema vijana wakajitahidi kupata habari na taarifa juu ya jambo hilo....kabla ya kuliendea......


Kwa leo ngoja niishie hapa....

Nawasilisha......
 
Back
Top Bottom