Kwa nini wanaume....................???

Kwa nini wanaume....................???

St. Paka Mweusi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2010
Posts
7,994
Reaction score
5,231
KWA NINI WANAUME/AKINA BABA WENGI WANAFIKIRI WAO NDIO WAAMUZI/WAFALME WA NYUMBA?



Suala hili limekuwa likinikera sana akilini mwangu kwa miaka mingi. Ya kwamba akina baba/wanaume wao wanafikiri kazi yao kubwa katika nyumba ni kuwa MUME/BABA basi. Mara nyingi utasikia wanasema mimi ndio mkubwa wa nyumba. Na kama wanafanya kazi za ofisini basi ndo itakuwa kero mno. Kwani hapa atataka anaporudi toka kazini akute chakula mezani, maji ya kuoga bafuni tena ya moto, nguo zmepigwa pasi n.k. Na kinyume kama hana kazi basi atakuwa anashinda kilabuni(UGIMBI) na akirudi toka huko basi ni kelele tu, hakuna amani wala maelewano

Bado naendelea, kuna wengine wanaona kupika, kulea watoto, kutafuta chakula ni kazi ya wanawake. Yaani hawawezi hata kujipikia chai kwa vile wao ni wanaume au hata kumbadili mtoto nepi, Mtoto amabaye ni wake. Kikubwa wanachofanya ni kukaa kitini/sofani na kuletewa kile wanachotaka. Wanasahau kabisha jambo la USAWA.

Bado wanaishi dunia ya mababu, mababu na mababuzi. Tuache UBINAFSI tuishi kwa kushirikiana/kusaidiana kwani wote ni SAWA. Nasema tena tuishi kwa kusaidiana hapo wote tutafurahia maisha. Tuache mambo ya UTUMWA

Na: Yasinta Ngonyani
 
Wewe ni jinsia gani?

Mbona siku hizi wanaume tunafanya mengi mno zaidi ya hayo....?

Mimi wife huwa nampelekea chai kwenye kitanda.....na kumfanyia massage juu...
 
KWA NINI WANAUME/AKINA BABA WENGI WANAFIKIRI WAO NDIO WAAMUZI/WAFALME WA NYUMBA?



Suala hili limekuwa likinikera sana akilini mwangu kwa miaka mingi. Ya kwamba akina baba/wanaume wao wanafikiri kazi yao kubwa katika nyumba ni kuwa MUME/BABA basi. Mara nyingi utasikia wanasema mimi ndio mkubwa wa nyumba. Na kama wanafanya kazi za ofisini basi ndo itakuwa kero mno. Kwani hapa atataka anaporudi toka kazini akute chakula mezani, maji ya kuoga bafuni tena ya moto, nguo zmepigwa pasi n.k. Na kinyume kama hana kazi basi atakuwa anashinda kilabuni(UGIMBI) na akirudi toka huko basi ni kelele tu, hakuna amani wala maelewano

Bado naendelea, kuna wengine wanaona kupika, kulea watoto, kutafuta chakula ni kazi ya wanawake. Yaani hawawezi hata kujipikia chai kwa vile wao ni wanaume au hata kumbadili mtoto nepi, Mtoto amabaye ni wake. Kikubwa wanachofanya ni kukaa kitini/sofani na kuletewa kile wanachotaka. Wanasahau kabisha jambo la USAWA.

Bado wanaishi dunia ya mababu, mababu na mababuzi. Tuache UBINAFSI tuishi kwa kushirikiana/kusaidiana kwani wote ni SAWA. Nasema tena tuishi kwa kusaidiana hapo wote tutafurahia maisha. Tuache mambo ya UTUMWA

Na: Yasinta Ngonyani
mkuu hawa viumbe hawaeleweki, unaweza ukawapa hiyo kampani wakakupakazia *b*w*e*g*e! mimi nazani hawa wadada wenyewe wa kibongo wana mentaliti hiyo hiyo ambayo unaidefend.
 
Wa kunyumba habari za leleno??? Uyumuike?? Pali pali penyewe hapo. Umeongea pointi sana wakunyumba.
Hawa wanaume bwana ukimwambia na wewe leo nipikie chai mungu wangu utatimuliwa kama kuku wa kienyeji
Eti oohhh umeanza dharau wewe eehhhh
Bwana wewe ukiongoea sana unapewa mistari ya Bibilia (Mungu alimuumba Adamu akapewa msaidizi wake Hawa tena toka kwenye ubavu wake) mwenyewe unanyamaza
 
Mimi mwenyewe nashangaa.
Wanaume mnataka kufanyiwa kila kitu.
 
mkuu hawa viumbe hawaeleweki, unaweza ukawapa hiyo kampani wakakupakazia *b*w*e*g*e! mimi nazani hawa wadada wenyewe wa kibongo wana mentaliti hiyo hiyo ambayo unaidefend.

Mnajishtukiaga tu kuwa mtaonekana mmewekwa kwenye kiganja cha mkono..Kusaidiana na partner wako siyo jambo baya wala jipya duniani..
 
mimi mwenyewe nashangaa.
Wanaume mnataka kufanyiwa kila kitu.

kila kitu?????
Tunawalipa mahari,,,
tunagharamia nyumba,
kula,kuvaa,
na mahitaji yote karibu,
wewe kupika na kupiga pasi unaona kazi?

