Marlex Jr El
JF-Expert Member
- Nov 6, 2015
- 1,819
- 2,413
Kwa Tanzania labda raisi afariki kabla ya mwisho wa msimu wake... Lakin kuhusu bunge kumwondoa labda shetani awe malaika
Mkianzisha huu mchakato wa uasi basi Rais anayo mamlaka ya kulivunja bunge ndani ya dakika tuuu.hahahahahaha kwisha habari yenu................Ibara ya 46A YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, 1977; INAYOHUSU KUMUONDOA MADARAKANI (IMPEACHMENT) RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 [Cap. 2 R.E. 2002.]
ZOEZI HILI HUCHUKUA JUMLA {KAMA KILA KITU KINAKWENDA SAWA - ceteris paribus} YA SIKU 150 au miezi mitano. Kwa mfano huu mchakato ukianza leo, mwezi wa tano Raisi anakuwa kaondolewa.
Rais (Mhimili wa Utawala) anaweza kuondolewa madarakani chini ya Ibara hii kwa tuhuma za aina nne:
- kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.
- Kukiuka Sheria ya Maadili ya Viongozi [Leadership Code]
- Kukiuka vipengele vilivyomo katika maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya Siasa yaliyotajwa katika Ibara ya 20 (2) ya Katiba, au
- Amekuwa na mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
1. Ili kuanzisha mchakato huo inahitaji idadi ya asilimia 20 (20%) ya Wabunge waliopo wafikishe Notisi ya maandishi na kuiwasilisha kwa Spika. Siku 30 zipite kabla ya kikao cha kujadili hizo tuhuma: ( wabunge wa CDM pekee wanatosha kufika 20% (
2. Baada ya kupita hizo siku 30, MTOA HOJA ATAIWASILISHA BUNGENI.
-Aidha tuhuma zitupwe au
- Wapendekeze kuunda Kamati ya Kuchunguza tuhuma hizo.
3. Bunge litapiga kura ili iundwe Kamati ya Kuchunguza tuhuma hizo; lakini kura hizo lazima zifikie au zizidi theluthi mbili ya kura zote. Kama ndio,
4. Spika anatakiwa kutaja majina ya Kamati ya Uchunguzi chini ya Ibara ya 46A(4) ambao ni:
(a) Jaji Mkuu (Mwenyekiti)
(b) Jaji Mkuu wa Zanzibar
(c) Wajumbe saba wanaoteuliwa na Spika; kwa kuzingatia Kanuni za Bunge na Uwakilishi wa Vyama vya Siasa Bungeni.
Matokea ya No. 3 hapo juu chini ya Ibara 46A (5) ni kwamba
- RAis anasimamishwa kazi
- Vivyo Ibara ya 37 (3) inafanya kazi. (Edapo Rais hatakuwepo madarakani wakati huo)
Jambo hili la kumsimamisha kazi Rais litaendelea hadi hapo Spika atakapomfahamisha Rais juu ya matokeo ya uchunguzi uliofanywa [Ibara ya 46A (5)]
Na. 4 hapo juu Kamati inapewa siku 7 kukamilisha uchunguzi wake na kumpa fursa Rais ya kujieleza [Ibara ya 46A (6)]
Kamati ya uchunguzi inapewa siku 90 kukamilisha ripoti yake na kuiwasilisha kwa Spika.
Ibara ya 46A (8) - Spika anawasilisha Ripoti ya Uchunguzi kwa Bunge
Ibara ya 46A (9) - Bunge lenye idadi isiyopungua theluthi mbili litajadili Ripoti hiyo na kumpa Rais fursa ya kujieleza.
Bunge linatakiwa liibuke na aidha ya majibu yafuatayo:
(i) Kwamba tuhuma zimethibitishwa.
(ii) Kwamba Rais hafai kuendelea kufanya kazi
(iii) Kwamba Rais hafai kuwa Rais
(iv) Kwamba tuhuma hazikuthibitishwa.
