Kwa rasimu hii, CCM inakufa

Kwa rasimu hii, CCM inakufa

Muhimu ni kusubiri kuisoma rasimu yote kwa utulivu ndo tuje na maoni hapa.MaCCM wajanja sana wanaweza kuwatega padogo mkaingia mkenge.!
 
Umeandika ukweli sana Mkuu , ndiyo maana nilisema kama tutakuwa na Tume huru ya Uchaguzi , hata hiyo rushwa ya Kitanda kwa kitanda inaweza kukomeshwa .
Mkuu, hapo kwenye RED unanishitua, hii ndiyo ruswa ya aina gani?. Samahani sijawahi kuisikia katika maisha yangu.
 
Sasa mkuu mambo ya uchama yametokea wapi? Tume ina base nzuri sana ya utaifa zaidi. Achana na mambo ya uchama. Taifa kwanza mkuu.
 
Matola hapo ndipo tulikuwa tunatofautiana lakini mimi nimejibu kulingana na jibu alilolitoa Mzee Warioba.

Sasa hawa Waislamu wa bara nao wana matatizo au lao jambo kwa sababu kama zanzibar wana mahakama ya kadhi inayoendesha mambo yake kama wanavyopenda, kwa nini waislamu wa bara wang'ang'anie kuwa na mahakama ya kadhi tofauti naya Zanzibar.

Kung'ang'ania na hoja yao hii ni kutafuta marumbano na serikali yasiyo kuwa na maana. Kama watu wa UAMSHO wanakubaliana na mahakama ya kadhi huko zanzibar, kwa nini masheikh wa bara wasifanye kama Zanzibar?

May be, I'm missing a point!
Mzee Warioba hana jibu la hili na ndio maana mambo yenye utata tume yake wameyatupa kwenye mambo yasiyo ya Muungano, ili kama ni kuparurana basi waparurane wenyewe wakati yeye ameshamaliza kazi yake na ya kamati yake.

Kuhusu hili la Mahakama ya kadhi Waislamu kuradhimisha liingizwe kwenye katiba na igharamiwe na pesa za walipa kodi hapa CCM moja kwa moja inahusika kwa kuipanda mbegu hii ambayo hawakuyajuwa madhara yake.

Kanisa Katoliki nalo lina mahakama zake wanatumia Canon law lakini hakuna ulalamishi huu kwamba Canon law itambulike kikatiba wao wanaendesha mambo yao kimya kimya na ukienda kinyume kisa si ya kikatiba basi simple decision unatengwa na kanisa.

Hili la kuniuliza kwa nini Waislamu wa Tanganyika wanakuwa ni walalamishi wakati wa Zanzibar hawana tatizo na hilo labda tu nirudishe swali kwako ni nchi gani Muslim there happy in this world?
 
You should have gone to specsavers, CCM chama cha weledi, kwa taarifa yako rasimu hii ni kuwakaanga Mi-Chadema kwa mafuta yao, Leo CCM imezaliwa upya na imeonyesha kukomaa kwake kisiasa.


mmh! ccm izaliwe upya kwa Rasmu hii! Unaweza kuelezea weledi wa ccm? Hapa naamini tumetanguliza u-chama kwanza badala ya utaifa!
 
Mzee Warioba hana jibu la hili na ndio maana mambo yenye utata tume yake wameyatupa kwenye mambo yasiyo ya Muungano, ili kama ni kuparurana basi waparurane wenyewe wakati yeye ameshamaliza kazi yake na ya kamati yake.

Kuhusu hili la Mahakama ya kadhi Waislamu kuradhimisha liingizwe kwenye katiba na igharamiwe na pesa za walipa kodi hapa CCM moja kwa moja inahusika kwa kuipanda mbegu hii ambayo hawakuyajuwa madhara yake.

Kanisa Katoliki nalo lina mahakama zake wanatumia Canon law lakini hakuna ulalamishi huu kwamba Canon law itambulike kikatiba wao wanaendesha mambo yao kimya kimya na ukienda kinyume kisa si ya kikatiba basi simple decision unatengwa na kanisa.