Mbona wanaume wakupika na kufanya kazi za ndani wapo wengi,
kwanini msiende kwa hao?mfano wanaume wa commoro....
 
Mnajishtukiaga tu kuwa mtaonekana mmewekwa kwenye kiganja cha mkono..Kusaidiana na partner wako siyo jambo baya wala jipya duniani..
ukisaidia sana mpaka ukacross border hata yeye pia atakuzarau kuna majukumu yako feminine zaidi. najua hapa mnafurahisha tu lakini mnajielewa BJ bana. eniwei mbona ulipoteaga sana? au JF mpya hatuonani?
 
mkuu hawa viumbe hawaeleweki, unaweza ukawapa hiyo kampani wakakupakazia *b*w*e*g*e! mimi nazani hawa wadada wenyewe wa kibongo wana mentaliti hiyo hiyo ambayo unaidefend.



Hapo sasa mkuu, sijui tuwafanyie nini hawa wapinzani wetu...........
 
Mimi mwenyewe nashangaa.
Wanaume mnataka kufanyiwa kila kitu.

sio kila kitu bana, lakini acheni mwanaume aitwe mwanaume. kuna majukumu mwanaume akifanya haipendezi labda asaidie siku moja moja tu kwa zarura
 
Hapo sasa mkuu, sijui tuwafanyie nini hawa wapinzani wetu...........
tuwasaidie lakini kwa tahazari na mipaka. kuna rafiki angu mmoja hapa anamfanyia waifu wake kila kitu , yaani anajitahidi kweli in the name of love lakini mdada anawaambia washkaji nje eti mume wake anafanya yote yale kwa sababu anajua akimpoteza yeye hawezi kupata mrembo mwengine kma yeye dah! jamaa mpaka sasa hajaskia hizo taarifa lakini namuoneaga huruma kweli aisee
 
Wapo wanaume wa kicongo
wao wanaweza mpaka kuwapaka lips stick...
Wanafua na kupiga pasi nguo za ndani za wake zao...
Ili mradi mwanamke awe na pesa..
Sasa si muende kwa hao muache kulalamika humu....
 
ukisaidia sana mpaka ukacross border hata yeye pia atakuzarau kuna majukumu yako feminine zaidi. najua hapa mnafurahisha tu lakini mnajielewa BJ bana. eniwei mbona ulipoteaga sana? au JF mpya hatuonani?

Basi msaidie kwa kiasi ambacho mnakipima nyie wenyewe. Mie kweli naomba nipate mtu tusaidie na akikubaliana kuwa hiyo iwe katiba ya mji wetu basi hatutajali jamii inahisi vipi ni kuheshimiana na kushirikiana...Hebu msaidie mamaa na wewe!!
Nipo klorokwin, majukumu yalitinga pia likizo ya mwisho wa mwaka ilichangia mana mikiki mingi. Nimerejea na JF naona imetulia!!
 
ndo maana mimi kwa kulitambua suala hili la usawa nilitoa vigezo hakuna aliyeni-PM.......mimi shurti upike,upasi,ufanye usafi,uende sokoni,uogeshe watoto,ukawachukue shule etc......nikiwa na maana hayo ni majukumu yetu wote.....wewe ukitaka kutoka kazini uweke miguu kwa kiti,unadai kahawa sijui bites za kusubiria mlo wa jioni,utaumia....nasi tunafanya kazi na tunachoka....tusaidiane.......kuna ubaya gani kuwa ***** kwa mkeo.....si ndo mapenzi kusaidiana,nyie mwataka hadi mkimaliza tendo na kufutwa mfutwe....haloooooooooooo:laugh::laugh:
 
Nadhani huyu Yasinta Ngonyani, ameandika hii habari 30 years late...., hii ingebidi aitoe kwenye 70s au 80s, hata 90s angekuwa amechelewa.., she is living in the past
 
ndo maana mimi kwa kulitambua suala hili la usawa nilitoa vigezo hakuna aliyeni-PM.......mimi shurti upike,upasi,ufanye usafi,uende sokoni,uogeshe watoto,ukawachukue shule etc......nikiwa na maana hayo ni majukumu yetu wote.....wewe ukitaka kutoka kazini uweke miguu kwa kiti,unadai kahawa sijui bites za kusubiria mlo wa jioni,utaumia....nasi tunafanya kazi na tunachoka....tusaidiane.......kuna ubaya gani kuwa ***** kwa mkeo.....si ndo mapenzi kusaidiana,nyie mwataka hadi mkimaliza tendo na kufutwa mfutwe....haloooooooooooo:laugh::laugh:

honestly hili la kufutwa sikuwahi kuli demand...
sasa nitaanza kuli demand.kumbe tunahaki nyingi hivi?zingine sizijui lol
 
honestly hili la kufutwa sikuwahi kuli demand...
sasa nitaanza kuli demand.kumbe tunahaki nyingi hivi?zingine sizijui lol

Mna haki nyingi sana......yaani mno......hadi zimewazidi..........:laugh::laugh:
 
Mna haki nyingi sana......yaani mno......hadi zimewazidi..........:laugh::laugh:

sasa kama wewe mwenewe unakubali ni haki zetu,why complain?
kwa nini usiwe mpole na kuzitoa tu taratibu?
 
Back
Top Bottom