"Kwa mshahara huu, CCM isitafute mchawi" ni title mbaya kwa hii thread. Watu hatuikatai CCM kwa sababu ya maslahi ya wafanyakazi sekta yoyote ile. Ni kweli maslahi ya wafanyakazi si jambo la kupuuza lakini msingi mkuu CCM haipaswi kuendelea kukaa madarakani ni mfumo mbovu sana wa uongozi na kisera unaosababisha inequalities na uduni wa tija katika jamii yote ya watanzania na katika sekta zote.
Leo hii sekta ya Kilimo inaonekana kulipa kimaslahi, lakini kilimo ndio kimeonekana kuwa na tija kwa wakulima wenyewe? Last I checked wakulima wengi ni watu duni sana na Tanzania bado haijajitosheleza kwa chakula.
Sekta ya afya ndo hivyo hivyo pia. Maslahi ya madaktari na wahudumu wa afya hakupelekei huduma bora kwa wagonjwa katika hospitali za umma.
Argument yangu ni kwamba mindset zetu sisi wafanyakazi ziende mbali zaidi na kutunisha matumbo yetu. Na inaonekana sisi wafanyakazi ndo tunarudisha nyuma harakati za mabadikiliko ya nchi hii. Tunaihukumu CCM tu kwa sababu haijaongeza mishahara. Ikifika 2015 wajinga wajinga fulani wa CCM wakistrategize tu kwamba pandisheni mishahara ya wafanyakazi asilimia 100 ili tupate kura, na kwa vile akili zetu ni fupi zinaangalia tumbo, tunasahau kwamba matatizo yetu si matumbo bali ni kuona maisha bora ya watanzania katika mfumo wa ushindani wa kiuchumi, kisayansi, kiteknolojia, kiafya, kilimo, na kadhalika.
Mshahara wangu hata ukiwa mkubwa kiasi gani, nina watoto wangu watahitaji huduma bora ambazo hazitegemei mshahara wangu. Wakienda shuleni au hospitalini au sokoni au popote pale watahitaji kupata huduma bora inayotokana na mfumo bora uliojengwa kwa sera sahihi, uongozi sahihi na weledi sahihi. CCM hawana maono hayo wao akili zao ni za miaka mitano mitano tu, tunahitaji maono ya miaka 100.