Kwa nini kuna madaraja ya watu katika dini?

Kwa nini kuna madaraja ya watu katika dini?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
57,707
Reaction score
91,649
Kwa nini Kanisani na misikitini viongozi wakubwa na matajiri hupewa umuhimu, kipaumbele au nafasi za mbele zaidi ikiwa kwa mungu watu wote ni sawa? Mfano RC kuna kitu kinaitwa Wakatoliki wa nguvu.Wiki hii Padri Kitima akiwa Bariadi kwenye shughuli ya kusimikwa Askofu aliwaita jukwaani Wakatoliki wa nguvu, Jenerali Mabeyo, Andrew Chenge(ambaye ni fisadi mmojawapo wa pesa za escrow) na jaji Mihayo wawasalimie maaskofu.

Kwenye Uislamu nako mbinguni au jannah zipo za madaraja tofauti kwa hiyo muislamu usitegemee sana ukifa au baada ya kiama kwamba utaenda kukaa mbingu moja na Nabii Ibrahim au mtume Muhamad, pia hatujui kama ahadi ya idadi mabikira itakuwa sawa mbingu zote, huenda wengine wakapata wachache zaidi.
 
Imeandikwa kuwa Petro alipewa Ufunguo kuwa atakacho kifungua duniani atakuwa amekifungua mbinguni. Vile vile atakachokifunga duniani atakuwa amekifunga mbinguni.

Ni kuwa ukiukata duniani na hata mbinguni utaukata. Ukiwa mlalahoi hapa duniani, hata kule mbinguni utakuwa nakadhalika. Yoda ukiwa wa Kulalamika lamamika hapa duniani, hata kwake ni gale gale . Kumbuka vyote hutoka kwa Mungu, mtu anaendesha V8 na wewe unapiyanga kwa mguu ni alama ya yajayo. Wateule ni wachache
 
Imeandikwa kuwa Petro alipewa Ufunguo kuwa atakacho kifungua duniani atakuwa amekifungua mbinguni. Vile vile atakachokifunga duniani atakuwa amekifunga mbinguni.

Ni kuwa ukiukata duniani na hata mbinguni utaukata. Ukiwa mlalahoi hapa duniani, hata kule mbinguni utakuwa nakadhalika. Yoda ukiwa wa Kulalamika lamamika hapa duniani, hata kwake ni gale gale . Kumbuka vyote hutoka kwa Mungu, mtu anaendesha V8 na wewe unapiyanga kwa mguu ni alama ya yajayo
Sitaki kuamini Andrew Chenge ni Mkatoliki wa nguvu kuliko Wakatoliki wengine, labda ungesema Papa au Askofu.
 
Mungu hana upendeleo ila cha ajabu sasa Mungu kaleta dini kwa kiarabu mm msukuma lazima niswali kwa kirabu na pia lazima nibinue kishindu kueelekea kibra sijui mecca... ila waafrica tulipigwa vibaya dah mpaka huruma
 
Imeandikwa kuwa Petro alipewa Ufunguo kuwa atakacho kifungua duniani atakuwa amekifungua mbinguni. Vile vile atakachokifunga duniani atakuwa amekifunga mbinguni.

Ni kuwa ukiukata duniani na hata mbinguni utaukata. Ukiwa mlalahoi hapa duniani, hata kule mbinguni utakuwa nakadhalika. Yoda ukiwa wa Kulalamika lamamika hapa duniani, hata kwake ni gale gale . Kumbuka vyote hutoka kwa Mungu, mtu anaendesha V8 na wewe unapiyanga kwa mguu ni alama ya yajayo. Wateule ni wachache
We jamaa bhana,Kwa hiyo Sisi walala hoi na mbinguni tutakuwa tiamaji tiamaji hivyohivyo??
 
We jamaa bhana,Kwa hiyo Sisi walala hoi na mbinguni tutakuwa tiamaji tiamaji hivyohivyo??
Hata mimi mlalahoi, nami huko mbinguni ni gale gale ila wewe mwenzangu, huwezi jua maana kesho unaweza fikiwa na zali la mentali ukawa mchepuko wa Mo, ukauaga ulalahoi (you never know with ladies)! Sie wanaume ndivyo hiyo, tunabook kisehemu motoni tu. Kisa ule Ufunguo aloopewa Petro ambaye Siku hizi mwakilishi ni Mmarekani anaitwa Leo wa 14
 
Back
Top Bottom