Kwa nini siku hizi hakuna miujiza kama Yesu alivyoagiza KWA wafuasi wake?

Kwa nini siku hizi hakuna miujiza kama Yesu alivyoagiza KWA wafuasi wake?

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
9,462
Reaction score
23,246
Wakatoriki ndio kabisaa hawataki kusikia hizi habari wao wamejielekeza zaidi kwenye mifumo yao ya kiibada basi.

Wasabato nao ni kama wamekatazwa kufanya eti KWA sababu Shetani atafanya na yeye miujiza bandia. Wamejikita kutaka Yesu arudi mapema.

Walokole badala ya miujiza wao wamejikita kwenye ushuhuda wa watu kifanyiwa miujiza sio miujiza. Ndio maana Polisi Kenya walimshikilia Pr aliyekuja na magongo mimbarini ya viwete waliopona wakimtaka awaonyeshe waliokuwa wanatumia hayo magongo.

Waislam wao wanafurahi tu kuona mtu amejiunga na dini yao na kusilimu kisha kuhudhuria Ibada. Mambo ya miujiza na matendo makuu ya Mungu kwanza hata kwenye Quran hayamo na Mtume hajawahi hata kufanya miujiza. Hivyo hawana morali ya kufanya hivyo.

Hakuna kupindi katika dunia ambacho kimekuwepo bila kuwepo watu wa Mungu wenye nguvu za Mungu. Naamini Hadi Sasa wapo.

Kwa nini licha ya msisimko mkubwa wa imani nchini tunaona uhaba mkubwa wa miujiza ya kimungu. Ha hata ikitokea ni ile ya kuungaunga na kulazimishia sio ile kama Petro na Yohana kilema anasomama watu wa kawaida na Serikali inashuhudia mubashara.


Ni hayo tu.

Nini maoni yako.
Mtumishi Matunduizi
 
Imani na nyumba za ibada imekuwa ni kichaka cha kufichia maovu, wengi wanahudhuria Kwa sababu ya mazoea na desturi...hiyo miujiza itatoka wapi?
 
Imani na nyumba za ibada imekuwa ni kichaka cha kufichia maovu, wengi wanahudhuria Kwa sababu ya mazoea na desturi...hiyo miujiza itatoka wapi?
Jamaa wanatukosesha MENGI sana.
Miujiza inanafasi yake hasa KWA yale ambayo SAYANSI na ubinadamu wetu umefikia kikomo.
 
Kama una imani katika Mungu hakika utaiona miujiza lakini kama huna kwako miujiza utaona ni mazingaombwe.Yesu aliwambia Siku ya tatu nitafufuka lakini hata wanafunzi wake walipata mashaka.Kwa hiyo imani katika Mungu ndiyo mhimu kuliko muujiza wenyewe kwani unaweza kuwa fake
 
Mmeruhusu ushoga,

Watu wanauwawa bila hatia na hakuna wa kukemea.
Dunia imekuwa mauwaji tu, dhulma na Viongozi wanacheka kwa kuwa wapo madarakani

Nani wa kuwatetea leo
Ishara zote mnaziona na matukio mnayaona ila mmekaa kimya tu
 
Kama una imani katika Mungu hakika utaiona miujiza lakini kama huna kwako miujiza utaona ni mazingaombwe.Yesu aliwambia Siku ya tatu nitafufuka lakini hata wanafunzi wake walipata mashaka.Kwa hiyo imani katika Mungu ndiyo mhimu kuliko muujiza wenyewe kwani unaweza kuwa fake
Hatuioni mkuu. Waigizaji watu wa hypnosis, manipulations, astral projections, mind programing na social psychologists na wasanii ndio wanatamba madhabahuni. Wale real jamii imeanza kuwamiss.
 
Mmeruhusu ushoga,

Watu wanauwawa bila hatia na hakuna wa kukemea.
Dunia imekuwa mauwaji tu, dhulma na Viongozi wanacheka kwa kuwa wapo madarakani

Nani wa kuwatetea leo
Ishara zote mnaziona na matukio mnayaona ila mmekaa kimya tu
Wakiingia kwenye siasa, kupinga au kuunga mkono harakati za kisiasa ndio hata hii feki itapotea kabisa.
 
Back
Top Bottom