Hivi mwaka 1992, huo unaolalamikiwa kuwa na MOU kati ya serikali na kanisa ulikuwa chini ya utawala wa nani ?
Pia, kuna haja gani kumjadili Nyerere mtu ambaye Mungu alishamchukua ( Amlaze mahali pema peponi, na njia yetu ni moja), alituanzishia mchakato, katika moja ya speech zake nilisikia akisema hivi: " ... msipoteze muda mwingi kujadili makosa yetu, ... wakati sisi tunachukua nchi hii kutoka kwa wakoloni, wasomi tulikuwa wachache, hivyo tusingeweza kufanya mambo yote sawa kwa ubora unaotakiwa kwa Tanzania nzima, ... tunaomba mjadili yale mazuri machache tuliyofanya, ... na katika yale mnayoona tulifanya sivyo, kwa wingi wenu, na wasomi wengi mlionao, muyatengenezee mkakati wa kuyarekebisha, ... na lengo lenu liwe ni kuendeleza yale mazuri tuliyofanya, na kurekebisha pale tulipokosea, ili mweze kusonga mbele ...." sitaweza kunukuu kila neno, but atleast nimeweza kunukuu baadhi ya maneno na hasa maana. Alipiga vita udini, alipigania usawa, hata kama hakuweza kwa 100%, naomba tumwenzi kwa yale machache aliyoweza kufanya. Labda niwaambie kitu: WAKATI WA MWINYI HATUJAONA MTU ALIYEMSEMA VIBAYA BABA WA TAIFA, WAKATI WA MKAPA PIA HATUJAONA, LAKINI WAKATI WA JK WATU WAMETUKANA NA KUSEMA SANA OVYO KUHUSU BABA WA TAIFA, Why ? why ? why ? ni CCM na Ukatoliki ? ni CCM na CDM ? ni CDM na ukatoliki? ni Uislam na Ukristu ? tuendelee kubaki kwenye hoja ya mtoa mada, WHAT IS OUR WAY FORWARD ?