Ibara 46A(10) - Baada ya hilo kufanyika, endapo ni (i) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatakiwa kuachia ngazi (resign) ndani ya siku tatu.
MCHAKATO HUO WOOOOTE ULIOTAJWA HAPO JUU UKIFUATAWA KAMA UNAVYOTOLEWA kisheria unatakiwa kumalizika ndani ya siku 150 sawa sawa na miezi 5 kamili.
Nilikuwa sijui. Nilidhani watu wanatoa mawazo yao kutoka mioyoni mwao. Kumbe wanandikiwa wapost. Du. Kali. Wajue wajue rais mwingine ataapishwa mwaka 2025 baada ya uchaguzi wa kawaida wa 2020.Naanza kupata hisia
Humu ndani kuna watu wanalipwa na yule bwana mwenye uchu wa kuingia ikulu
Tuwe makini sana
Maana moja ya mikakati yake siku zote
Ni kununua vyombo ya habari
Haiwezekani mh Rais anajitahidi kufanya kazi kubwa
Ila watu wachache wao ni kukosoa tu kila kitu
kwani hamna kazi zingine za kufanya?,si wana mitaji,watashindwa kweli hata kufungua streetcorner shop na maisha yakaenda?,hahaa umenichekesha sana mleta uzi hii kitu haijitokea kwa wabunge wabongo maana wakimuondoa raisi nao ina bidi waondoke bunge linavunjwa sasa hawa wabunge wetu wanaoshinda uchaguzi kwa ngekewa unahisi wanaujasiri wa kufanya hivo maana ukiitishwa uchaguzi mwingine ni wabunge wachache watarudi mjengoni ,sasa ni mbunge gani atajitoa sadaka kwa hilo?
Ila sio bunge hili la Tz, bunge liko divided yaani hata sasa wakipiga kura unajua sisiemu wana ngapi na ukawa wana ngapi! Bado sana.
Nini malengo ya kuleta mada hii hapa? Acha ujinga wewe. Mlishindwa kwa kura ndio mnafikiria njia za kipuuzi hizo?
anaongelea bunge la uchagganiUnaongelea Bunge lipi kwanza? hili la Tanzania au la Kufikirika?
Ww ndiyo mbumbumbu kabisa hujui kwamba rais anaweza kulivunja bunge ? Au ni wale wanaolipwa na yule anaetaka urais kwa gharama yoyote ili mjitoe ufahamu mlopoke ovyo ? Iko kaziRaisi hana mamlaka ya kuvunja Bunge
Ukiitwa Takukuru Unaweza kulitolea ushahidi?wabunge wa CCM ambao ndiyo majority wamepewa rushwa miliion 10 kila mmoja
Mngeanza kumtoa mbowe katika kiti alichokalia kwanza.Ibara ya 46A YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, 1977; INAYOHUSU KUMUONDOA MADARAKANI (IMPEACHMENT) RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 [Cap. 2 R.E. 2002.]
ZOEZI HILI HUCHUKUA JUMLA {KAMA KILA KITU KINAKWENDA SAWA - ceteris paribus} YA SIKU 150 au miezi mitano. Kwa mfano huu mchakato ukianza leo, mwezi wa tano Raisi anakuwa kaondolewa.
Rais (Mhimili wa Utawala) anaweza kuondolewa madarakani chini ya Ibara hii kwa tuhuma za aina nne:
- kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.
- Kukiuka Sheria ya Maadili ya Viongozi [Leadership Code]
- Kukiuka vipengele vilivyomo katika maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya Siasa yaliyotajwa katika Ibara ya 20 (2) ya Katiba, au
- Amekuwa na mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
1. Ili kuanzisha mchakato huo inahitaji idadi ya asilimia 20 (20%) ya Wabunge waliopo wafikishe Notisi ya maandishi na kuiwasilisha kwa Spika. Siku 30 zipite kabla ya kikao cha kujadili hizo tuhuma: ( wabunge wa CDM pekee wanatosha kufika 20% (
2. Baada ya kupita hizo siku 30, MTOA HOJA ATAIWASILISHA BUNGENI.
-Aidha tuhuma zitupwe au
- Wapendekeze kuunda Kamati ya Kuchunguza tuhuma hizo.
