Kwanini mahusiano/ndoa nyingi hazidumu?

Kwanini mahusiano/ndoa nyingi hazidumu?

NDOA KWANINI HAZIDUMU SIKU HIZI

Ndoa hazidumu kwa sababu kabla ya kufunga ndoa watu wanakuwa obssesed na wedding ceremony imaginations, bila kujua ndoa inaenda mbali zaidi!
Kuna ndoa na kuna harusi...

Wengi mnapenda zaidi harusi, na mnapowaza ndoa picha inayowajia ni suti kali, boonge la shela kutoka Uturuki, make up ya ukweli ya bibi harusi kutoka Maznat Mikocheni, mashosti kuingia ukumbini na wimbo wa selfie,wanafiki kukomeshwa kwa jinsi pati yako itakavyokuwa kali pale Karimjee Hall.

Je, Umewahi kuwaza?

1. Mmeo au mkeo akiumwa miaka 5 mfululizo utaweza kumvumilia?

2. Watoto watakapozaliwa na ulemavu utawa-care namna gani?

3. Mtakapokosa watoto miaka 6 ya ndoa utahimili maneno ya mama mkwe na mawifi kwamba unawajazia choo cha kaka yao na huna kizazi?

Ndoa ni zaidi ya sherehe ya harusi. Baada ya yale matarumbeta kuzimika usiku kifuatacho ni majukumu mazito na kiapo kisichovunjika.

Achana na fantasy za kwaito,waza mbali kidoogo.

Je, Uko tayari kuwa mme au mke wa mtu mmoja tu au Ma-Ex watarejea kidogo kidogo kama hupati satisfaction ya kutosha kama ya Ex wako?

Huwa mnawaza hayo au mnawaza zawadi ya kamati itatoa Verossa ya kuanzia maisha?

Sidhani kabla ya kuoa na kuolewa jiulize,unatamani ndoa au ni tamaa ya sherehe ya harusi?
 
Wakijiuliza maswali hayo uliyoyainisha wabongo na kuyafanyia kazi nahamia MARS! Hatutaki kufikiri beyond tunataka kuona vile tunavyotaka tuone tu,halafu reality iki-take its place tunaanza kulaumu na kutafuta chanzo! Vyanzo ni sisi wenyewe,tubadilike kifikra na kimatendo pia. Tusikurupukie tu ndoa!
 
Maisha yamekuwa maigizo hizo ndoa zitadumu vipi?wazee wetu walifanya further investigation na kujiridhisha sisi upembuzi yakinifu umebakia penye projects za kupiga hela tu.Watu mnakutana billz au Serena baada ya siku 3 mnatutembezea kadi za michango na harusi mnataka mtokee front page ya magazeti yote ya UDAKU unadhani itasimama hiyo ndoa?achilia mbali Beijing na ubrothermen mwingi niambie hiyo ndoa inawezaje kudumu?
 
Wakijiuliza maswali hayo uliyoyainisha wabongo na kuyafanyia kazi nahamia MARS! Hatutaki kufikiri beyond tunataka kuona vile tunavyotaka tuone tu,halafu reality iki-take its place tunaanza kulaumu na kutafuta chanzo! Vyanzo ni sisi wenyewe,tubadilike kifikra na kimatendo pia. Tusikurupukie tu ndoa!
Asante kwa mawazo mazurii sanaa.. ila kila jambo linawezekana ni kijipanga.
 
Maisha yamekuwa maigizo hizo ndoa zitadumu vipi?wazee wetu walifanya further investigation na kujiridhisha sisi upembuzi yakinifu umebakia penye projects za kupiga hela tu.Watu mnakutana billz au Serena baada ya siku 3 mnatutembezea kadi za michango na harusi mnataka mtokee front page ya magazeti yote ya UDAKU unadhani itasimama hiyo ndoa?achilia mbali Beijing na ubrothermen mwingi niambie hiyo ndoa inawezaje kudumu?
Asante kwa maneno mazuri.
 
Kuolewa/kuoa kwa vile rafiki.,ndugu wameolewa.......achilia mbali muda.umekwenda anayekuja sukuma twende liwalo na liwe huko baadaye.....ndio maisha ya ndoa yaliyopo sasa....
 
Nakubaliana na wewe mkuu kwa asilimia zote,watu wanafikiria Ndoa ni lele mama,mie ningejua mwanzo Ndoa ikoje mbona ningesema basi staki tena,kama hukujikaza wallah hukai hata miezi 6,manake baada ya ndoa tuu ndio ma buzi ndio yatakua mengi mpaka unajiuliza jamani mlikua wapi mwanzo,kwa upande wa mume nae Totoz wanajileta mpaka unasikia kichefuchefu,upande wa pili kuna ma wifi na na mashemeji wana midomo na maneno makali utadhani wao hawana watoto au hawana mume/mke, lakini chamsingi bora hizo hela za mchango ukalipie japo kodi ya nyumba na usitake harusi kubwa
kwanza hapo kwenye harusi unaweza ukapa mtu akakutonya "yule alovaa nguo ya red anaecheza sana ndio mwanamke wake
na yeye ndio kamualika aje akuone tena kaja na wapambe wake wakuthamini kama unamfikia uzuri" hapo bi harusi picha lazima zitoke kama analia...
 
Ndoa ni mpango wa Mungu, akili na mawazo ya Mungu hayachunguziki hivyo sioni sababu ya kujiuliza saaaaaana, let's me do my best and God will do the rest.
 
Ndoa ni wito hahaaa manake km huna wito unaoa/unaolewa ijumaa jumatatu taraka
 
Hill halinihusu. kuoa haimo katika mipango yangu ya maisha. ukitaka kupoteza furaha ya maisha yako, oa/olewa.
 
Nakubaliana na wewe mkuu kwa asilimia zote,watu wanafikiria Ndoa ni lele mama,mie ningejua mwanzo Ndoa ikoje mbona ningesema basi staki tena,kama hukujikaza wallah hukai hata miezi 6,manake baada ya ndoa tuu ndio ma buzi ndio yatakua mengi mpaka unajiuliza jamani mlikua wapi mwanzo,kwa upande wa mume nae Totoz wanajileta mpaka unasikia kichefuchefu,upande wa pili kuna ma wifi na na mashemeji wana midomo na maneno makali utadhani wao hawana watoto au hawana mume/mke, lakini chamsingi bora hizo hela za mchango ukalipie japo kodi ya nyumba na usitake harusi kubwa
kwanza hapo kwenye harusi unaweza ukapa mtu akakutonya "yule alovaa nguo ya red anaecheza sana ndio mwanamke wake
na yeye ndio kamualika aje akuone tena kaja na wapambe wake wakuthamini kama unamfikia uzuri" hapo bi harusi picha lazima zitoke kama analia...
Hahaha! Apo kwenye kutonywa ni balaa inaweza biaashara ikaisha apoapo kuna watu nuksi
 
Hahaha! Apo kwenye kutonywa ni balaa inaweza biaashara ikaisha apoapo kuna watu nuksi
Umeona eeeeh! Binadamu wengine nuksi huko kote hawajasema pale ndio wanapokutia jiti la Roho ukatamani kufa..
 
Back
Top Bottom