Hili la kuniuliza kwa nini Waislamu wa Tanganyika wanakuwa ni walalamishi wakati wa Zanzibar hawana tatizo na hilo labda tu nirudishe swali kwako ni nchi gani Muslim there happy in this world?

Na wapagani wana mahakama yao ya matambiko na haitambuliwi na katiba.
 
Katiba ya ccm ipo kwenye mfuko wa shati wa KINAna anasubiri tu mudondoshe karata zenu wooote!! Halafu ndio anafuta ya kwake na kuidondosha!!!!! Ntawakumbusha mtakapo tawanyika kwa njia 16 (idadi ya vyama vyetu vya upinzani) hivi munaijua ccm?munamfahamu vizuri KINAna ?

Zaidi ya Kashfa zinazomkabili ( kwa uchache meno ya Tembo na loliondo ) Kinana hana uwezo wowote wala jambo lolote la kumwezesha kuhujumu Katiba , na wala hakuna yeyote katika CCM mwenye uwezo huo ( hapa namaanisha hata JK ) , Vile wananchi watakavyotaka ndivyo itakavyokuwa , HIYO HUJUMA UNAYOISEMA SIYO RAHISI KAMA UNAVYODHANI ! We are Watching at a ZERO DISTANCE .
 
Last edited by a moderator:
Mzee Warioba hana jibu la hili na ndio maana mambo yenye utata tume yake wameyatupa kwenye mambo yasiyo ya Muungano, ili kama ni kuparurana basi waparurane wenyewe wakati yeye ameshamaliza kazi yake na ya kamati yake.

Kuhusu hili la Mahakama ya kadhi Waislamu kuradhimisha liingizwe kwenye katiba na igharamiwe na pesa za walipa kodi hapa CCM moja kwa moja inahusika kwa kuipanda mbegu hii ambayo hawakuyajuwa madhara yake.

Kanisa Katoliki nalo lina mahakama zake wanatumia Canon law lakini hakuna ulalamishi huu kwamba Canon law itambulike kikatiba wao wanaendesha mambo yao kimya kimya na ukienda kinyume kisa si ya kikatiba basi simple decision unatengwa na kanisa.

Hili la kuniuliza kwa nini Waislamu wa Tanganyika wanakuwa ni walalamishi wakati wa Zanzibar hawana tatizo na hilo labda tu nirudishe swali kwako ni nchi gani Muslim there happy in this world?

Point of correction: Siyo waislamu wote wenye hulka ya kulalamika.

Inawezekana ikawa ni kweli Mzee Warioba na tume yake wameamua kutokuingia kwenye marumbano ambayo yangechukua muda tena katika mchakato huu, hasa ikichukuliwa kama swala liko kwenye ilani ya uchaguzi wa chama kilichoko madarakani. wameamua Yangoswe kumwachie ngoswe mwenyewe.

Ingekuwa ni vizuri kama tungepata rasimu yote tukaisoma ili kupata picha kamili lakini vidokezo vinaashiria kwa ujumla rasimu ni nzuri.
 
Point of correction: Siyo waislamu wote wenye hulka ya kulalamika.

Inawezekana ikawa ni kweli Mzee Warioba na tume yake wameamua kutokuingia kwenye marumbano ambayo yangechukua muda tena katika mchakato huu, hasa ikichukuliwa kama swala liko kwenye ilani ya uchaguzi wa chama kilichoko madarakani. wameamua Yangoswe kumwachie ngoswe mwenyewe.

Ingekuwa ni vizuri kama tungepata rasimu yote tukaisoma ili kupata picha kamili lakini vidokezo vinaashiria kwa ujumla rasimu ni nzuri.
Mimi kama Mtanzania wa kawaida nimeridhika na hii rasimu japo bado hatujaipata yote infull, sintompa mwanasiasa yeyote nafasi ya kuniburuza katika mchakato huu.
 