3. Bunge litapiga kura ili iundwe Kamati ya Kuchunguza tuhuma hizo; lakini kura hizo lazima zifikie au zizidi theluthi mbili ya kura zote. Kama ndio,
4. Spika anatakiwa kutaja majina ya Kamati ya Uchunguzi chini ya Ibara ya 46A(4) ambao ni:
(a) Jaji Mkuu (Mwenyekiti)
(b) Jaji Mkuu wa Zanzibar
(c) Wajumbe saba wanaoteuliwa na Spika; kwa kuzingatia Kanuni za Bunge na Uwakilishi wa Vyama vya Siasa Bungeni.
Matokea ya No. 3 hapo juu chini ya Ibara 46A (5) ni kwamba
- RAis anasimamishwa kazi
- Vivyo Ibara ya 37 (3) inafanya kazi. (Edapo Rais hatakuwepo madarakani wakati huo)
Jambo hili la kumsimamisha kazi Rais litaendelea hadi hapo Spika atakapomfahamisha Rais juu ya matokeo ya uchunguzi uliofanywa [Ibara ya 46A (5)]
Na. 4 hapo juu Kamati inapewa siku 7 kukamilisha uchunguzi wake na kumpa fursa Rais ya kujieleza [Ibara ya 46A (6)]
Kamati ya uchunguzi inapewa siku 90 kukamilisha ripoti yake na kuiwasilisha kwa Spika.
Ibara ya 46A (8) - Spika anawasilisha Ripoti ya Uchunguzi kwa Bunge
Ibara ya 46A (9) - Bunge lenye idadi isiyopungua theluthi mbili litajadili Ripoti hiyo na kumpa Rais fursa ya kujieleza.
Bunge linatakiwa liibuke na aidha ya majibu yafuatayo:
(i) Kwamba tuhuma zimethibitishwa.
(ii) Kwamba Rais hafai kuendelea kufanya kazi
(iii) Kwamba Rais hafai kuwa Rais
(iv) Kwamba tuhuma hazikuthibitishwa.
Ibara 46A(10) - Baada ya hilo kufanyika, endapo ni (i) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatakiwa kuachia ngazi (resign) ndani ya siku tatu.
MCHAKATO HUO WOOOOTE ULIOTAJWA HAPO JUU UKIFUATAWA KAMA UNAVYOTOLEWA kisheria unatakiwa kumalizika ndani ya siku 150 sawa sawa na miezi 5 kamili.
Kuzuia mikutano ya siasa na maandamano ..kavunja au hajavunja katiba.... Jibu kwanzaMTOA MADA NDOTO HIZO HAZIWEZI KUTIMIA, NI WEWE TU AMBAYE HUIONI KAZI ANAYOIFANYA RAIS ,ILA WATANZANIA TUNAMKUBALI , UTABAKIA KULALAMA TU ,FANYA KAZI ACHA POROJO NA MAWAZO HASI
Mikutano na maandamano yenye tija gani kwa jamii? Bora azuie watu wafanye kazi. Tumechoka watoto wetu kuwa vilema kwa sababu za kijinga!!Kuzuia mikutano ya siasa na maandamano ..kavunja au hajavunja katiba.... Jibu kwanza
Wabunge wa upinzani wa raise motion ya impeachment ingawa wako wachahe lakini let it be on record!Katiba inalipa bunge fursa ya kumwondoa mtu huyu madarakani kabla ya muda wake kama anajifanya "kichwangumu"
Si lazima iwe 2020