Kwa mara ya kwanza Tsh Milioni 350 imeingia kwenye account

Pesa ni ya Urithi! Afu bado tena unatutukania wazee wetu!
We jamaa Wewe japo sina kiwango icho cha pesa ila nakuonea huruma sana! Na Wewe bado ni Masikini zaidi yangu.
 
Milioni 350 ya urithi inakupa jeuri ya kutukana watu hata huwajui na matusi yako based na hisia kuwa Baba zao walikimbia umande na waliendekeza ngono?

Wewe bado sio tajiri na hiyo mentality itaku cost very soon
Nijuavyo hela inayodumu ni ile iliyopatikana baada ya kuitafuta kwa mipangilio na mikakati yako mwenyewe, kwani utajua namna ya kuizalisha, lakini kama imekuja bila mipangilio, hiyo itaondoka bila mipangilio.
 
ili usifirisike inabidi utenge 50M za kula bata na wanawake ili uzizoeee...Halafu hiyo 300M ndio unafanyia mambo ya maana.
Hiyo pesa ni nyingi Sana sio yakuisha leo kama pesa nyingine atafanya uwekezaji ungemshauri vyema jamaa bado anaushamba utamcost
 
Tumpe ndugu yetu mwongozo ulio mwema yaani watu wanamchuria mabaya tu dah ngozi nyeusi bana
Tatizo katukana wazazi wa wenzie akiamini kwa vile hawana basi hawakusoma na niwapenda ngono na hapo ndipo alipo ununua ugomvi

unaweza kuta huyo mzazi wake alikuwa mwizi wa mali za watu au mdhurumaji wa mali za wengine
 
Tatizo katukana wazazi wa wenzie akiamini kwa vile hawana basi hawakusoma na niwapenda ngono na hapo ndipo alipo ununua ugomvi

unaweza kuta huyo mzazi wake alikuwa mwizi wa mali za watu au mdhurumaji wa mali za wengine

Mnajieleza sana mkuu, huyu ni kunyamaza kimya na kumpa muda tu. Ni wachache sana, kama wapo wanaopata pesa nyingi ya ghafla wakaitunza, wakaizalisha na ikaongezeka, kama wapo lakini.
 
Mnajieleza sana mkuu, huyu ni kunyamaza kimya na kumpa muda tu. Ni wachache sana, kama wapo wanaopata pesa nyingi ya ghafla wakaitunza, wakaizalisha na ikaongezeka, kama wapo lakini.
Hekima inasema tumuongoze aende vyema pia elewa kwa hesabu za haraka huyu ni bado kijana mdogo, haijui fedha vizuri, haijui kama mda huu wanga na wachawi wameshaanza kumpiga vyuma vya nguvu ili apotee njia wanga wengine ni best friends wake kindakindani, kijana #msweden nunua majengo hutajuta usijimwambafai hata kidogo kwani hapo ulipo tayari washakupiga mrogo na si mmoja.
 
Wabarikiwe wazee waliojipinda kutafuta mali na kupiga kitabu kwa sana, leo hii wajukuu tunakula matunda yenu na sisi wajukuu tunapambana kwa jasho na damu kutafuta mali ili wajukuu zetu waje kula matunda ya Babu zao wasije kuishi kwa shida.

Poleni kwa wale ambao wazee/Babu zenu walikimbia shule ingawa walikuwa na utajiri wa ardhi Mwenge, Oysterbay, Masaki ila waliendekeza ngono wakauza ardhi yote, wao wamekufa wajukuu mmeachiwa msala mnakula msoto na bahasha mkononi. Pole sana

Mjifunze muanze kupambana muwatengenezee njia wajukuu wenu.
...Mbona Kichwa Habari Cha Thread ni tofauti na Thead yenyewe??
 
Milioni 350 ya urithi inakupa jeuri ya kutukana watu hata huwajui na matusi yako based na hisia kuwa Baba zao walikimbia umande na waliendekeza ngono?

Wewe bado sio tajiri na hiyo mentality itaku cost very soon
Tena very very soon
 
Back
Top Bottom