Sasa mkuu mambo ya uchama yametokea wapi? Tume ina base nzuri sana ya utaifa zaidi. Achana na mambo ya uchama. Taifa kwanza mkuu.

Vizuri ukamwambia taifa lenyewe ni tanganyika.
 
Mimi kama Mtanzania wa kawaida nimeridhika na hii rasimu japo bado hatujaipata yote infull, sintompa mwanasiasa yeyote nafasi ya kuniburuza katika mchakato huu.

Muhimu kuliko yote taifa lako ni tanganyika sio tanzania tena.
 
"Mtakufa nyinyi, CCM mtaiacha". By J.M. Kikwete, mkutano mkuu, Dodoma.
 
Ndugu zangu wana jf,ni dhahiri kwamba rasimu ya katiba hii imekidhi haja za wengi,pia imetoa mbadala kwa wabunge na wanaharakati ndani ya chama cha mapinduzi,muda mrefu kundi hili limekuwa likibanwa na kukalipiwa na viongozi wa chama na hata kuchakachuliwa na NEC wakati wa uteuzi wa wagombea..kwa mwelekeo wa katiba hii ukiritimba wa NEC CCM hauna nguvu kwa sababu mwanachama atagombea bila kutegemea kuungwa mkono na chama lakini pia hata kama akiwa mbunge kupitia chama chake hataweza kuvuliwa ubunge wake au uongozi wowote kupitia chama hicho iwe kitongoji,mwenyekiti wa kijiji,diwani ama mbunge...kwa mantiki hiyo sioni sababu ya kuwapigia magoti akina kinana na kundi lao,pia nguvu ya NEC na makando kando yao sasa yamekwisha! Kwa awamu hii wananchi wamepewa mamlaka na si vyama vya siasa....Tutegemee kuvunjika kwa baadhi ya vyama vya siasa,lakini pia kwa vijana wanaotumika na wanasiasa watambua kuwa kwa sasa hawana msaada kama kubebwa kwenye vyama vyao---wananchi ndio waamuzi! Ahsanteni
 
kwa sasa vyama vitabaki na nguvu kuliko wagombea binafsi kwa sababu ya mitandao ya kiuongozi unaoenda mpaka chini.
 
Huyo anayesimama peke yake lazima awe na akili ya Mtikila tu.. vinginevyo unahitaji chama imara kama Chadema... ili ueleweke kwa wananchi... maana Nchi sio bustani ya mtu... kiongozi wa nchi anahitaji kuungwa mkono na walio chini yake ili naye aweze kutimiza matakwa ya waliomtuma.
 
Tume imependekeza ushindi wa kura za urais upatikane kwa zaidi ya 50%. Nadhani hapa walikuwa wamelewa pombe!! Wameruhusu utitiri wa wagombea binafsi na hivi inawezekana wagombea wa urais wakawa hata 15 au zaidi kama ilivyokuwa Ethiopia. Huko tuendako inawezekana kabisa hiyo 50% haitapatikana kirahisi. Je isipopatikana uchaguzi urudiwe? Na isipopatikana kwa mara ya pili je?!!! Hapa wangepaswa kusema: Ushindi wa simple majority..
 
Tume imependekeza ushindi wa kura za urais upatikane kwa zaidi ya 50%. Nadhani hapa walikuwa wamelewa pombe!! Wameruhusu utitiri wa wagombea binafsi na hivi inawezekana wagombea wa urais wakawa hata 15 au zaidi kama ilivyokuwa Ethiopia. Huko tuendako inawezekana kabisa hiyo 50% haitapatikana kirahisi. Je isipopatikana uchaguzi urudiwe? Na isipopatikana kwa mara ya pili je?!!! Hapa wangepaswa kusema: Ushindi wa simple majority..

raundi ya pili inahusu wagombea wawili tu wenye kura nyingi hivyo lazima mmoja atapata zaidi ya 50%
 
Back
Top Bottom