Earthmover
JF-Expert Member
- Sep 28, 2012
- 22,756
- 19,989
....Club ya Chelsea ilipofanya vibaya viongozi wake waliwajibishwa ,pia Arsenal viongozi wake waliwajibishwa na sasa hizo timu zinafanya vizuri baada ya kuingia uongozi mpya.
Uongozi ni dhamana na uongozi ni matokeo ,kama uongozi wako umekosa ubunifu na unaleta matokeo yanayotishia uhai wa taasisi unayoiongoza ,basi kiungwana tu unatakiwa kuachia ngazi mara moja kupisha mabadikiko chanya.
Binafsi sina chuki yoyote na kiongozi wa sasa wa chadema. ,Ila tu kwa hali ilipofikia viongozi wote wa juu wa chadema waachie ngazi mara moja . Wachaguliwe viongozi wapya wa kukivusha chama
Kwa sasa tangu chaguzi za marudio zianze ,Chadema imeshinda kata moja tu huku ikipoteza mamia ya kata na majimbo mengi..
Hii siyo sawa na jambo hili haliwezi kupita kimyakimya bila kujadiliwa.
......NYANOKOKONOUKE